1 Sina budi kujisifu, ijapokuwa haipendezi; lakini nitafikilia maono na mafunuo ya Bwana.
Galates 2.2  Galates 1.12  2 Corinthiens 12.7  1 Corinthiens 10.23  Actes 18.9  
 2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.
2 Corinthiens 11.11  Apocalypse 12.5  Actes 22.17  1 Thessaloniciens 4.17  Romains 16.7  
 3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua); 
4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.
Luc 23.43  Apocalypse 2.7  Ezéchiel 31.9  
 5 Kwa habari za mtu kama huyo nitajisifu; lakini kwa ajili ya nafsi yangu sitajisifu, isipokuwa katika habari ya udhaifu wangu.
1 Corinthiens 2.3  2 Corinthiens 12.9-12.10  2 Corinthiens 11.30  
 6 Maana kama ningetaka kujisifu singekuwa mpumbavu, kwa sababu nitasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu asinihesabie zaidi ya hayo ayaonayo kwangu au kuyasikia kwangu.
2 Corinthiens 11.16  2 Corinthiens 12.11  Job 24.25  1 Corinthiens 3.9-3.10  2 Corinthiens 5.13  
 7 Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.
1 Corinthiens 5.5  Daniel 5.20  Juges 2.3  2 Chroniques 26.16  Nombres 33.55  
 8 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.
2 Samuel 12.16-12.18  Hébreux 5.7  1 Samuel 15.11  Psaumes 77.2-77.11  Matthieu 20.21-20.22  
 9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
2 Corinthiens 12.10  Philippiens 4.13  Ephésiens 3.16  Esaïe 40.29-40.31  1 Corinthiens 10.13  
 10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.
2 Corinthiens 13.4  Romains 5.3  Jacques 1.2  2 Corinthiens 6.4  2 Corinthiens 12.9  
 11 Nimekuwa mpumbavu, ninyi mmenilazimisha. Maana ilinipasa nisifiwe na ninyi; kwa sababu sikuwa duni ya mitume walio wakuu kwa lo lote, nijapokuwa si kitu.
2 Corinthiens 11.5  2 Corinthiens 11.1  2 Corinthiens 11.16-11.17  1 Corinthiens 3.4-3.7  2 Corinthiens 12.6  
 12 Kweli ishara za mtume zilitendwa katikati yenu katika saburi yote, kwa ishara na maajabu na miujiza.
Romains 15.18-15.19  2 Corinthiens 6.4-6.10  1 Corinthiens 1.5-1.7  1 Corinthiens 14.18  2 Corinthiens 11.4  
 13 Maana ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila kwa kuwa mimi sikuwalemea? Mnisamehe udhalimu huu.
1 Corinthiens 9.12  2 Corinthiens 12.14  1 Corinthiens 9.6  2 Corinthiens 11.7-11.9  1 Corinthiens 9.15-9.18  
 14 Tazama, hii ni mara ya tatu ya mimi kuwa tayari kuja kwenu, wala sitawalemea. Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi; maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto.
Proverbes 19.14  2 Corinthiens 1.15  1 Corinthiens 4.14-4.15  1 Corinthiens 10.33  Proverbes 13.22  
 15 Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya roho zenu. Je! Kadiri nizidivyo kuwapenda sana, ninapungukiwa kupendwa?
1 Thessaloniciens 2.8  Philippiens 2.17  Colossiens 1.24  2 Corinthiens 1.6  2 Corinthiens 2.3  
 16 Lakini na iwe hivyo, mimi sikuwalemea; bali kwa kuwa mwerevu naliwapata kwa hila.
1 Thessaloniciens 2.5  1 Thessaloniciens 2.3  2 Corinthiens 1.12  2 Corinthiens 7.2  2 Corinthiens 12.13  
 17 Je! Mtu ye yote niliyemtuma kwenu, kwa mtu huyo naliwatoza kitu?
1 Corinthiens 16.10  1 Corinthiens 4.17  2 Rois 5.16  2 Corinthiens 12.18  2 Corinthiens 9.5  
 18 Nalimwonya Tito, nikamtuma ndugu yule pamoja naye. Je! Tito aliwatoza kitu? Je! Hatukuenenda kwa Roho yeye yule na katika nyayo zile zile?2 Corinthiens 8.6  Romains 4.12  1 Samuel 12.3-12.4  1 Pierre 2.21  2 Corinthiens 7.6  
 19 Mwadhani hata sasa ya kuwa najidhuru kwenu! Mbele za Mungu twanena katika Kristo. Na hayo yote, wapenzi, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
Romains 9.1  2 Corinthiens 10.8  1 Corinthiens 14.26  2 Corinthiens 3.1  Romains 12.19  
 20 Maana nachelea, nisije nikawakuta si kama vile nitakavyo kuwakuta, nikaonekana kwenu si kama vile mtakavyo; nisije nikakuta labda fitina na wivu, na ghadhabu, na ugomvi, na masingizio, na manong’onezo, na majivuno, na ghasia;
1 Corinthiens 1.11  Romains 1.29  Galates 5.15  1 Pierre 2.1  1 Corinthiens 3.3-3.4  
 21 nami nitakapokuja tena, Mungu wangu asije akanidhili kwenu, nami nikawasikitikia wengi waliokosa tangu hapo, wasiutubie uchafu, na uasherati, na ufisadi walioufanya.
2 Corinthiens 13.2  Colossiens 3.5  Galates 5.19  1 Corinthiens 5.1  2 Pierre 2.10-2.14