Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 16.6
Bible en Swahili de l’est


Territoire accordé à Éphraïm

1 Kura ya wana wa Yusufu ilianza kutoka mto wa Yordani hapo Yeriko, hapo penye maji ya Yeriko upande wa mashariki, maana, ni hiyo nyika, kukwea kutoka Yeriko kati ya hiyo nchi ya vilima mpaka Betheli;
Josué 18.12 Josué 8.15 Josué 15.61 2 Rois 2.19-2.21
2 kisha ikatoka huko Betheli kwendelea Luzu, kisha ikaendelea hata kuufikilia mpaka wa Waarki mpaka Atarothi;
Josué 18.13 Genèse 28.19 Juges 1.22-1.26 2 Samuel 16.16 1 Chroniques 27.33
3 kisha ikatelemkia upande wa magharibi hata kuufikilia mpaka wa Wayafleti, hata mpaka wa Beth-horoni ya chini, hata kufikilia Gezeri; na matokeo yake yalikuwa hapo baharini.
Josué 10.33 Josué 18.13 2 Chroniques 8.5 1 Chroniques 7.28 1 Rois 9.15-9.17
4 Na wana wa Yusufu, Manase na Efraimu, walitwaa urithi wao.
Josué 17.14
5 Na mpaka wa wana wa Efraimu kwa kuandama jamaa zao ulikuwa hivi; mpaka na urithi wao upande wa mashariki ulikuwa ni Ataroth-adari, hata Beth-horoni wa juu;
Josué 18.13 Josué 16.2
6 kisha mpaka ukatokea kwendelea upande wa magharibi huko Mikmeta upande wa kaskazini; kisha mpaka ukazunguka kwendea upande wa mashariki hata Taanath-shilo, kisha ukaendelea upande wa mashariki wa Yanoa;
Josué 17.7 Josué 18.1
7 kisha ulitelemka kutoka Yanoa hata Atarothi, na Naara, kisha ukafikilia Yeriko, na kutokea hapo penye mto wa Yordani.
1 Chroniques 7.28 Josué 3.16 Josué 6.1 Nombres 33.48 Josué 6.26
8 Kutoka hapo Tapua mpaka ukaendelea upande wa magharibi hata kijito cha Kana; na matokeo yake yalikuwa baharini. Huo ndio urithi wa hao wana wa Efraimu kwa kuandama jamaa zao;
Josué 17.8-17.9 Nombres 34.6 Josué 19.28 Josué 12.17 Josué 16.3-16.6
9 pamoja na ile miji iliyotengwa kwa ajili ya wana wa Efraimu katikati ya urithi wa hao wana wa Manase, miji yote pamoja na vijiji vyake.
Josué 17.9
10 Nao hawakuwatoa Wakanaani waliokuwa Wakikaa Gezeri; lakini hao Wakanaani waliketi kati ya Efraimu, hata hivi leo, wakawa watumishi wa kufanya kazi za shokoa.
Juges 1.29 1 Rois 9.16 Josué 17.13 Deutéronome 7.1-7.2 Nombres 33.52-33.55

Cette Bible est dans le domaine public.