Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 12.11
Bible en Swahili de l’est


Une nécessaire humilité

1 Sina budi kujisifu, ijapokuwa haipendezi; lakini nitafikilia maono na mafunuo ya Bwana.
Galates 2.2 Galates 1.12 2 Corinthiens 12.7 Daniel 10.5-10.10 Actes 23.11
2 Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.
2 Corinthiens 11.11 1 Thessaloniciens 4.17 Apocalypse 12.5 Actes 22.17 Romains 16.7
3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua);
4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene.
Luc 23.43 Apocalypse 2.7 Ezéchiel 31.9
5 Kwa habari za mtu kama huyo nitajisifu; lakini kwa ajili ya nafsi yangu sitajisifu, isipokuwa katika habari ya udhaifu wangu.
1 Corinthiens 2.3 2 Corinthiens 12.9-12.10 2 Corinthiens 11.30
6 Maana kama ningetaka kujisifu singekuwa mpumbavu, kwa sababu nitasema kweli. Lakini najizuia, ili mtu asinihesabie zaidi ya hayo ayaonayo kwangu au kuyasikia kwangu.
2 Corinthiens 11.16 2 Corinthiens 12.7 2 Corinthiens 12.11 Job 24.25 1 Corinthiens 3.9-3.10
7 Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.
1 Corinthiens 5.5 Daniel 5.20 Juges 2.3 2 Chroniques 26.16 Nombres 33.55
8 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.
2 Samuel 12.16-12.18 Hébreux 5.7 1 Samuel 15.11 Psaumes 77.2-77.11 Matthieu 20.21-20.22
9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.
2 Corinthiens 12.10 Philippiens 4.13 Ephésiens 3.16 Esaïe 40.29-40.31 1 Corinthiens 10.13
10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.
2 Corinthiens 13.4 Romains 5.3 2 Corinthiens 12.9 Jacques 1.2 2 Corinthiens 6.4
11 Nimekuwa mpumbavu, ninyi mmenilazimisha. Maana ilinipasa nisifiwe na ninyi; kwa sababu sikuwa duni ya mitume walio wakuu kwa lo lote, nijapokuwa si kitu.
2 Corinthiens 11.5 2 Corinthiens 11.1 Ephésiens 3.8 2 Corinthiens 12.12 2 Corinthiens 11.16-11.17
12 Kweli ishara za mtume zilitendwa katikati yenu katika saburi yote, kwa ishara na maajabu na miujiza.
Romains 15.18-15.19 2 Corinthiens 6.4-6.10 1 Corinthiens 1.5-1.7 1 Corinthiens 14.18 2 Corinthiens 11.4
13 Maana ni kitu gani mlichopungukiwa kuliko makanisa mengine, ila kwa kuwa mimi sikuwalemea? Mnisamehe udhalimu huu.
1 Corinthiens 9.12 2 Corinthiens 12.14 1 Corinthiens 9.6 2 Corinthiens 11.7-11.9 1 Corinthiens 9.15-9.18
14 Tazama, hii ni mara ya tatu ya mimi kuwa tayari kuja kwenu, wala sitawalemea. Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi; maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto.
Proverbes 19.14 2 Corinthiens 1.15 1 Corinthiens 4.14-4.15 1 Corinthiens 10.33 Proverbes 13.22
15 Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya roho zenu. Je! Kadiri nizidivyo kuwapenda sana, ninapungukiwa kupendwa?
1 Thessaloniciens 2.8 Philippiens 2.17 Colossiens 1.24 2 Corinthiens 1.6 2 Corinthiens 2.3
16 Lakini na iwe hivyo, mimi sikuwalemea; bali kwa kuwa mwerevu naliwapata kwa hila.
1 Thessaloniciens 2.5 1 Thessaloniciens 2.3 2 Corinthiens 1.12 2 Corinthiens 7.2 2 Corinthiens 12.13
17 Je! Mtu ye yote niliyemtuma kwenu, kwa mtu huyo naliwatoza kitu?
1 Corinthiens 16.10 1 Corinthiens 4.17 2 Rois 5.16 2 Corinthiens 12.18 2 Corinthiens 9.5
18 Nalimwonya Tito, nikamtuma ndugu yule pamoja naye. Je! Tito aliwatoza kitu? Je! Hatukuenenda kwa Roho yeye yule na katika nyayo zile zile?
2 Corinthiens 8.6 Romains 4.12 2 Corinthiens 7.2 Nombres 16.15 1 Samuel 12.3-12.4
19 Mwadhani hata sasa ya kuwa najidhuru kwenu! Mbele za Mungu twanena katika Kristo. Na hayo yote, wapenzi, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
Romains 9.1 2 Corinthiens 10.8 1 Corinthiens 14.26 1 Corinthiens 10.33 Philippiens 4.1
20 Maana nachelea, nisije nikawakuta si kama vile nitakavyo kuwakuta, nikaonekana kwenu si kama vile mtakavyo; nisije nikakuta labda fitina na wivu, na ghadhabu, na ugomvi, na masingizio, na manong’onezo, na majivuno, na ghasia;
1 Corinthiens 1.11 Romains 1.29 Galates 5.15 1 Pierre 2.1 2 Corinthiens 10.6
21 nami nitakapokuja tena, Mungu wangu asije akanidhili kwenu, nami nikawasikitikia wengi waliokosa tangu hapo, wasiutubie uchafu, na uasherati, na ufisadi walioufanya.
2 Corinthiens 13.2 Colossiens 3.5 Galates 5.19 1 Corinthiens 5.1 Esdras 10.1

Cette Bible est dans le domaine public.