Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Juges 17
Bible en Swahili de l’est


La déchéance morale d’Israël

Instauration d’un culte idolâtrique

1 Wakati huo alikuwako mtu mmoja wa nchi ya vilima ya Efraimu, ambaye jina lake alikuwa akiitwa Mika.
Juges 10.1 Juges 18.2 Josué 15.9 Josué 17.14-17.18
2 Naye akamwambia mama yake, Hizo fedha elfu na mia moja ulizonyang’anywa, ambazo uliweka kiapo kwa ajili yake na kusema masikioni mwangu, tazama, ninazo mimi hizo fedha; ni mimi niliyezitwaa. Mama yake akasema, mwanangu na abarikiwe na Bwana.
Néhémie 13.25 Ruth 3.10 Genèse 14.19 Genèse 24.30-24.31 Juges 5.23
3 Basi akamrudishia mama yake hizo fedha elfu na mia moja. Mama yake akasema, Mimi naziweka fedha hizi kabisa ziwe wakfu kwa Bwana, zitoke mkononi mwangu kwa ajili ya mwanangu, ili kufanya sanamu ya kuchonga, na sanamu ya kusubu; basi kwa hiyo nakurudishia wewe.
Exode 20.4 Lévitique 19.4 Exode 20.23 Jérémie 10.3-10.5 Jean 16.2
4 Basi hapo alipomrudishia mama yake hizo fedha, mama yake akatwaa fedha mia mbili, akampa fundi mwenye kusubu fedha, naye akafanya sanamu ya kuchonga kwazo, na sanamu ya kusubu; ambazo zilikuwa ndani ya nyumba ya Mika.
Jérémie 10.9-10.10 Esaïe 46.6-46.7
5 Basi mtu huyo Mika alikuwa na nyumba ya miungu, naye akafanya naivera, na kinyago, akamweka wakfu mmoja miongoni mwa wanawe, akawa kuhani wake.
Genèse 31.19 Juges 18.14 Juges 8.27 Genèse 31.30 Juges 18.24
6 Siku hizo hapakuwa na mfalme katika israeli; kila mtu alifanya hayo aliyoyaona kuwa ni mema machoni pake mwenyewe.
Juges 18.1 Juges 19.1 Juges 21.25 Deutéronome 12.8 Proverbes 14.12
7 Alikuwako mtu mmoja hirimu aliyetoka Bethlehemu-yuda, wa jamaa ya Yuda, aliyekuwa ni Mlawi, naye akakaa huko hali ya ugeni.
Michée 5.2 Ruth 1.1-1.2 Matthieu 2.1 Matthieu 2.5-2.6 Genèse 35.19
8 Mtu huyo akatoka katika huo mji, katika Bethlehemu-yuda, ili aende kukaa hali ya ugeni hapo atakapoona mahali; akafikilia nchi ya vilima vilima ya Efraimu katika safari yake, hata nyumba ya huyo Mika.
Josué 24.33 Juges 17.11 Néhémie 13.10-13.11
9 Mika akamwuliza, Watoka wapi wewe? Akamwambia, Mimi ni Mlawi wa Bethlehemu-yuda, nami naenda kukaa hali ya ugeni po pote nitakapoona mahali.
10 Mika akamwambia, kaa pamoja nami, uwe kwangu baba, tena kuhani, nami nitakupa fedha kumi mwaka kwa mwaka, na nguo ya kuvaa, na vyakula. Basi huyo Mlawi akaingia ndani.
Jean 12.6 2 Rois 6.21 1 Pierre 5.2 1 Timothée 6.10 Juges 18.19-18.20
11 Huyo Mlawi aliridhika kukaa na mtu huyo; kisha huyo hirimu akawa kwake kama wanawe mmojawapo.
12 Basi Mika akamweka wakfu huyo Mlawi, huyo hirimu, naye akawa kuhani wake, akakaa nyumbani mwa Mika.
Juges 18.30 1 Rois 12.31 Nombres 16.5 1 Rois 13.33-13.34 Nombres 16.8-16.10
13 Ndipo Mika akasema, Sasa najua ya kwamba Bwana atanitendea mema, kwa kuwa nina Mlawi kuwa kuhani wangu.
Proverbes 14.12 Matthieu 15.13 Actes 26.9 Esaïe 44.20 Jean 16.2

Cette Bible est dans le domaine public.