Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 21.15
Bible en Swahili de l’est


Règlements concernant les prêtres

1 Kisha Bwana akamwambia Musa, Nena na hao makuhani, wana wa Haruni, uwaambie, Mtu asijinajisi kwa ajili ya wafu katika watu wake;
Ezéchiel 44.25 Lévitique 21.11 Nombres 19.14 Lévitique 10.6-10.7 Lévitique 19.28
2 isipokuwa ni kwa ajili ya jamaa yake wa karibu, kwa ajili ya mama yake, na kwa ajili baba yake, na kwa ajili ya mwanawe, na kwa ajili ya binti yake, na kwa ajili ya nduguye mwanamume;
1 Thessaloniciens 4.13 Lévitique 18.6
3 na kwa ajili ya umbu lake aliye mwanamwali, aliye wa udugu kwake, ambaye hajaolewa na mume; ana ruhusa kujitia unajisi kwa ajili yake huyo.
4 Asijitie unajisi, ijapokuwa ni mkubwa katika watu wake, hata akajinajisi.
Ezéchiel 24.16-24.17
5 Wasijifanyie upaa kichwani, wala wasinyoe pembe za ndevu zao, wala wasichanje chale katika miili yao.
Deutéronome 14.1 Ezéchiel 44.20 Lévitique 19.27-19.28 Esaïe 22.12 Jérémie 16.6
6 Watakuwa watakatifu kwa Mungu wao, wala wasilinajisi jina la Mungu wao; kwa kuwa wao ndio wasongezao sadaka za Bwana kwa njia ya moto, chakula cha Mungu wao; kwa ajili ya hayo watakuwa watakatifu.
Lévitique 3.11 Lévitique 18.21 Malachie 1.6-1.7 Lévitique 19.12 Lévitique 21.8
7 Wasimwoe mwanamke aliye kahaba, au huyo aliye mwenye unajisi; wala wasimwoe mwanamke aliyeachwa na mumewe; kwa kuwa yeye kuhani ni mtakatifu kwa Mungu wake.
Lévitique 21.13-21.14 Ezéchiel 44.22 Lévitique 21.8 Deutéronome 24.1-24.4 Esaïe 50.1
8 Kwa hiyo basi utamtakasa; kwa kuwa yeye husongeza chakula cha Mungu wako; atakuwa mtakatifu kwako wewe; kwa kuwa mimi Bwana niwatakasaye ninyi ni mtakatifu.
Lévitique 21.6 Jean 17.19 Hébreux 7.26 Exode 29.43-29.44 Hébreux 10.29
9 Na binti ya kuhani ye yote atakapojitia unajisi kwa ukahaba, amemtia unajisi baba yake; atachomwa moto.
Genèse 38.24 1 Timothée 3.4-3.5 Lévitique 20.14 Josué 7.25 Tite 1.6
10 Na yeye aliye kuhani mkuu katika nduguze, ambaye mafuta ya kutiwa yamemiminwa kichwani mwake, naye akawekwa wakfu ili ayavae hayo mavazi, yeye hataziacha wazi nywele za kichwa chake, wala hatazirarua nguo zake;
Lévitique 16.32 Lévitique 10.6-10.7 Nombres 35.25 Exode 29.29-29.30 Matthieu 26.65
11 wala hataingia penye maiti, wala asijitie unajisi kwa ajili ya baba yake wala mama yake;
Nombres 19.14 Lévitique 19.28 Lévitique 21.1-21.2 Nombres 6.7 Matthieu 8.21-8.22
12 wala asitoke katika mahali patakatifu, wala asipatie unajisi mahali patakatifu pa Mungu wake; kwa kuwa utakaso wa hayo mafuta ya kutiwa ya Mungu wake u juu yake; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 10.7 Exode 29.6-29.7 Lévitique 8.30 Esaïe 61.1 Exode 28.36
13 Naye atamwoa mwanamke katika ubikira wake.
Lévitique 21.7 Ezéchiel 44.22 Apocalypse 14.4 2 Corinthiens 11.2
14 Asitwae mjane, wala mwanamke aliyeachwa na mumewe, wala mwanamke mwenye unajisi, wala kahaba; lakini atamwoa mwanamwali katika watu wake mwenyewe.
Lévitique 21.7 Ezéchiel 44.22
15 Naye asiwatie unajisi kizazi chake katika watu wake; kwa kuwa mimi ndimi Bwana nimtakasaye.
Malachie 2.11 1 Corinthiens 7.14 Esdras 9.2 Esdras 2.62 Malachie 2.15
16 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
17 Nena na Haruni, umwambie, Mtu awaye yote wa kizazi chako wewe katika vizazi vyao, aliye na kilema, asikaribie kusongeza chakula cha Mungu wake.
Lévitique 10.3 Nombres 16.5 Psaumes 65.4 1 Timothée 3.2 Lévitique 21.21
18 Kwa kuwa mtu awaye yote aliye na kilema hatakaribia; mtu kipofu, au kiwete, au mtu aliye na pua iliyoharibika, au aliye na kitu kilichozidi vimpasavyo mwili,
1 Timothée 3.2-3.3 Lévitique 22.19-22.25 1 Timothée 3.7 Matthieu 23.19 Tite 1.10
19 au mtu aliyevunjika mguu, au aliyevunjika mkono,
20 au aliye na kijongo, au aliye kibeti, au aliye na kilema cha jichoni, au aliye na upele, au mwenye buba, au aliyevunjika mapumbu;
Deutéronome 23.1 Esaïe 56.3
21 mtu awaye yote wa kizazi cha Haruni kuhani aliye na kilema asikaribie kuzisongeza sadaka za Bwana kwa njia ya moto; ana kilema huyo asikaribie kusongeza chakula cha Mungu wake.
Lévitique 21.6 Lévitique 21.17 Lévitique 21.8
22 Atakula chakula cha Mungu wake, katika hicho kilicho kitakatifu sana, na hicho kilicho kitakatifu.
Lévitique 2.10 Lévitique 7.1 Lévitique 2.3 Nombres 18.9-18.10 Lévitique 6.29
23 Lakini hataingia ndani ya pazia, wala asikaribie madhabahu, kwa sababu ana kilema; ili kwamba asipanajisi patakatifu pangu; kwa kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye.
Lévitique 21.12 Ezéchiel 44.9-44.14 Exode 30.6-30.8 Exode 40.26-40.27 Lévitique 15.31
24 Basi Musa akanena na Haruni na wanawe, na wana wa Israeli wote.
1 Timothée 1.18 Colossiens 4.17 Malachie 2.1-2.7 2 Timothée 2.2

Cette Bible est dans le domaine public.