Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Jean 1.4
Bible en Swahili de l’est


Introduction : la parole de vie

1 Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;
Jean 20.27 Actes 4.20 1 Jean 4.14 Luc 24.39 Jean 5.26
2 (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu);
1 Jean 3.8 1 Jean 5.20 Jean 1.4 1 Jean 3.5 Jean 17.3
3 hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.
1 Jean 1.1 1 Corinthiens 1.9 Philippiens 2.1 Jean 17.21 Jean 17.3
4 Na haya twayaandika, ili furaha yetu itimizwe.
Jean 15.11 Jean 16.24 1 Jean 2.1 Jean 3.29 2 Jean 1.12

La vie dans la lumière

5 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.
Jean 8.12 Jacques 1.17 Psaumes 27.1 Esaïe 60.19 1 Timothée 6.16
6 Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli;
1 Jean 4.20 1 Jean 1.10 Jean 3.19-3.21 1 Jean 2.4 2 Corinthiens 6.14-6.16
7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
Apocalypse 1.5 Romains 13.12 Ephésiens 1.7 Ephésiens 5.8 1 Timothée 6.16
8 Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
1 Jean 2.4 Jacques 3.2 Romains 3.23 Esaïe 53.6 Job 15.14
9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
Psaumes 32.5 Proverbes 28.13 1 Jean 1.7 Psaumes 51.2-51.5 Jérémie 33.8
10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.
1 Jean 5.10 1 Jean 1.8 Psaumes 130.3 1 Jean 2.14 Job 24.25

Cette Bible est dans le domaine public.