Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 18.23
Bible en Swahili de l’est


Fonctions et revenus des prêtres et des Lévites

1 Bwana akamwambia Haruni, Wewe na wanao na nyumba ya baba zako pamoja nawe mtachukua uovu wa patakatifu; wewe na wanao pamoja nawe mtauchukua ukuhani wenu.
Exode 28.38 Nombres 14.34 Esaïe 53.6 Nombres 17.13 Lévitique 22.9
2 Na ndugu zako nao, kabila ya Lawi, kabila ya baba yako, uwalete karibu pamoja nawe, ili waungwe nawe, na kukuhudumia; bali wewe na wanao pamoja nawe mtakuwa mbele ya hema ya ushahidi.
Nombres 18.4 Genèse 29.34 Ezéchiel 44.15 2 Chroniques 30.16 1 Chroniques 16.39-16.40
3 Nao watashika ulinzi kwa amri yako, na ulinzi wa Hema yote; lakini wasikaribie vyombo vya patakatifu, wala madhabahu, wasife, wao pamoja na ninyi.
Nombres 4.15 Nombres 16.40 Nombres 4.19-4.20 Nombres 3.36 Nombres 3.31
4 Nao wataungwa nawe, na kuushika ulinzi wa hema ya kukutania, kwa ajili ya utumishi wote wa hema; na mgeni asiwakaribie ninyi.
1 Samuel 6.19 Nombres 3.10 Nombres 1.51 2 Samuel 6.6-6.7
5 Nanyi mtashika ulinzi wa patakatifu, na ulinzi wa madhabahu, isiwe ghadhabu juu ya wana wa Israeli tena.
Exode 27.21 Lévitique 24.3 Nombres 16.46 Jérémie 23.15 Exode 30.7-30.10
6 Nami, tazama, nimewatwaa ndugu zenu Walawi miongoni mwa wana wa Israeli; kwenu ninyi watu hao ni kipawa alichopewa Bwana, waufanye utumishi wa hema ya kukutania.
Nombres 3.9 Nombres 3.45 Nombres 3.12 Genèse 9.9 Exode 14.17
7 Nawe na wanao pamoja nawe mtautunza ukuhani wenu, kwa ajili ya kila kitu cha madhabahu, na kwa ajili ya vile vilivyomo ndani ya pazia, nanyi mtatumika. Nawapeni ukuhani kuwa utumishi wa kipawa; na mgeni akaribiaye atauawa.
Nombres 3.10 Nombres 3.38 Hébreux 9.3-9.6 Ephésiens 3.8 1 Samuel 2.28
8 Kisha Bwana akamwambia Haruni, Tazama, nimekupa wewe ulinzi wa sadaka zangu za kuinuliwa, maana, vitu vyote vya hao wana wa Israeli vilivyowekwa wakfu; nimekupa wewe na wanao vitu hivyo kwa ajili ya kule kutiwa mafuta kwenu, kuwa haki yenu milele.
Lévitique 6.16 Lévitique 6.18 Exode 40.13 Lévitique 7.6 Exode 40.15
9 Vitu hivi vitakuwa vyako katika vile vilivyo vitakatifu sana, visiteketezwe motoni; matoleo yao yote, maana, kila sadaka yao ya unga, na kila sadaka yao ya dhambi, na kila sadaka yao ya hatia watakayonitolea, vitakuwa vitakatifu sana kwa ajili yako wewe na kwa wanao.
Lévitique 7.7 Lévitique 6.25-6.26 Lévitique 4.22 Lévitique 4.27 Lévitique 14.13
10 Utakula vitu hivyo kuwa ni vitu vitakatifu sana; kila mume atakula vitu hivyo; vitakuwa vitakatifu kwako wewe.
Lévitique 7.6 Lévitique 6.29 Lévitique 6.16 Lévitique 10.13 Exode 29.31-29.32
11 Tena kitu hiki ni chako; ile sadaka ya kuinuliwa ya kipawa chao, maana, sadaka za kutikiswa zote za wana wa Israeli; hizi nimekupa wewe, na wanao na binti zako pamoja nawe, ni haki yenu milele; kila mtu katika nyumba yako aliye safi atakula katika hizo.
Deutéronome 18.3 Exode 29.27-29.28 Lévitique 10.14 Lévitique 7.30-7.34 Lévitique 7.14
12 Yaliyo mazuri katika mafuta, na yaliyo mazuri ya mavuno ya zabibu, na ya mavuno ya nafaka, malimbuko yake watakayompa Bwana, amekupa wewe hayo.
Deutéronome 18.4 Exode 23.19 Exode 34.26 Lévitique 23.17 Exode 22.29
13 Matunda ya kwanza yaivayo katika yote yaliyo katika nchi yao, watakayomletea Bwana, yatakuwa yako, kila mtu aliye safi katika nyumba yako atakula katika vitu hivyo.
Exode 22.29 Osée 9.10 Jérémie 24.2 Exode 23.19 Michée 7.1
14 Kila kitu kilichowekwa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
Lévitique 27.28 Ezéchiel 44.29
15 Kila kifunguacho tumbo, cha wenye mwili wote watakachomsongezea Bwana cha wanadamu na cha wanyama, ni chako; lakini mzaliwa wa kwanza wa binadamu, huna budi utamkomboa, na mzaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi utamkomboa.
Exode 34.20 Exode 13.2 Exode 13.12-13.13 Nombres 3.46 Lévitique 27.26-27.27
16 Na hao watakaokombolewa katika wanyama hao, tangu aliyepata umri wa mwezi mmoja utamkomboa, kama utakavyohesabu kima chake, kwa fedha ya shekeli tano, kwa shekeli ya mahali patakatifu (nayo ni gera ishirini).
Exode 30.13 Nombres 3.47 Lévitique 27.25 Ezéchiel 45.12 Lévitique 27.2-27.7
17 Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe, au mzaliwa wa kwanza wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, hutawakomboa hao; maana, ni watakatifu hao; utanyunyiza damu yao katika madhabahu, na kuyateketeza mafuta yao kuwa sadaka iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto, iwe harufu ya kupendeza.
Exode 29.16 Deutéronome 15.19-15.22 Lévitique 3.2-3.5
18 Tena nyama yao itakuwa ni yako wewe, kama kile kidari cha kutikiswa, na kama mguu wa nyuma wa upande wa kuume, itakuwa yako.
Exode 29.26-29.28 Lévitique 7.31-7.34
19 Sadaka zote za kuinuliwa za vitu vitakatifu, wana wa Israeli wavisongezavyo kwa Bwana, nimekupa wewe na wanao na binti zako pamoja nawe, ni haki yenu ya milele; ni agano la chumvi la milele mbele za Bwana kwa ajili yako, na kizazi chako pamoja nawe.
2 Chroniques 13.5 Lévitique 2.13 Nombres 18.11 Deutéronome 12.6 Nombres 31.41
20 Kisha Bwana akamwambia Haruni, Wewe hutakuwa na urithi katika nchi yao, wala hutakuwa na fungu lo lote kati yao; mimi ni fungu lako, na urithi wako, katika wana wa Israeli.
Ezéchiel 44.28 Deutéronome 10.9 Josué 13.33 Deutéronome 14.27 Josué 14.3
21 Na wana wa Lawi, nimewapa zaka yote katika Israeli kuwa urithi wao, badala ya huo utumishi wautumikao, maana, ni huo utumishi wa hema ya kukutania.
Néhémie 10.37 Deutéronome 14.22-14.29 Néhémie 12.44 2 Chroniques 31.5-31.6 Lévitique 27.30-27.33
22 Mwanzo wa sasa wana wa Israeli wasikaribie hema ya kukutania, wasije wakachukua dhambi, nao wakafa.
Lévitique 22.9 Nombres 1.51-1.52 Nombres 18.7 Nombres 3.38 Nombres 3.10
23 Lakini Walawi watatumika utumishi wa hema ya kukutania, nao watauchukua uovu wao; hii itakuwa amri ya milele katika vizazi vyenu vyote, na kati ya wana wa Israeli hawatakuwa na urithi.
Nombres 3.7 Nombres 18.20 Nombres 18.1
24 Kwa kuwa zaka ya wana wa Israeli, waisongezayo kuwa sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana, nimewapa Walawi kuwa urithi wao; kwa hiyo nimewaambia, ya kwamba, katika wana wa Israeli hawatakuwa na urithi uwao wote.
Nombres 18.26 Malachie 3.8-3.10
25 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
26 Tena utanena na Walawi, na kuwaambia, Hapo mtakapoitwaa zaka mkononi mwa wana wa Israeli niliyowapa ninyi kutoka kwao kuwa urithi wenu, ndipo mtakaposongeza sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana katika hiyo, iwe zaka katika hiyo zaka.
Néhémie 10.38 Nombres 18.21
27 Na sadaka yenu ya kuinuliwa itahesabiwa kwenu, kama ndiyo nafaka ya sakafu ya kupuria, na kama kujaa kwake kinu cha kushindikia zabibu.
Nombres 18.30 Nombres 15.20 2 Rois 6.27 Deutéronome 15.14 Osée 9.1-9.2
28 Hivyo ninyi nanyi mtasongeza sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana katika zaka zenu zote, mpokeazo mikononi mwa wana wa Israeli; kwa hiyo mtampa Haruni kuhani hiyo sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
Genèse 14.18 Hébreux 6.20-7.10
29 Katika vipawa vyenu vyote mtasongeza kila sadaka ya kuinuliwa ya Bwana, ya wema wake wote, hiyo sehemu yake iliyowekwa takatifu.
30 Kwa ajili ya hayo utawaambia, Mtakapoinua humo hayo yaliyo mema, ndipo yatahesabiwa kuwa ya Walawi, kama kuongea kwake sakafu ya kupuria nafaka, na kama maongeo ya kinu cha kushindikia zabibu.
Genèse 43.11 Deutéronome 6.5 Malachie 1.8 Philippiens 3.8-3.9 Matthieu 6.33
31 Nanyi mtakula hayo kila mahali, ninyi na watu wa nyumbani mwenu; kwa kuwa ni thawabu yenu badala ya utumishi wenu katika hema ya kukutania.
Luc 10.7 1 Timothée 5.17-5.18 1 Corinthiens 9.10-9.14 Matthieu 10.10 Deutéronome 14.22-14.23
32 Nanyi hamtachukua dhambi kwa ajili yake, hapo mtakapokwisha kuinua humo hayo mema yake; lakini msivitie unajisi vile vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, ili msife.
Lévitique 19.8 Lévitique 22.2 Lévitique 22.15-22.16 1 Corinthiens 11.29 1 Corinthiens 11.27

Cette Bible est dans le domaine public.