Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 48.13

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 48

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 47 Chapitre 49

La beauté de Sion

1 Bwana ndiye aliye mkuu, Na mwenye kusifiwa sana. Katika mji wa Mungu wetu, Katika mlima wake mtakatifu.
2 Kuinuka kwake ni mzuri sana, Ni furaha ya dunia yote. Mlima Sayuni pande za kaskazini, Mji wa Mfalme mkuu.
3 Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika; Walipita wote pamoja.
5 Waliona, mara wakashangaa; Wakafadhaika na kukimbia.
6 Papo hapo tetemeko liliwashika, Utungu kama wa mwanamke azaaye.
7 Kwa upepo wa mashariki Wavunja jahazi za Tarshishi.
8 Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, Katika mji wa Bwana wa majeshi. Mji wa Mungu wetu; Mungu ataufanya imara hata milele.
9 Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, Katikati ya hekalu lako.
10 Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. Mkono wako wa kuume umejaa haki;
11 Na ufurahi mlima Sayuni. Binti za Yuda na washangilie Kwa sababu ya hukumu zako.
12 Tembeeni katika Sayuni, Uzungukeni mji, Ihesabuni minara yake,
13 Tieni moyoni boma zake, Yafikirini majumba yake, Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.
14 Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 48.13 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.