Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 8.11
Bible en Swahili de l’est


Punition : destruction et exil

1 Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya Bwana; kwa sababu wamelihalifu agano langu, wameiasi sheria yangu.
Osée 6.7 Deutéronome 28.49 Osée 5.8 Jérémie 4.13 Habakuk 1.8
2 Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua.
Matthieu 7.21 Tite 1.16 1 Jean 2.4 Luc 13.25 Psaumes 78.34-78.37
3 Israeli ameyatupa yaliyo mema; adui watamfuatia.
Deutéronome 28.25 Lamentations 3.66 Lévitique 26.36 Amos 1.11 Psaumes 36.3
4 Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nalikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyizia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.
Osée 2.8 Osée 13.2 2 Rois 15.10-15.30 1 Rois 12.16-12.20 Jérémie 44.7-44.8
5 Amemtupa ndama yako, Ee Samaria; hasira yangu imewaka juu yao; siku ngapi zitapita kabla ya hao kupata hali isiyo na hatia?
Osée 10.5 Jérémie 13.27 Deutéronome 32.22 Osée 8.6 Jérémie 4.14
6 Maana katika Israeli kimetokea hata na kitu hiki; fundi ndiye aliyekifanya, nacho si mungu kamwe; naam, ndama ya Samaria itavunjika vipande vipande.
Jérémie 50.2 Jérémie 43.12-43.13 Psaumes 106.19-106.20 Psaumes 135.15-135.18 Osée 10.5-10.6
7 Kwa maana wao hupanda upepo, nao watavuna tufani; nafaka haina bua; machipuko yake hayatoi masuke; hata ikiwa yatoa, wageni watayameza.
Proverbes 22.8 Galates 6.7 Osée 7.9 Job 4.8 Deutéronome 28.33
8 Israeli amemezwa; sasa wamo miongoni mwa mataifa kama chombo kisichopendeza.
Jérémie 22.28 Jérémie 51.34 Romains 9.22 Lamentations 2.2 Lévitique 26.33
9 Kwa maana wamekwea kwenda Ashuru, mfano wa punda wa mwituni aliye peke yake; Efraimu ameajiri wapenzi.
Jérémie 2.24 Osée 7.11 Osée 5.13 Ezéchiel 16.33-16.34 Esaïe 30.6
10 Naam, ijapokuwa waajiri kati ya mataifa, sasa nitawakusanya; nao wanaanza kupunguka kwa sababu ya mzigo wa mfalme wa wakuu.
Ezéchiel 16.37 Ezéchiel 26.7 Esaïe 10.8 Ezéchiel 23.46-23.47 Aggée 2.6
11 Kwa kuwa Efraimu ameongeza madhabahu kwa dhambi, madhabahu zimekuwa dhambi kwake.
Osée 12.11 Osée 10.8 Jérémie 16.13 Esaïe 10.10-10.11 Osée 10.1-10.2
12 Nijapomwandikia sheria yangu katika amri elfu kumi, zimehesabiwa kuwa ni kitu kigeni.
Osée 4.6 Esaïe 30.9 Psaumes 119.18 Néhémie 9.13-9.14 Psaumes 50.17
13 Kwa habari za dhabihu za matoleo yangu, hutoa dhabihu ya nyama na kuila; lakini Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao, na kuwapatiliza dhambi zao; watarudi kwenda Misri.
Osée 9.6 Osée 9.9 Deutéronome 28.68 Amos 5.22 Jérémie 14.10
14 Maana Israeli amemsahau Muumba wake, naye amejenga nyumba za enzi; na Yuda ameongeza miji yenye maboma; lakini nitapeleka moto juu ya miji yake, nao utaziteketeza ngome zake.
Deutéronome 32.18 Jérémie 17.27 Amos 2.5 Osée 13.6 Ephésiens 2.10

Cette Bible est dans le domaine public.