Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 7.30
Bible en Swahili de l’est


1 Na sheria ya hiyo sadaka ya hatia ni hii; ni takatifu sana.
Lévitique 6.17 Lévitique 6.25 Lévitique 5.1-5.6 Lévitique 5.14-6.7 Lévitique 21.22
2 Wataichinja sadaka ya hatia pale pale waichinjapo sadaka ya kuteketezwa; na damu yake atainyunyiza katika madhabahu pande zote.
Lévitique 1.5 Lévitique 6.25 Lévitique 1.11 Lévitique 3.2 Nombres 6.12
3 Katika sadaka hiyo atasongeza mafuta yake yote; yaani, mkia wake wenye mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo,
Exode 29.13 Lévitique 3.15-3.16 Lévitique 3.3-3.5 Psaumes 51.6 Lévitique 4.8-4.10
4 na figo zake mbili, na mafuta yaliyoshikamana nazo, yaliyo karibu na kiuno chake, na kitambi kilicho katika ini, pamoja na figo zake mbili, hayo yote atayaondoa;
Lévitique 3.4
5 na kuhani atayateketeza juu ya madhabahu, kuwa dhabihu kwa Bwana kwa njia ya moto; ni sadaka ya hatia.
Galates 2.20 Lévitique 1.9 1 Pierre 4.1-4.2 Lévitique 3.16 Lévitique 2.2
6 Kila mtu mume miongoni mwa makuhani atakula katika sadaka hiyo; italiwa katika mahali patakatifu; ni takatifu sana.
Lévitique 6.29 Nombres 18.9-18.10 Lévitique 2.3 Lévitique 6.16-6.18
7 Kama hiyo sadaka ya dhambi ilivyo, na sadaka ya hatia ni vivyo; sheria yake ni moja; huyo kuhani afanyaye upatanisho kwayo, ndiye atakayekuwa nayo.
Lévitique 6.25-6.26 Lévitique 14.13 1 Corinthiens 9.13
8 Tena kuhani atakayesongeza sadaka ya kuteketezwa ya mtu awaye yote, huyo kuhani atatwaa awe nayo ngozi ya huyo mnyama wa sadaka ya kuteketezwa aliyemsongeza.
Genèse 3.21 Romains 13.14 Nombres 19.5 Lévitique 1.6 Lévitique 4.11
9 Na kila sadaka ya unga iliyookwa mekoni, na yote yaliyoandaliwa chunguni, au kaangoni, yote yatakuwa ya huyo kuhani aliyeyasongeza.
Ezéchiel 44.29 Lévitique 2.10 Nombres 18.9 1 Corinthiens 9.13 Lévitique 5.13
10 Na kila sadaka ya unga, kama umeandaliwa na mafuta, au kama ni mkavu, watautwaa wana wote wa Haruni kuutumia, kila mtu sawasawa.
2 Corinthiens 8.14 Exode 16.18
11 Na sheria ya matoleo ya sadaka za amani, atakazosongeza mtu kwa Bwana, ni hii.
Lévitique 3.1-3.17 Lévitique 22.18-22.21 Ezéchiel 45.15
12 Kwamba aitoa kwa ajili ya shukrani, ndipo atakaposongeza pamoja na hiyo sadaka ya shukrani mikate isiyotiwa chachu, iliyoandaliwa na mafuta, na mikate ya kaki isiyochachwa iliyopakwa mafuta, na mikate ya unga mwembamba uliolowama mafuta.
Lévitique 2.4 Nombres 6.15 2 Chroniques 33.16 Lévitique 7.15 2 Chroniques 29.31
13 Ataleta matoleo yake, pamoja na mikate iliyotiwa chachu, na pamoja na sadaka zake za amani, kwa ajili ya shukrani.
Amos 4.5 Lévitique 23.17 1 Timothée 4.4 Matthieu 13.33
14 Na katika hayo atasongeza kimoja katika kila toleo kiwe sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana; itakuwa ni ya kuhani atakayeinyunyiza hiyo damu ya sadaka za amani.
Nombres 18.19 Exode 29.27-29.28 Nombres 31.29 Nombres 31.41 Nombres 18.24-18.32
15 Na hiyo nyama ya sadaka zake za amani zilizochinjwa kwa ajili ya shukrani italiwa siku iyo hiyo ya matoleo yake; asisaze yo yote hata asubuhi.
Lévitique 22.29-22.30
16 Lakini kwamba hii sadaka ya matoleo yake ni nadhiri, au sadaka ya hiari, italiwa siku hiyo aliyoileta sadaka yake; kisha siku ya pili yake kitakachosalia kitaliwa;
Deutéronome 12.6 Lévitique 19.5-19.8 Deutéronome 12.26 Nombres 15.3 Ezéchiel 46.12
17 lakini hicho kitakachosalia, katika hizo nyama za sadaka, hata siku ya tatu kitachomwa moto.
Exode 12.10 1 Corinthiens 15.4 Osée 6.2 Genèse 22.4 Lévitique 6.22-6.23
18 Tena kama nyama yo yote katika hiyo dhabihu yake ya sadaka za amani ikiliwa siku ya tatu, haitakubaliwa, wala haitahesabiwa kwake huyo mwenye kuisongeza; itakuwa ni machukizo, na mtu atakayeila atachukua uovu wake.
Lévitique 19.7-19.8 Lévitique 22.25 Nombres 18.27 Lévitique 11.41 Romains 4.11
19 Tena nyama itakayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa; itachomwa moto. Na katika hiyo nyama nyingine, kila mtu aliye safi ana ruhusa kuila;
Nombres 19.11-19.16 Romains 14.20 Lévitique 11.24-11.39 Actes 10.15-10.16 Tite 1.15
20 lakini mtu huyo atakayekula katika nyama ya sadaka za amani, ambazo ni za Bwana, na unajisi wake akiwa nao juu yake, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
1 Corinthiens 11.28 Lévitique 22.3-22.7 Lévitique 15.2-15.33 Genèse 17.14
21 Kisha mtu awaye yote atakapogusa kitu cho chote kilicho najisi, uchafu wa binadamu, au mnyama aliye najisi, au machukizo yo yote yaliyo najisi, kisha akala nyama ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo ni za Bwana, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
Lévitique 5.2-5.3 Lévitique 11.10-11.13 Lévitique 11.20 Lévitique 15.1-15.33 Lévitique 12.1-13.59
22 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
23 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Msile mafuta yo yote, ya ng’ombe, wala ya kondoo, wala ya mbuzi.
Lévitique 3.16-3.17 Lévitique 17.6 Romains 8.13 1 Samuel 2.15-2.17 1 Samuel 2.29
24 Tena mafuta ya mnyama afaye mwenyewe, na mafuta ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama, mna ruhusa kuyatumia kwa ajili ya matumizi mengine; lakini msiyale kabisa.
Exode 22.31 Lévitique 17.15 Lévitique 22.8 Deutéronome 14.21 Ezéchiel 4.14
25 Kwani huyo mtu atakayekula mafuta ya mnyama, ambaye ni katika wanyama ambao watu husongeza sadaka kwa Bwana kwa moto, mtu huyo atakayekula mafuta hayo atakatiliwa mbali na watu wake.
26 Tena msiile damu yo yote, ama ya ndege, ama ya mnyama, katika nyumba zenu zote.
Genèse 9.4 Lévitique 17.10-17.14 Actes 15.20 Lévitique 3.17 Actes 15.29
27 Mtu ye yote alaye damu, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.
Lévitique 7.25 Hébreux 10.29 Lévitique 7.20-7.21
28 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
29 Nena na wana wa Israeli uwaambie, Yeye asongezaye dhabihu yake ya sadaka za amani kwa Bwana, atamletea Bwana matoleo yake, kutoka katika ile dhabihu ya sadaka zake za amani;
1 Jean 1.7 Lévitique 3.1-3.17 Colossiens 1.20
30 mikono yake mwenyewe itamletea hizo sadaka za kusongezwa kwa moto; mafuta yake pamoja na kidari atayaleta, ili kwamba hicho kidari kitikiswe kuwa sadaka ya kutikiswa mbele ya Bwana.
Nombres 6.20 Lévitique 3.9 Lévitique 3.3-3.4 Lévitique 3.14 Lévitique 8.27
31 Kuhani atayateketeza hayo mafuta juu ya madhabahu; lakini hicho kidari kitakuwa cha Haruni na cha wanawe.
Lévitique 3.16 Lévitique 3.5 Lévitique 3.11 Lévitique 7.34 Lévitique 8.29
32 Mguu wa nyuma wa upande wa kuume mtampa kuhani kuwa sadaka ya kuinuliwa kutoka katika hizo sadaka zenu za amani.
Lévitique 9.21 Lévitique 7.34 Nombres 6.20 Lévitique 8.25-8.26 Lévitique 10.14
33 Katika wana wa Haruni, huyo atakayeisongeza damu ya sadaka za amani, na mafuta yake, yeye atapata mguu wa nyuma wa upande wa kuume kuwa sehemu yake.
Lévitique 6.1-6.30 Lévitique 7.3 Lévitique 26.1-26.46
34 Kwa maana, hicho kidari cha kutikiswa, na huo mguu wa kuinuliwa, nimevitwaa kwa wana wa Israeli, katika dhabihu zao za sadaka za amani, nami nimempa Haruni kuhani na wanawe, kuwa haki yao ya milele kutoka kwa wana wa Israeli.
Nombres 18.18-18.19 Lévitique 10.14-10.15 Exode 29.9 Exode 29.27-29.28 Lévitique 3.17
35 Hii ndiyo sehemu ya Haruni, na sehemu ya wanawe, katika kutiwa mafuta kwao, katika hizo dhabihu zisongezwazo kwa Bwana kwa njia ya moto, siku hiyo aliyowaweka ili wamtumikie Bwana katika kazi ya ukuhani;
Exode 40.13-40.15 Exode 29.7 Lévitique 8.10-8.12 Exode 28.1 1 Jean 2.27
36 sehemu ambayo Bwana aliagiza wapewe na wana wa Israeli, siku hiyo aliyowatia mafuta. Ni haki yao ya milele katika vizazi vyao vyote.
Lévitique 8.12 Lévitique 8.30 Exode 40.13-40.15
37 Sheria ya sadaka ya kuteketezwa ni hii, na ya sadaka ya unga, na ya sadaka ya dhambi, na ya sadaka ya hatia, na ya kuwekwa wakfu, na ya sadaka za amani;
Exode 29.1 Lévitique 6.9-6.18 Exode 29.38-29.42 Lévitique 7.11-7.21 Lévitique 6.20-7.7
38 ambazo Bwana alimwagiza Musa katika mlima wa Sinai, siku hiyo aliyowaagiza wana wa Israeli wamtolee Bwana matoleo yao, huko katika jangwa la Sinai.
Lévitique 1.1-1.2

Cette Bible est dans le domaine public.