Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 4.6
Bible en Swahili de l’est


Fonctions des Lévites

1 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
2 Katika wana wa Lawi uitenge hesabu ya wana wa Kohathi, kwa jamaa zao, na nyumba za baba zao,
Nombres 3.19 Nombres 3.27
3 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi hata umri wa miaka hamsini, wote waingiao katika utumishi huo, ili kufanya kazi ya hema ya kukutania.
Nombres 4.23 Nombres 4.35 Nombres 4.30 1 Chroniques 23.3-23.5 1 Timothée 3.6
4 Huu ndio utumishi wa wana wa Kohathi katika hema ya kukutania, katika vile vyombo vitakatifu sana;
Nombres 4.19 Marc 13.34 Nombres 3.30-3.31 Nombres 4.24 Nombres 4.15
5 hapo watakapong’oa safari, Haruni ataingia ndani, na wanawe, nao watalishusha pazia la sitara, na kulifunika sanduku la ushahidi kwa hilo pazia;
Matthieu 27.51 Hébreux 9.3 Exode 26.31-26.33 Nombres 3.27-3.32 Hébreux 10.20
6 kisha atatia juu yake ngozi za pomboo za kulifunikia, na kutandika juu yake nguo ya rangi ya samawi tupu, kisha watatia hiyo miti yake.
Exode 25.13-25.15 Nombres 4.11-4.13 Nombres 4.7-4.8 Exode 39.1 1 Rois 8.7-8.8
7 Tena juu ya meza ya mikate ya wonyesho watatandika nguo ya rangi ya samawi, na kuweka juu yake sahani, na miiko, na mabakuli, na vikombe vya kumiminia; na hiyo mikate ya daima itakuwa juu yake;
Lévitique 24.5-24.8 Exode 25.23-25.30 Exode 37.10-37.16
8 nao watatandika juu yake nguo ya rangi nyekundu, na kuifunika kwa ngozi za pomboo za kuifunikia, na kuitia ile miti yake.
Nombres 4.6-4.7 Nombres 4.11-4.13 Nombres 4.9
9 Kisha watatwaa nguo ya rangi ya samawi, na kukifunika kinara cha taa ya nuru, na taa zake, na makasi yake, na sahani zake za kutilia makaa, na vyombo vyake vyote vya mafuta, watumiavyo kwa kazi yake;
Exode 25.31-25.39 Psaumes 119.105 Apocalypse 1.20-2.1 Exode 37.17-37.24
10 nao watakitia, na vyombo vyake vyote, ndani ya ngozi ya pomboo, na kukitia juu ya miti ya kukichukulia
Nombres 4.12 Nombres 4.6
11 Tena watatandika nguo ya rangi ya samawi juu ya madhabahu ya dhahabu, na kuifunika kwa ngozi za pomboo, na kuitia ile miti yake;
Exode 37.25-37.28 Exode 40.26-40.27 Exode 30.1-30.19 Exode 39.38 Exode 40.5
12 kisha watavitwaa vile vyombo vyote vya utumishi wavitumiavyo katika mahali patakatifu, na kuvitia katika nguo ya rangi ya samawi, na kuvifunika kwa ngozi za pomboo, na kuvitia juu ya miti ya kuvichukulia.
1 Chroniques 9.29 Nombres 3.8 Nombres 4.7 2 Rois 25.14-25.15 Nombres 4.9
13 Nao watayaondoa hayo majivu madhabahuni; na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake;
Nombres 4.6-4.9 Nombres 4.11-4.12 Lévitique 6.12-6.13 Exode 39.1 Exode 39.41
14 nao wataweka vyombo vyake vyote juu yake ambavyo wavitumia katika madhabahu, vyetezo, na nyuma, na miiko, na mabakuli, vyombo vyote vya hiyo madhabahu; nao watatandika juu yake ngozi za pomboo, na kutia miti yake mahali pake.
Exode 38.1-38.7 2 Chroniques 4.19
15 Na Haruni na wanawe watakapokwisha kupafunika mahali patakatifu, na vyombo vyote vya mahali patakatifu, hapo watakapong’oa kambi; baadaye, wana wa Kohathi watakuja kuvichukua; lakini wasiviguse vile vitu vitakatifu, wasife. Vyombo vile ni mzigo wa wana wa Kohathi katika hema ya kukutania.
2 Samuel 6.6-6.7 Nombres 7.9 1 Chroniques 13.9-13.10 Deutéronome 31.9 Nombres 10.21
16 Na ulinzi wake Eleazari mwana wa Haruni kuhani utakuwa ni kuyaangalia mafuta kwa nuru, na uvumba mzuri, na sadaka ya unga ya daima, na mafuta ya kupaka, tena ulinzi wa hiyo maskani yote, na wa vitu vyote vilivyo ndani yake, mahali patakatifu, na vyombo vyake.
Exode 25.6 Lévitique 24.2 Exode 30.23-30.38 Exode 29.39-29.41 Luc 4.18
17 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
18 Msiitenge kabisa kabila ya jamaa za Wakohathi katika hao Walawi;
Jérémie 38.23 Exode 19.21 Nombres 18.5 Lévitique 10.1-10.2 2 Samuel 6.6-6.7
19 lakini wafanyieni neno hili, ili kwamba wawe hai, wasife, hapo watakapovikaribia vile vitu vilivyo vitakatifu sana; Haruni na wanawe wataingia ndani, na kuwawekea kila mtu utumishi wake, na kila mtu mzigo wake;
Nombres 4.15
20 lakini wasiingie wao kupaona mahali pale patakatifu, hata kwa dakika moja, ili wasife.
1 Samuel 6.19 Exode 19.21 Nombres 4.19 Nombres 4.15 Lévitique 10.2
21 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
22 Fanya jumla ya wana wa Gershoni nao, kwa nyumba za baba zao, na jamaa zao;
Nombres 3.21 Nombres 3.18 Nombres 3.24
23 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini utawahesabu; wote watakaoingia kutumika, ili kufanya kazi katika hema ya kukutania.
Nombres 4.3 1 Corinthiens 9.7 2 Timothée 4.7 Ephésiens 6.10-6.19 Romains 7.14-7.24
24 Huu ni utumishi wa jamaa za Wagershoni, katika kutumika na katika kuchukua mizigo;
Nombres 4.47 Nombres 4.49 Nombres 4.15 Nombres 4.27 Nombres 4.31-4.32
25 wao watayachukua mapazia ya maskani, na hema ya kukutania, hizo nguo za kufunikia, na zile ngozi za pomboo za kufunikia zilizo juu yake, na pazia la mlango wa hema ya kukutania;
Exode 26.14 Nombres 3.25-3.26 Nombres 7.5-7.7
26 na kuta za nguo za ua, na sitara ya ile nafasi ya kuingilia ya lango la ua, ulio karibu na maskani na madhabahu, kuzunguka pande zote, na kamba zake, na vyombo vyote vya utumishi wao, na yote yatakayotendeka kwavyo, watatumika katika hayo.
Exode 35.18 Exode 27.9
27 Utumishi wote wa wana wa Wagershoni, katika mzigo wao wote, na utumishi wao wote, utakuwa kwa amri ya Haruni na wanawe; nanyi mtawaagizia mzigo wao wote kuulinda.
1 Corinthiens 11.2 Luc 1.70
28 Huu ni utumishi wa jamaa za wana wa Wagershoni katika hema kukutania; na ulinzi utakuwa chini ya mkono wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani.
Nombres 4.33 1 Corinthiens 12.5-12.6
29 Katika habari ya wana wa Merari, utawahesabu kwa jamaa zao, na nyumba za baba zao;
Nombres 3.33-3.35
30 tangu aliyepata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini, utawahesabu, kila atakayeingia katika huo utumishi, ili kufanya kazi ya hema ya kukutania.
Nombres 4.23 Nombres 4.3 2 Timothée 2.4 2 Timothée 4.7-4.8 Psaumes 110.1-110.7
31 Na mausia ya mzigo wao ni haya, kwa utumishi wao wote katika hema ya kukutania; mbao za maskani, na mataruma yake, na nguzo zake, na matako yake;
Nombres 3.36-3.37 Nombres 7.8-7.9 Exode 26.15
32 na viguzo vya ua vya kuuzunguka pande zote, na matako yake, na vigingi vyake, na kamba zake, na vyombo vyake vyote, pamoja na utumishi wake wote; nanyi mtawaagizia kila mtu kwa jina lake vile vyombo vya mzigo wao watakaoulinda.
Exode 38.21 Exode 25.9 Exode 38.17 Nombres 7.1 1 Chroniques 9.29
33 Huu ni utumishi wa jamaa za wana wa Merari, kwa utumishi wao wote, katika hema ya kukutania, chini ya mkono wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani.
Nombres 4.28 Esaïe 3.6 Josué 3.6
34 Basi Musa na Haruni na hao wakuu wa mkutano wakawahesabu wana wa Kohathi kwa jamaa zao, na nyumba za baba zao,
35 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini, kila mtu aliyeingia katika utumishi kwa kazi katika hema ya kukutania,
Nombres 4.23 1 Chroniques 23.24 Nombres 4.3 1 Timothée 3.6 Nombres 4.47
36 na waliohesabiwa kwao kwa jamaa zao, walikuwa elfu mbili na mia saba hamsini.
37 Hao ndio waliohesabiwa katika jamaa za Wakohathi, wote waliotumika katika hema ya kukutania, ambao Musa na Haruni waliwahesabu kwa amri ya Bwana kwa mkono wa Musa.
38 Na hao waliohesabiwa katika wana wa Gershoni, kwa jamaa zao na nyumba zao baba zao,
39 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini, kila mtu aliyeingia katika utumishi, kwa kazi katika hema ya kukutania,
40 hata wale waliohesabiwa kwao, kwa jamaa zao na nyumba za baba zao, walikuwa elfu mbili na mia sita na thelathini.
Nombres 3.32
41 Hao ndio waliohesabiwa katika jamaa za wana wa Gershoni, wote waliotumika katika hema ya kukutania, ambao Musa na Haruni waliwahesabu kwa amri ya Bwana.
42 Na hao waliohesabiwa katika jamaa za wana wa Merari, kwa jamaa zao, na nyumba za baba zao,
43 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini, kila mtu aliyeingia katika utumishi kwa kazi katika hema ya kukutania,
44 wale waliohesabiwa kwao, kwa jamaa zao, walikuwa elfu tatu na mia mbili.
Deutéronome 33.25 1 Corinthiens 10.13 1 Corinthiens 12.8-12.12 2 Corinthiens 12.9-12.10 Nombres 3.34
45 Hao ndio waliohesabiwa katika jamaa za wana wa Merari, ambao Musa na; Haruni waliwahesabu kwa amri ya Bwana, kwa mkono wa Musa.
Nombres 4.29
46 Wote waliohesabiwa katika Walawi, ambao Musa na Haruni na hao wakuu wa Israeli waliwahesabu, kwa jamaa zao, na nyumba za baba zao,
47 tangu waliopata umri wa miaka thelathini na zaidi, hata umri wa miaka hamsini, kila aliyeingia kufanya kazi ya utumishi, na kazi ya kuchukua mizigo katika hema ya kukutania,
Nombres 4.3 Romains 12.6-12.8 Nombres 4.23-4.24 1 Chroniques 23.3 Nombres 4.30
48 hao waliohesabiwa kwao, walikuwa elfu nane na mia tano themanini.
Nombres 3.39 Matthieu 20.16 Matthieu 22.15 Matthieu 7.14
49 Kwa amri ya Bwana, walihesabiwa kwa mkono wa Musa, kila mtu kwa utumishi wake, na kama mzigo wake ulivyokuwa; ndivyo walivyohesabiwa na yeye, kama Bwana alivyomwagiza Musa.
Nombres 4.15 Nombres 4.21 Nombres 4.31 Nombres 4.24 Esaïe 42.1-42.7

Cette Bible est dans le domaine public.