Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Joël 3.12
Bible en Swahili de l’est


Annonce de la venue de l’Esprit

1 Kwa maana, angalieni, siku zile, na wakati ule, nitakapowarudisha mateka wa Yuda na Yerusalemu,
Jérémie 30.3 Jérémie 16.15 Jérémie 23.3-23.8 Ezéchiel 39.25 Psaumes 85.1
2 nitakusanya mataifa yote, nami nitawaleta chini katika bonde la Yehoshafau, na huko nitawahukumu kwa ajili ya watu wangu, na kwa ajili ya urithi wangu, Israeli, ambao wamewatawanya kati ya mataifa, na kuigawanya nchi yangu.
Esaïe 66.16 Sophonie 3.8 Zacharie 14.2-14.4 Ezéchiel 38.22 Ezéchiel 39.11
3 Nao wamewapigia kura watu wangu; na mtoto mwanamume wamemtoa ili kupata kahaba, na mtoto mwanamke wamemwuza ili kupata divai, wapate kunywa.
Nahum 3.10 Abdias 1.11 Amos 2.6 Apocalypse 18.13 2 Chroniques 28.8-28.9
4 Naam, na ninyi ni kitu gani kwangu, enyi Tiro, na Sidoni, na nchi zote za Filisti? Je! Mtanirudishia malipo? Au mtanitenda neno lo lote? Upesi na kwa haraka nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.
Esaïe 34.8 Esaïe 23.1-23.2 Amos 1.6-1.10 Esaïe 59.18 Jérémie 47.4
5 Kwa kuwa mmetwaa fedha yangu na dhahabu yangu, nanyi mmevichukua vitu vyangu vyema vipendezavyo, na kuviingiza katika hekalu zenu;
2 Chroniques 21.16-21.17 2 Rois 12.18 2 Rois 18.15-18.16 Jérémie 50.28 Jérémie 51.11
6 tena watoto wa Yuda na watoto wa Yerusalemu mmewauzia Wayunani, mpate kuwahamisha mbali na mipaka yao;
Ezéchiel 27.13 Joël 3.3 Joël 3.8 Deutéronome 28.68 Deutéronome 28.32
7 tazameni, nitawaamsha wapatoke mahali mlipowauza, nami nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.
Esaïe 43.5-43.6 Jérémie 23.8 2 Thessaloniciens 1.6 Joël 3.4 1 Samuel 15.33
8 Na mimi nitawauza wana wenu na binti zenu, na kuwatia katika mikono ya wana wa Yuda, nao watawauzia watu wa Sheba, taifa lililo mbali kabisa; kwa maana Bwana ndiye aliyesema neno hili.
Esaïe 60.14 Job 1.15 Juges 4.2 Esaïe 14.1-14.2 Ezéchiel 23.42
9 Tangazeni haya kati ya mataifa; takaseni vita; waamsheni mashujaa; watu wa vita na wakaribie; na wapande juu.
Jérémie 46.3-46.4 Ezéchiel 38.7 Esaïe 8.9-8.10 Jérémie 31.10 Ezéchiel 21.21-21.22
10 Yafueni majembe yenu yawe panga, na miundu yenu iwe mikuki; aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari.
Michée 4.3 Esaïe 2.4 Zacharie 12.8 Luc 22.36 2 Chroniques 25.8
11 Fanyeni haraka, mje, enyi mataifa yote, wa pande zote, jikusanyeni pamoja; na huko watelemshe mashujaa wako wote, Ee Bwana.
Esaïe 13.3 Sophonie 3.8 Esaïe 37.36 2 Thessaloniciens 1.7 Apocalypse 19.14
12 Mataifa na wajihimize, wakapande juu katika bonde la Yehoshafau; maana huko ndiko nitakakoketi niwahukumu mataifa yote yaliyo pande zote.
Joël 3.2 Psaumes 98.9 Psaumes 96.13 Esaïe 3.13 Esaïe 2.4
13 Haya! Utieni mundu, maana mavuno yameiva; njoni, kanyageni; kwa maana shinikizo limejaa, mapipa nayo yanafurika; kwani uovu wao ni mwingi sana.
Apocalypse 14.15-14.20 Esaïe 63.3 Osée 6.11 Marc 4.29 Jérémie 51.33
14 Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya Bwana i karibu, katika bonde la kukata maneno.
Esaïe 34.2-34.8 Joël 2.1 Joël 3.2 Philippiens 3.2 Joël 1.15
15 Jua na mwezi vimetiwa giza, na nyota zimeacha kuangaza.
Joël 2.10 Joël 2.31 Matthieu 24.29 Esaïe 13.10 Apocalypse 6.12-6.13
16 Naye Bwana atanguruma toka Sayuni, atatoa sauti yake toka Yerusalemu; na mbingu na nchi zitatetemeka; lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli.
Amos 1.2 Joël 2.10-2.11 Ezéchiel 38.19 Jérémie 25.30-25.31 Esaïe 33.16
17 Hivyo ndivyo mtakavyojua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, nikaaye Sayuni, mlima wangu mtakatifu; ndipo Yerusalemu utakapokuwa mtakatifu, wala wageni hawatapita tena ndani yake kamwe.
Joël 2.27 Esaïe 52.1 Nahum 1.15 Apocalypse 21.27 Esaïe 4.3
18 Tena itakuwa siku ile, ya kwamba milima itadondoza divai tamu, na vilima vitatiririka maziwa, na vijito vyote vya Yuda vitatoa maji tele; na chemchemi itatokea katika nyumba ya Bwana, na kulinywesha bonde la Shitimu.
Esaïe 30.25 Apocalypse 22.1-22.2 Esaïe 35.6 Ezéchiel 47.1-47.12 Nombres 25.1
19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya dhuluma waliowatenda wana wa Yuda; kwa sababu wamemwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.
Esaïe 19.1-19.15 Abdias 1.1 Malachie 1.3-1.4 Abdias 1.10-1.16 Ezéchiel 35.1-35.15
20 Bali Yuda atadumu milele, na Yerusalemu tangu kizazi hata kizazi.
Ezéchiel 37.25 Amos 9.15 Esaïe 33.20
21 Nami nitaitakasa damu yao ambayo sijaitakasa; kwa maana Bwana ndiye akaaye Sayuni.
Esaïe 4.4 Ezéchiel 36.25 Ezéchiel 36.29 Matthieu 27.25 Apocalypse 21.3

Cette Bible est dans le domaine public.