Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 2.15
Bible en Swahili de l’est


Exploration à Jéricho

1 Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko.
Jacques 2.25 Hébreux 11.31 Nombres 25.1 Matthieu 1.5 Juges 18.17
2 Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi.
Psaumes 127.1 Daniel 4.35 Proverbes 21.30 Esaïe 43.13
3 Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi.
Lévitique 24.14 Genèse 42.31 2 Samuel 10.3 Job 21.30 Genèse 42.9-42.12
4 Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka;
2 Samuel 17.19-17.20 2 Rois 6.19 2 Samuel 16.18-16.19 Exode 1.19
5 ikawa kama wakati wa kufungwa lango la mji, kulipokuwa giza, watu wale wakatoka, wala sijui walikokwenda; wafuateni upesi, maana mtawapata.
Néhémie 13.19 Ezéchiel 47.1-47.2 Ezéchiel 47.12 Jérémie 50.20 Romains 3.7-3.8
6 Lakini yeye alikuwa amewapandisha darini, akawaficha kwa mabua ya kitani, aliyokuwa ameyatandika juu ya dari.
2 Samuel 17.19 Deutéronome 22.8 Exode 2.2 1 Rois 18.13 Exode 1.15-1.21
7 Basi hao watu wakawafuata kwa njia iendayo Yordani mpaka vivukoni; na mara wale watu waliowafuatia walipokwisha kutoka, wakalifunga lango.
Juges 3.28 Juges 12.5 Josué 2.5 Actes 5.23
8 Tena kabla hawajalala akawaendea juu darini,
9 akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu.
Exode 23.27 Deutéronome 2.25 Genèse 35.5 Josué 2.11 Exode 15.15-15.16
10 Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng’ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa.
Nombres 21.21-21.35 Deutéronome 2.30-3.8 Exode 14.21-14.31 Nombres 23.22 Josué 4.24
11 Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.
Josué 7.5 Esaïe 13.7 Deutéronome 4.39 Josué 5.1 Psaumes 22.14
12 Basi sasa, nawasihi, niapieni kwa Bwana, kwa kuwa nimewatendea ihisani, ya kwamba ninyi nanyi mtaitendea ihisani nyumba ya baba yangu; tena nipeni alama ya uaminifu;
Josué 2.18 Esther 8.6 Genèse 24.9 1 Samuel 20.14-20.17 Ezéchiel 9.4-9.6
13 ya kwamba mtawaponya hai baba yangu na mama yangu, na ndugu zangu wanaume na wanawake, na vitu vyote walivyo navyo, na kutuokoa roho zetu na kufa.
14 Wale wanaume wakamwambia, Uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa ihisani na uaminifu.
Matthieu 5.7 Juges 1.24-1.25 Genèse 24.49 Josué 6.17 Nombres 10.29-10.32
15 Ndipo akawashusha kwa kamba dirishani, maana nyumba yake ilikuwa katika ukuta wa mji; naye alikaa ukutani.
Actes 9.25 2 Corinthiens 11.33 1 Samuel 19.12-19.17 Josué 6.20
16 Akawaambia, Enendeni zenu mlimani, wale wanaowafuatia wasije wakawapata; mkajifiche huko siku tatu hata wao wanaowafuatia watakaporudi; kisha enendeni zenu.
1 Samuel 23.14 Josué 2.22 1 Samuel 23.29 Psaumes 11.1 Jacques 2.25
17 Wale wanaume wakamwambia, Sisi tunataka tusiwe na hatia kwa ajili ya kiapo hiki ulichotuapisha.
Genèse 24.3-24.8 Lévitique 19.11-19.12 Josué 2.20 2 Samuel 21.1-21.2 Exode 20.7
18 Angalia, tutakapoingia katika nchi hii, funga kamba hii nyekundu katika dirisha hili ulilotutelemshia; nawe uwakusanye kwako nyumbani mwako, baba yako, na mama yako, na ndugu zako, na watu wote wa nyumba ya baba yako.
Josué 6.23 Genèse 7.1 Josué 2.21 Genèse 19.12-19.17 Josué 2.12-2.13
19 Itakuwa mtu awaye yote atakayetoka katika mlango wa nyumba yako kwenda njiani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, na sisi tutakuwa hatuna hatia; na mtu atakayekuwa ndani ya nyumba yako damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu, mkono wa mtu ukimpata.
Matthieu 27.24-27.25 Hébreux 10.29 Exode 12.13 Lévitique 20.9 Actes 27.31
20 Lakini wewe ukitangaza habari yetu hii, ndipo tutakuwa hatuna hatia, katika kiapo hiki ulichotuapisha.
Proverbes 11.13
21 Naye akasema, Na iwe hivyo kama yalivyo maneno yenu. Akawatoa, nao wakaenda zao; naye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani
Josué 2.18 Matthieu 7.24 Jean 2.5
22 Watu hao wakaenda, wakafika mlimani, wakakaa huko siku tatu, hata wale waliowafuatia walipokuwa wamerudi; na wale waliowafuatia wakawafuatia katika njia ile yote, lakini hawakuwaona.
2 Samuel 17.20 Psaumes 32.6-32.7 1 Samuel 19.10-19.12
23 Kisha wale watu wakarudi, wakatelemka mlimani, wakavuka, wakamwendea Yoshua, mwana wa Nuni, nao wakamwambia habari za mambo yote yaliyowapata.
24 Wakamwambia Yoshua, Hakika Bwana ameitia nchi yote katika mikono yetu; tena zaidi ya hayo wenyeji wa nchi wanayeyuka mbele yetu.
Exode 23.31 Nombres 13.32-13.33 Josué 2.9-2.11 Apocalypse 6.16-6.17 Proverbes 25.13

Cette Bible est dans le domaine public.