Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 5.12
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa, wafalme wa Waamori, waliokaa ng’ambo ya Yordani pande za magharibi, na wafalme wote wa Wakanaani, waliokuwa karibu na bahari, waliposikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya Yordani mbele ya wana wa Israeli, hata tulipokwisha kuvuka, basi mioyo yao iliyeyuka, wala haikuwamo roho ya nguvu ndani yao tena; kwa ajili ya wana wa Israeli.
Nombres 13.29 Josué 2.9-2.11 1 Rois 10.5 Josué 24.15 Genèse 48.22

Circoncision et célébration de la Pâque

2 Wakati huo Bwana akamwambia Yoshua, Haya, jifanyie visu vya mawe ya gumegume, watahiri tena wana wa Israeli mara ya pili.
Exode 4.25 Genèse 17.10-17.14 Deutéronome 10.16 Colossiens 2.11 Deutéronome 30.6
3 Basi Yoshua akajifanyia visu vya mawe ya gumegume, akawatahiri wana wa Israeli huko Gibea-haaralothi.
Matthieu 16.24 Genèse 17.23-17.27
4 Na sababu ya Yoshua kutahiri ni hii; watu wote waliotoka Misri, waliokuwa waume, hao watu waume wote waendao vitani walikufa katika bara njiani, baada ya wao kutoka Misri.
Deutéronome 2.16 Nombres 26.64-26.65 1 Corinthiens 10.5 Nombres 14.22 Deutéronome 2.14
5 Kwa kuwa watu wote waliotoka walikuwa wamekwisha kutahiriwa; lakini watu wote waliozaliwa katika bara njiani walipokwisha kutoka Misri, hao hawakutahiriwa.
Romains 2.26 1 Corinthiens 7.19 Matthieu 12.7 Deutéronome 12.8-12.9 Osée 6.6-6.7
6 Kwa kuwa wana wa Israeli walitembea muda wa miaka arobaini barani, hata hilo taifa zima, yaani, watu waume waendao vitani, waliotoka Misri, walipokuwa wameangamia; kwa sababu hawakuisikiza sauti ya Bwana; nao ndio Bwana aliowaapia ya kwamba hatawaacha waione hiyo nchi, ambayo Bwana aliwaapia baba zao kwamba atatupa sisi; nchi ijaayo maziwa na asali.
Deutéronome 2.7 Deutéronome 2.14 Exode 3.8 Nombres 14.23 Deutéronome 8.4
7 Na watoto wao, aliowainua badala yao ndio hao aliowatahiri Yoshua; kwa kuwa wao walikuwa hawakutahiriwa, kwa maana walikuwa hawakuwatahiri njiani.
Deutéronome 1.39 Nombres 14.31
8 Ilikuwa walipokwisha kutahiriwa taifa zima, wakakaa kila mtu mahali pake maragoni, hata walipopoa.
Genèse 34.25
9 Bwana akamwambia Yoshua, Siku hii ya leo nimeivingirisha hiyo aibu ya Misri iondoke juu yenu. Kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Gilgali, hata hivi leo.
Josué 4.19 Genèse 34.14 1 Samuel 17.36 Josué 24.14 Ephésiens 2.11-2.12
10 Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare za Yeriko.
Ezéchiel 12.3 Ezéchiel 12.6-12.16 Exode 12.6 Nombres 9.1-9.5
11 Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandama hiyo sikukuu ya pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi, siku iyo hiyo.
Lévitique 23.14 Lévitique 23.6 Exode 13.6-13.7 Exode 12.18-12.20
12 Ndipo ile mana ikakoma siku ya pili yake, baada ya wao kuyala hayo mazao ya nchi; na hao wana wa Israeli hawakuwa na mana tena; lakini wakala katika viliwa vya nchi ya Kanaani mwaka huo.
Exode 16.35 Proverbes 13.22 Néhémie 9.20-9.21 Deutéronome 6.10-6.11 Jean 4.38

Prise de Jéricho

13 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu?
Genèse 18.2 Nombres 22.23 1 Chroniques 21.30 Daniel 10.5 Actes 1.10
14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la Bwana. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake?
Genèse 17.3 Esaïe 55.4 Luc 20.42 Matthieu 22.44 Daniel 10.13
15 Huyo amiri wa jeshi la Bwana akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo.
Exode 3.5 Actes 7.32-7.33 2 Pierre 1.18

Cette Bible est dans le domaine public.