Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 57.6

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 57

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 56 Chapitre 58

Confiance dans la difficulté

1 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi, Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe. Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako, Hata misiba hii itakapopita.
2 Nitamwita MUNGU Aliye juu, Mungu anitimiziaye mambo yangu.
3 Atapeleka toka mbinguni na kuniokoa, Atukanapo yule atakaye kunimeza. Mungu atazipeleka Fadhili zake na kweli yake
4 Nafsi yangu i kati ya simba, Nitastarehe kati yao waliowaka moto. Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, Na ndimi zao ni upanga mkali.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.
6 Wameweka wavu ili kuninasa miguu; Nafsi yangu imeinama; Wamechimba shimo mbele yangu; Wametumbukia ndani yake!
7 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, Moyo wangu u thabiti. Nitaimba, nitaimba zaburi,
8 Amka, utukufu wangu. Amka, kinanda na kinubi, Nitaamka alfajiri.
9 Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
10 Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni, Na uaminifu wako hata mawinguni.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 57.6 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.