Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 16.16
Bible en Swahili de l’est


Sur la collecte organisée

1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo.
Actes 24.17 Galates 2.10 2 Corinthiens 8.1-8.9 1 Jean 3.17 Romains 15.25-15.26
2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;
Actes 20.7 2 Corinthiens 9.3-9.5 Apocalypse 1.10 Luc 24.1 2 Chroniques 31.10
3 nami nitakapofika nitawatuma kwa nyaraka wale mtakaowachagua, wachukue hisani yenu mpaka Yerusalemu.
2 Corinthiens 8.18-8.24 1 Corinthiens 11.34 1 Corinthiens 4.19-4.21 2 Corinthiens 8.4 Actes 6.1-6.6
4 Na kama ikifaa niende na mimi, watasafiri pamoja nami.
2 Corinthiens 8.4 2 Corinthiens 8.19 Romains 15.25

Projets de Paul et salutations

5 Lakini nitakuja kwenu, nikiisha kupita kati ya Makedonia; maana napita kati ya Makedonia.
Actes 19.21 1 Corinthiens 4.19 Actes 20.1-20.3 2 Corinthiens 1.15-1.17
6 Labda nitakaa kwenu; naam, labda wakati wote wa baridi, mpate kunisafirisha ko kote nitakakokwenda.
Actes 15.3 Romains 15.24 Actes 20.38 Actes 17.15 Actes 27.12
7 Maana sipendi kuonana nanyi sasa, katika kupita tu, kwa sababu nataraji kukaa kwenu muda kidogo, Bwana akinijalia.
Actes 18.21 1 Corinthiens 4.19 Proverbes 19.21 Romains 1.10 Jacques 4.15
8 Lakini nitakaa Efeso hata Pentekoste;
Actes 2.1 1 Corinthiens 15.32 Lévitique 23.15-23.21 Actes 18.19 Exode 23.16
9 kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao.
Actes 14.27 2 Corinthiens 2.12 Colossiens 4.3 Philippiens 3.18 Apocalypse 3.7-3.8
10 Lakini, Timotheo akija, angalieni akae kwenu pasipo hofu; maana anaifanya kazi ya Bwana vile vile kama mimi mwenyewe;
1 Corinthiens 15.58 1 Corinthiens 4.17 1 Thessaloniciens 3.2 Romains 16.21 Actes 16.1
11 basi mtu ye yote asimdharau, lakini msafirisheni kwa amani, ili aje kwangu; maana ninamtazamia pamoja na ndugu zetu.
Actes 15.33 1 Timothée 4.12 1 Corinthiens 16.6 Tite 2.15 1 Corinthiens 16.10
12 Lakini kwa habari za Apolo, ndugu yetu, nalimsihi sana aende kwenu pamoja na hao ndugu; ambaye si mapenzi yake kwenda sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi.
1 Corinthiens 1.12 1 Corinthiens 3.5 Ecclésiaste 3.1 Marc 6.21 Tite 3.4
13 Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari.
Josué 1.9 Ephésiens 6.10 Ephésiens 6.13-6.18 Galates 5.1 2 Thessaloniciens 2.15
14 Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.
Galates 5.13-5.14 Jean 13.34-13.35 Jean 15.17 1 Corinthiens 12.31-14.1 1 Corinthiens 8.1
15 Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu);
1 Corinthiens 1.16 Romains 16.5 1 Pierre 4.10 Romains 16.2 2 Corinthiens 9.1
16 watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha.
1 Thessaloniciens 5.12 Hébreux 13.17 1 Corinthiens 12.28 Ephésiens 5.21 Romains 16.6
17 Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu.
2 Corinthiens 11.9 Philippiens 2.30 Philémon 1.13
18 Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao.
2 Corinthiens 7.13 Philémon 1.7 1 Thessaloniciens 5.12 Romains 15.32 1 Thessaloniciens 3.6-3.7
19 Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao.
Actes 18.2 2 Timothée 4.19 Romains 16.3-16.5 Romains 16.15 Colossiens 4.15
20 Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
Romains 16.16 2 Corinthiens 13.12-13.13 Romains 16.21 1 Pierre 5.14 1 Thessaloniciens 5.26
21 Hii ni salamu yangu Paulo kwa mkono wangu mwenyewe.
Colossiens 4.18 Galates 6.11 2 Thessaloniciens 3.17 Philémon 1.19 Romains 16.22
22 Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha.
Romains 9.3 1 Jean 4.19 Apocalypse 22.20 Jean 14.21 Ephésiens 6.24
23 Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi.
Romains 16.20 Romains 16.23
24 Pendo langu na liwe pamoja nanyi nyote katika Kristo Yesu.
Apocalypse 3.19 2 Corinthiens 11.11 2 Corinthiens 12.15 Matthieu 28.20 1 Corinthiens 4.14-4.15

Cette Bible est dans le domaine public.