Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 8.8
Bible en Swahili de l’est


Restauration et bénédiction

1 Neno la Bwana wa majeshi likanijia, kusema,
2 Bwana wa majeshi asema hivi, Mimi nina wivu kwa ajili ya Sayuni, wivu mkuu, nami nina wivu kwa ajili yake kwa ghadhabu kuu.
Esaïe 59.17 Ezéchiel 36.5-36.6 Esaïe 42.13-42.14 Nahum 1.6 Psaumes 78.58-78.59
3 Bwana asema hivi, Mimi nimerudi Sayuni, nami nitakaa katikati ya Yerusalemu; na Yerusalemu utaitwa, Mji wa kweli; na Mlima wa Bwana wa majeshi utaitwa, Mlima mtakatifu.
Zacharie 1.16 Zacharie 2.10-2.11 Esaïe 1.26 Apocalypse 21.10 Ezéchiel 48.35
4 Bwana wa majeshi asema hivi, Wazee wanaume na wazee wanawake watakaa tena katika njia za Yerusalemu, kila mtu ana mkongojo wake mkononi, kwa kuwa ni mzee sana.
Job 42.17 Lamentations 5.11-5.15 Esaïe 65.20-65.22 1 Samuel 2.31 Lamentations 2.20-2.22
5 Na hizo njia za mji zitajaa wavulana, na wasichana, wakicheza katika njia zake.
Jérémie 30.19-30.20 Jérémie 31.13 Psaumes 144.12-144.15 Jérémie 33.11 Zacharie 2.4
6 Bwana wa majeshi asema hivi, Ingawa hili ni neno lililo gumu mbele ya macho ya mabaki ya watu hawa katika siku hizo, je! Liwe neno gumu mbele ya macho yangu? Asema Bwana wa majeshi.
Jérémie 32.17 Jérémie 32.27 Psaumes 118.23 Genèse 18.14 Luc 18.27
7 Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama, nitawaokoa watu wangu toka nchi ya mashariki, na toka nchi ya magharibi;
Esaïe 49.12 Esaïe 27.12-27.13 Esaïe 59.19 Romains 11.25-11.27 Psaumes 50.1
8 nami nitawaleta, nao watakaa katikati ya Yerusalemu; nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, katika kweli na katika haki.
Jérémie 4.2 Ezéchiel 36.28 Ezéchiel 11.20 Ezéchiel 37.25 Jérémie 31.33
9 Bwana wa majeshi asema hivi, Mikono yenu na iwe hodari, ninyi mnaosikia siku hizi maneno haya kwa vinywa vya manabii, waliokuwapo siku hiyo ulipowekwa msingi wa nyumba ya Bwana wa majeshi; yaani, hekalu hilo; ili lijengwe.
Esdras 5.1-5.2 1 Chroniques 22.13 Esaïe 35.4 Aggée 1.12 Aggée 2.21
10 Maana kabla ya siku zile hapakuwa na ijara kwa mwanadamu, wala hapakuwa na ijara kwa mnyama; wala hapakuwa na amani kwake yeye aliyetoka, wala kwake yeye aliyeingia, kwa sababu ya adui; nami nalimwacha kila mtu kugombana na jirani yake.
Aggée 2.16-2.18 Amos 9.4 Esaïe 19.2 Amos 3.6 Jérémie 16.16
11 Lakini sasa sitakuwa kwa mabaki ya watu hawa kama nilivyokuwa siku zile za kwanza, asema Bwana wa majeshi.
Esaïe 12.1 Aggée 2.19 Psaumes 103.9 Zacharie 8.8-8.9 Esaïe 11.13
12 Kwa maana itakuwako mbegu ya amani; mzabibu utatoa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na hizo mbingu zitatoa umande wake; nami nitawarithisha mabaki ya watu hawa vitu hivi vyote.
Genèse 27.28 Lévitique 26.4-26.5 Deutéronome 33.13 Joël 2.22 Esaïe 61.7
13 Kisha itakuwa, kama vile mlivyokuwa laana katika mataifa, Ee nyumba ya Yuda, na nyumba ya Israeli, ndivyo nitakavyowaokoa, nanyi mtakuwa baraka; msiogope, lakini mikono yenu na iwe hodari.
Zacharie 8.9 Jérémie 42.18 Genèse 12.2-12.3 Psaumes 72.17 Ezéchiel 5.15
14 Maana Bwana wa majeshi asema hivi, Kama vile nilivyoazimia kuwatenda ninyi mabaya, baba zenu waliponikasirisha, asema Bwana wa majeshi, wala mimi sikujuta;
Jérémie 31.28 Ezéchiel 24.14 Jérémie 4.28 Psaumes 33.11 Zacharie 1.6
15 vivyo hivyo nimeazimia katika siku hizi kuutendea Yerusalemu mema, na nyumba ya Yuda pia; msiogope.
Zacharie 8.13 Michée 7.18-7.20 Esaïe 43.1-43.2 Michée 4.10-4.13 Jérémie 32.42
16 Haya ndiyo mtakayoyatenda; kila mtu na aseme kweli na jirani yake; hukumuni kweli na hukumu ya amani malangoni mwenu;
Zacharie 7.9 Ephésiens 4.25 Psaumes 15.2 Zacharie 8.19 Proverbes 12.17
17 wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema Bwana.
Proverbes 3.29 Zacharie 7.10 Proverbes 6.16-6.19 Matthieu 15.19 Habakuk 1.13
18 Tena neno la Bwana wa majeshi likanijia, kusema,
19 Bwana wa majeshi asema hivi, Saumu ya mwezi wa nne, na saumu ya mwezi wa tano, na saumu ya mwezi wa saba, na saumu ya mwezi wa kumi, zitakuwa furaha na shangwe, na sikukuu za kuchangamkia, kwa nyumba ya Yuda; basi zipendeni kweli na amani.
Zacharie 7.5 Jérémie 39.2 Zacharie 8.16 2 Rois 25.25 Psaumes 30.11
20 Bwana wa majeshi asema hivi, Itatokea halafu ya kwamba watakuja mataifa na wenyeji wa miji mingi;
Zacharie 2.11 Jérémie 16.19 Psaumes 138.4-138.5 Osée 1.10 Esaïe 66.18-66.20
21 wenyeji wa mji huu watauendea mji huu, wakisema, Haya! Twendeni zetu kwa haraka tuombe fadhili za Bwana, na kumtafuta Bwana wa majeshi; Mimi nami nitakwenda.
Zacharie 7.2 Osée 6.3 Psaumes 146.1-146.2 Psaumes 103.22 Psaumes 122.1-122.9
22 Naam, watu wa kabila nyingi na mataifa hodari watakuja Yerusalemu kumtafuta Bwana wa majeshi, na kuomba fadhili za Bwana.
Zacharie 8.21 Apocalypse 21.24 Apocalypse 15.4 Esaïe 25.7 Esaïe 55.5
23 Bwana wa majeshi asema hivi, Siku hizo watu kumi, wa lugha zote za mataifa, wataushika upindo wa nguo yake yeye aliye Myahudi; naam, wataushika wakisema, Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.
1 Corinthiens 14.25 Genèse 31.7 Esaïe 66.18 Esaïe 45.14 Actes 13.47-13.48

Cette Bible est dans le domaine public.