Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jonas 2.5
Bible en Swahili de l’est


Jonas dans le poisson

1 Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,
Psaumes 130.1-130.2 Job 13.15 Actes 16.24-16.25 Osée 5.15-6.3 Lamentations 3.53-3.56
2 Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu naliomba, Nawe ukasikia sauti yangu.
Psaumes 18.4-18.6 Psaumes 120.1 Psaumes 34.6 Psaumes 65.2 Matthieu 12.40
3 Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.
Psaumes 42.7 Lamentations 3.54 Psaumes 69.14-69.15 Psaumes 69.1-69.2 Psaumes 88.5-88.8
4 Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako; Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.
Psaumes 31.22 Psaumes 5.7 2 Chroniques 6.38 Jérémie 7.15 Daniel 6.10
5 Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu; Vilindi vilinizunguka; Mwani ulikizinga kichwa changu;
Psaumes 69.1-69.2 Lamentations 3.54 Psaumes 40.2
6 Nalishuka hata pande za chini za milima; Hiyo nchi na mapingo yake yalinifunga hata milele; Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni, Ee Bwana, Mungu wangu,
Psaumes 30.3 Psaumes 16.10 Esaïe 38.17 Esaïe 40.12 Psaumes 55.23
7 Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka Bwana; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu.
Psaumes 11.4 Psaumes 18.6 2 Chroniques 30.27 Habakuk 2.20 Jonas 2.4
8 Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo Hujitenga na rehema zao wenyewe;
Psaumes 31.6 Jérémie 2.13 2 Rois 17.15 Jérémie 10.8 1 Samuel 12.21
9 Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa Bwana.
Psaumes 3.8 Psaumes 50.14 Osée 14.2 Ecclésiaste 5.4-5.5 Esaïe 45.17
10 Bwana akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.
Matthieu 8.8-8.9 Jonas 1.17 Genèse 1.9 Genèse 1.7 Psaumes 105.31

Cette Bible est dans le domaine public.