Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 15.4
Bible en Swahili de l’est


Le cœur humain

1 Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema,
Matthieu 23.15-23.28 Matthieu 5.20 Luc 5.21 Actes 23.9 Luc 5.30
2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula.
Luc 11.38 Colossiens 2.8 Marc 7.2 Marc 7.5 Colossiens 2.20-2.23
3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
Colossiens 2.23 Matthieu 7.3-7.5 Marc 7.6-7.8 Colossiens 2.8 Marc 7.13
4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe.
Exode 20.12 Exode 21.17 Deutéronome 5.16 Lévitique 20.9 Proverbes 23.22
5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu,
Actes 4.19 Amos 7.15-7.17 Marc 7.10-7.13 Matthieu 23.16-23.18 Actes 5.29
6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.
Psaumes 119.126 1 Timothée 5.8 1 Timothée 5.3-5.4 Marc 7.13 Psaumes 119.139
7 Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema,
Marc 7.6 Actes 28.25-28.27 Matthieu 23.23-23.29 Matthieu 7.5
8 Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami.
Esaïe 29.13 Actes 8.21 Ezéchiel 33.31 Jérémie 12.2 Proverbes 23.26
9 Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu.
Tite 1.14 Esaïe 29.13 Marc 7.7 Hébreux 13.9 1 Timothée 1.4
10 Akawaita makutano akawaambia
Marc 7.14-7.15 Luc 20.45-20.47 Esaïe 55.3 Matthieu 24.15 Colossiens 1.9
11 Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi.
Actes 10.14-10.15 Romains 14.14 Marc 7.15 Matthieu 15.18-15.20 Psaumes 58.3-58.4
12 Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa?
2 Corinthiens 6.3 Jacques 3.17 Galates 2.5 Matthieu 17.27 1 Corinthiens 10.32-10.33
13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang’olewa.
Jean 15.2 Esaïe 60.21 Esaïe 61.3 Matthieu 13.40-13.41 1 Corinthiens 3.9
14 Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.
Luc 6.39 Osée 4.17 Malachie 2.8 Esaïe 56.10 Apocalypse 22.15
15 Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo.
Matthieu 13.36 Marc 7.17 Jean 16.29 Marc 4.34
16 Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili?
Matthieu 16.9 Marc 9.32 Marc 7.18 Matthieu 15.10 Luc 9.45
17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni?
1 Corinthiens 6.13 2 Rois 10.27 Luc 6.45 Jacques 3.6 Colossiens 2.21-2.22
18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
Matthieu 12.34 Proverbes 15.28 Jacques 3.6-3.10 Proverbes 15.2 Matthieu 15.11
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
Galates 5.19-5.21 Jacques 1.13-1.15 Romains 3.10-3.19 Tite 3.2-3.6 Actes 8.22
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi.
Marc 7.3-7.4 1 Corinthiens 6.9-6.11 Apocalypse 21.8 1 Corinthiens 3.16-3.17 Ephésiens 5.3-5.6

Jésus et la femme non juive

21 Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.
Josué 19.28-19.29 Juges 1.31 Matthieu 10.5-10.6 Marc 7.24-7.30 Josué 13.6
22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
Matthieu 9.27 Matthieu 17.15 Matthieu 4.24 Ezéchiel 3.6 Psaumes 6.2
23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
Matthieu 14.15 Genèse 42.7 Psaumes 28.1 Deutéronome 8.2 Marc 10.47-10.48
24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Matthieu 10.5-10.6 Romains 15.8 Actes 3.25-3.26 Jérémie 50.6-50.7 Ezéchiel 34.23
25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.
Matthieu 8.2 Osée 12.4 Genèse 32.26 Luc 18.1-18.8 Matthieu 20.31
26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
Philippiens 3.2 Apocalypse 22.15 Marc 7.27-7.28 Actes 22.21-22.22 Galates 2.15
27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
Job 40.4-40.5 1 Timothée 1.13-1.15 Luc 18.13 Luc 15.18-15.19 1 Corinthiens 15.8-15.9
28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.
Matthieu 9.22 Matthieu 8.10 Marc 5.34 Matthieu 8.13 Luc 18.42-18.43
29 Yesu akaondoka huko, akafika kando ya bahari ya Galilaya; akapanda mlimani, akaketi huko.
Matthieu 4.18 Jean 6.1 Matthieu 5.1 Esaïe 9.1 Jean 21.1
30 Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya;
Psaumes 103.3 Matthieu 14.35-14.36 Actes 19.11-19.12 Actes 5.15-5.16 Luc 7.21-7.22
31 hata ule mkutano wakastaajabu, walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, na vipofu wanaona; wakamtukuza Mungu wa Israeli.
Matthieu 9.8 Matthieu 18.8 Marc 9.43 Matthieu 9.33 Luc 14.13

Multiplication des pains pour quatre mille hommes

32 Yesu akawaita wanafunzi wake, akasema, Nawahurumia mkutano, kwa kuwa yapata siku tatu wamekaa pamoja nami, wala hawana kitu cha kula, tena kuwaaga wakifunga sipendi, wasije wakazimia njiani.
Matthieu 9.36 Luc 7.13 Matthieu 20.34 Marc 9.22 Matthieu 12.40
33 Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?
Marc 6.37 Marc 8.4-8.5 Luc 9.13 2 Rois 4.42-4.44 Nombres 11.21-11.22
34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.
Jean 21.9-21.10 Matthieu 16.9-16.10 Luc 24.41-24.42
35 Akawaagiza mkutano waketi chini;
Matthieu 14.19-14.21 Marc 6.39-6.40 Jean 6.10 Luc 9.14-9.16
36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akashukuru akavimega, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.
Romains 14.6 Luc 22.19 Actes 27.35 Jean 6.11 1 Timothée 4.3-4.4
37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.
Marc 8.19-8.21 Matthieu 14.20-14.21 Matthieu 15.33 Luc 1.53 Psaumes 107.9
38 Nao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila wanawake na watoto.
39 Akawaaga makutano, akapanda chomboni, akaenda pande za Magadani.
Marc 8.10 Matthieu 14.22

Cette Bible est dans le domaine public.