Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 3.9
Bible en Swahili de l’est


Raisons du jugement

Impossibilité d’échapper au jugement

1 Lisikieni neno hili alilolisema Bwana juu yenu, enyi wana wa Israeli, juu ya jamaa yote niliowapandisha kutoka nchi ya Misri, nikisema,
Amos 2.10 Jérémie 8.3 2 Chroniques 20.15 Michée 3.1 Osée 5.1
2 Ni ninyi tu niliowajua katika jamaa zote zilizo duniani; kwa sababu hiyo nitawapatiliza ninyi maovu yenu yote.
Deutéronome 7.6 Exode 19.5-19.6 1 Pierre 4.17 Romains 2.9 Deutéronome 10.15
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
2 Corinthiens 6.14-6.16 Genèse 17.1 Genèse 6.9 Genèse 5.22
4 Je! Simba atanguruma mwituni, asipokuwa na mawindo? Mwana-simba atalia pangoni mwake, ikiwa hakupata kitu?
Psaumes 104.21 Osée 11.10 Amos 1.2 Amos 3.8 Osée 5.14
5 Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu cho chote?
Ecclésiaste 9.12 Jérémie 31.28 Daniel 9.14
6 Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta Bwana?
Esaïe 45.7 Esaïe 14.24-14.27 Sophonie 1.16 Genèse 50.20 Jérémie 4.5
7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
Jean 15.15 Genèse 18.17 Genèse 6.13 Psaumes 25.14 Apocalypse 4.1
8 Simba amekwisha kunguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana MUNGU amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri?
Amos 3.4 Jérémie 20.9 Actes 4.20 Amos 7.12-7.17 Amos 2.12
9 Tangazeni habari katika majumba ya Ashdodi, na katika majumba ya nchi ya Misri, mkaseme, Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria, katazameni, ni mishindo mikubwa kama nini iliyomo humo, na udhalimu mwingi kama nini uliomo ndani yake.
Amos 4.1 Amos 6.1 Amos 1.8 1 Samuel 5.1 Amos 8.6
10 Kwa maana hawajui kutenda haki, asema Bwana, hao wawekao akiba ya jeuri na unyang’anyi katika majumba yao.
Sophonie 1.9 Jérémie 4.22 Zacharie 5.3-5.4 Psaumes 14.4 Jacques 5.3-5.4
11 Basi, haya ndiyo asemayo Bwana MUNGU; Atakuwako adui, kuizunguka nchi pande zote; naye atazishusha chini nguvu zako zikutoke; na majumba yako yatatekwa nyara.
Amos 2.5 Amos 6.14 2 Rois 17.3-17.6 2 Rois 18.9-18.11 Amos 3.15
12 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao Samaria katika pembe ya semadari, na juu ya mito ya hariri ya kitanda.
1 Samuel 17.34-17.37 Amos 6.4 1 Rois 22.25 1 Rois 20.34 Esaïe 8.4
13 Sikieni, mkashuhudu juu ya nyumba ya Yakobo, asema Bwana, MUNGU wa majeshi.
1 Thessaloniciens 4.6 Josué 22.22 Amos 5.27 Deutéronome 30.18-30.19 2 Rois 17.13
14 Kwani katika siku ile nitakapompatiliza Israeli makosa yake, nitazipatiliza pia madhabahu za Betheli, na pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali, na kuanguka chini.
2 Rois 23.15 Osée 10.5-10.8 Osée 10.14-10.15 2 Chroniques 31.1 Exode 32.34
15 Nami nitaipiga nyumba ya wakati wa baridi pamoja na nyumba ya wakati wa hari; na hizo nyumba za pembe zitaangamia, nazo nyumba kubwa zitakuwa na mwisho, asema Bwana.
1 Rois 22.39 Jérémie 36.22 Juges 3.20 Amos 6.11 Esaïe 5.9

Cette Bible est dans le domaine public.