Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 15.6
Bible en Swahili de l’est


Le cœur humain

1 Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,
Matthieu 23.2 Marc 7.1-7.23 Marc 3.22 Luc 5.17 Matthieu 23.15-23.28
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.
Luc 11.38 Colossiens 2.8 Colossiens 2.20-2.23 1 Pierre 1.18 Marc 7.2
3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
Tite 1.14 Colossiens 2.23 Matthieu 7.3-7.5 Marc 7.6-7.8 Colossiens 2.8
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
Exode 20.12 Exode 21.17 Deutéronome 5.16 Lévitique 20.9 Matthieu 19.19
5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,
Proverbes 20.25 Lévitique 27.9-27.34 Actes 4.19 Amos 7.15-7.17 Marc 7.10-7.13
6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.
1 Timothée 5.8 Psaumes 119.126 Jérémie 8.8 1 Timothée 5.16 Osée 4.6
7 Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,
Marc 7.6 Actes 28.25-28.27 Matthieu 23.23-23.29 Matthieu 7.5
8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.
Esaïe 29.13 Actes 8.21 Ezéchiel 33.31 Jérémie 12.2 Jean 1.47
9 Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.
Esaïe 29.13 Tite 1.14 Colossiens 2.18-2.22 Marc 7.7 Hébreux 13.9
10 Akawaita makutano akawaambia
Marc 7.14-7.15 Ephésiens 1.17 1 Rois 22.28 Esaïe 6.9 Luc 24.45
11 Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi.
Actes 10.14-10.15 Marc 7.15 Romains 14.14 Psaumes 52.2-52.4 Psaumes 12.2
12 Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa?
1 Rois 22.13-22.14 2 Corinthiens 6.3 Jacques 3.17 Galates 2.5 Matthieu 17.27
13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa.
Jean 15.2 Esaïe 60.21 Esaïe 61.3 Matthieu 13.40-13.41 Psaumes 92.13
14 Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.
Luc 6.39 Osée 4.17 Malachie 2.8 Esaïe 56.10 Matthieu 23.16-23.24
15 Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo.
Matthieu 13.36 Marc 7.17 Jean 16.29 Marc 4.34
16 Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?
Matthieu 16.9 Marc 7.18 Matthieu 15.10 Marc 9.32 Matthieu 16.11
17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
1 Corinthiens 6.13 Matthieu 7.19-7.20 2 Rois 10.27 Luc 6.45 Jacques 3.6
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
Matthieu 12.34 Proverbes 15.28 Jacques 3.6-3.10 Proverbes 15.2 Matthieu 15.11
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
Galates 5.19-5.21 Jacques 1.13-1.15 Actes 8.22 Jérémie 17.9 Psaumes 119.113
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi.
Apocalypse 21.27 1 Corinthiens 6.18-6.20 Matthieu 23.25-23.26 Matthieu 15.2 Luc 11.38-11.40

Jésus et la femme non juive

21 Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.
Josué 13.6 Matthieu 11.21-11.23 Josué 19.28-19.29 Juges 1.31 Matthieu 10.5-10.6
22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
Matthieu 9.27 Matthieu 17.15 Psaumes 45.12 Luc 18.38-18.39 Matthieu 22.42-22.45
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
Matthieu 14.15 Genèse 42.7 Psaumes 28.1 Deutéronome 8.2 Marc 10.47-10.48
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Matthieu 10.5-10.6 Romains 15.8 Actes 3.25-3.26 Ezéchiel 34.5-34.6 Matthieu 9.36
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
Matthieu 8.2 Matthieu 14.33 Marc 9.22 Luc 11.8-11.10 Marc 9.24
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
Philippiens 3.2 Apocalypse 22.15 Ephésiens 2.12 Matthieu 7.6 Romains 9.4
27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
Job 40.4-40.5 Ephésiens 3.8 Matthieu 8.8 1 Timothée 1.13-1.15 Luc 18.13
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.
Matthieu 8.10 Marc 5.34 Matthieu 8.13 Matthieu 9.22 Luc 7.50
29 Yesu akaondoka huko, akafika kando ya bahari ya Galilaya; akapanda mlimani, akaketi huko.
Matthieu 4.18 Matthieu 5.1 Jean 6.1 Marc 1.16 Marc 7.31-7.37
30 Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya;
Psaumes 103.3 Luc 6.17-6.19 Matthieu 4.23-4.24 Matthieu 11.4-11.5 Actes 2.22
31 hata ule mkutano wakastaajabu, walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, na vipofu wanaona; wakamtukuza Mungu wa Israeli.
Matthieu 9.8 Marc 9.43 Matthieu 9.33 Matthieu 18.8 Genèse 33.20

Multiplication des pains pour quatre mille hommes

32 Yesu akawaita wanafunzi wake, akasema, Nawahurumia mkutano, kwa kuwa yapata siku tatu wamekaa pamoja nami, wala hawana kitu cha kula, tena kuwaaga wakifunga sipendi, wasije wakazimia njiani.
Matthieu 9.36 Marc 8.1-8.10 Luc 12.29-12.30 Matthieu 6.32-6.33 Actes 27.33
33 Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?
Jean 6.5-6.9 Matthieu 14.15 Marc 6.37 Marc 8.4-8.5 Luc 9.13
34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.
Jean 21.9-21.10 Matthieu 16.9-16.10 Luc 24.41-24.42
35 Akawaagiza mkutano waketi chini;
Matthieu 14.19-14.21 Marc 6.39-6.40 Jean 6.10 Luc 9.14-9.16
36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akashukuru akavimega, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.
Luc 22.19 Romains 14.6 Jean 6.11 Actes 27.35 1 Timothée 4.3-4.4
37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.
Marc 8.19-8.21 Marc 8.8-8.9 Matthieu 16.9-16.10 Matthieu 14.20-14.21 Matthieu 15.33
38 Nao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila wanawake na watoto.
39 Akawaaga makutano, akapanda chomboni, akaenda pande za Magadani.
Marc 8.10 Matthieu 14.22

Cette Bible est dans le domaine public.