Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 2.21
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nalipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito pamoja nami.
Galates 2.13 Galates 2.3 Tite 1.4 Actes 4.36-4.37 2 Corinthiens 8.23
2 Nami nalikwenda kwa kuwa nalifunuliwa, nikawaeleza injili ile niihubiriyo katika Mataifa, lakini kwa faragha kwa hao walio wenye sifa, isiwe labda napiga mbio bure, au nalipiga mbio bure.
Philippiens 2.16 Galates 2.9 Actes 15.12 1 Corinthiens 2.2 Actes 15.4
3 Lakini Tito aliyekuwa pamoja nami, naye ni Myunani, hakulazimishwa kutahiriwa.
Actes 16.3 Galates 5.2-5.6 1 Corinthiens 9.20-9.21 2 Corinthiens 2.13 Actes 15.24
4 Bali kwa ajili ya ndugu za uongo walioingizwa kwa siri; ambao waliingia kwa siri ili kuupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, ili watutie utumwani;
2 Corinthiens 11.26 Jude 1.4 Galates 5.1 Actes 15.1 Actes 15.24
5 ambao hata saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae pamoja nanyi.
Galates 2.14 Colossiens 1.5 Galates 4.16 Galates 3.1-3.2 Colossiens 2.4-2.8
6 Lakini wale wenye sifa ya kuwa wana cheo; (walivyokuwa vyo vyote ni mamoja kwangu; Mungu hapokei uso wa mwanadamu); nasema, hao wenye sifa hawakuniongezea kitu;
2 Corinthiens 12.11 Actes 10.34 Galates 6.3 2 Corinthiens 11.5 Galates 2.2
7 bali, kinyume cha hayo, walipoona ya kuwa nimekabidhiwa injili ya wasiotahiriwa, kama vile Petro ya waliotahiriwa;
1 Thessaloniciens 2.4 Galates 1.16 Galates 2.9 Actes 9.15 1 Timothée 1.11
8 (maana yeye aliyemwezesha Petro kuwa mtume wa waliotahiriwa ndiye aliyeniwezesha mimi kwenda kwa Mataifa);
Actes 13.2-13.11 1 Corinthiens 1.5-1.7 Actes 19.26 Actes 21.19 Actes 26.17-26.18
9 tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;
Romains 12.3 Apocalypse 3.12 Galates 2.2 Romains 1.5 1 Pierre 4.10-4.11
10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.
Actes 24.17 Hébreux 13.16 1 Jean 3.17 Jacques 2.15-2.16 Actes 11.29-11.30
11 Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu.
Actes 15.1 1 Timothée 5.20 Exode 32.21-32.22 Nombres 20.12 2 Corinthiens 12.11
12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.
Actes 10.28 Luc 15.2 Actes 11.2-11.3 Galates 2.9 Ephésiens 3.6
13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.
1 Corinthiens 5.6 Ephésiens 4.14 1 Corinthiens 15.33 Actes 4.36 Galates 2.1
14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?
Actes 10.28 Galates 2.5 Psaumes 84.11 1 Timothée 5.20 Proverbes 2.7
15 Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wakosaji wa Mataifa,
Ephésiens 2.3 Tite 3.3 Romains 3.9 Philippiens 3.4 Ephésiens 2.11-2.12
16 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
Philippiens 3.9 Psaumes 143.2 Romains 3.19-3.28 Romains 9.30 Galates 4.5
17 Lakini ikiwa sisi wenyewe, kwa kutafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, tulionekana kuwa wenye dhambi, je! Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? Hasha!
Romains 6.1-6.2 Galates 2.15 Romains 3.6 1 Jean 3.5 Romains 3.4
18 Maana nikiyajenga tena yale niliyoyabomoa, naonyesha ya kuwa mimi mwenyewe ni mkosaji.
Galates 4.9-4.12 Galates 2.4-2.5 Galates 2.12-2.16 Galates 5.11 Romains 14.15
19 Maana mimi kwa njia ya sheria naliifia sheria ili nimwishie Mungu.
Romains 6.11 Romains 7.4 Romains 6.2 2 Corinthiens 5.15 Hébreux 9.14
20 Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.
Romains 6.4-6.6 Galates 5.24 2 Corinthiens 4.10-4.11 2 Corinthiens 5.15 Colossiens 3.3-3.4
21 Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure.
Galates 3.21 Galates 5.2-5.4 1 Corinthiens 15.14 Galates 2.16 Hébreux 7.11

Cette Bible est dans le domaine public.