Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 8.10
Bible en Swahili de l’est


Punition : destruction et exil

1 Tia baragumu kinywani mwako. Kama tai, anakuja juu ya nyumba ya Bwana; kwa sababu wamelihalifu agano langu, wameiasi sheria yangu.
Osée 6.7 Deutéronome 28.49 Osée 5.8 Jérémie 4.13 Habakuk 1.8
2 Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua.
Matthieu 7.21 Tite 1.16 Osée 5.15 Matthieu 25.11 Michée 3.11
3 Israeli ameyatupa yaliyo mema; adui watamfuatia.
Amos 1.11 Psaumes 36.3 Lamentations 4.19 1 Timothée 5.12 Psaumes 81.10-81.11
4 Wamesimamisha wafalme, lakini si kwa shauri langu; wamejifanyia wakuu, lakini nalikuwa sina habari; kwa fedha yao na dhahabu yao wamejifanyizia sanamu, kusudi wakatiliwe mbali.
Osée 13.2 Osée 2.8 2 Rois 15.10-15.30 1 Rois 13.34 Galates 4.9
5 Amemtupa ndama yako, Ee Samaria; hasira yangu imewaka juu yao; siku ngapi zitapita kabla ya hao kupata hali isiyo na hatia?
Osée 10.5 Jérémie 13.27 2 Rois 17.21-17.23 2 Rois 17.16-17.18 Actes 7.41
6 Maana katika Israeli kimetokea hata na kitu hiki; fundi ndiye aliyekifanya, nacho si mungu kamwe; naam, ndama ya Samaria itavunjika vipande vipande.
Osée 10.5-10.6 Psaumes 115.4-115.8 2 Rois 23.19 Esaïe 44.9-44.20 2 Rois 23.15
7 Kwa maana wao hupanda upepo, nao watavuna tufani; nafaka haina bua; machipuko yake hayatoi masuke; hata ikiwa yatoa, wageni watayameza.
Proverbes 22.8 Osée 7.9 Job 4.8 Galates 6.7 2 Rois 13.3-13.7
8 Israeli amemezwa; sasa wamo miongoni mwa mataifa kama chombo kisichopendeza.
Jérémie 22.28 Jérémie 51.34 Lévitique 26.33 2 Rois 18.11 Jérémie 50.17
9 Kwa maana wamekwea kwenda Ashuru, mfano wa punda wa mwituni aliye peke yake; Efraimu ameajiri wapenzi.
Osée 7.11 Osée 5.13 Jérémie 2.24 Ezéchiel 16.33-16.34 Job 39.5-39.8
10 Naam, ijapokuwa waajiri kati ya mataifa, sasa nitawakusanya; nao wanaanza kupunguka kwa sababu ya mzigo wa mfalme wa wakuu.
Ezéchiel 16.37 Ezéchiel 26.7 Esaïe 10.8 Esaïe 36.13 Daniel 2.37
11 Kwa kuwa Efraimu ameongeza madhabahu kwa dhambi, madhabahu zimekuwa dhambi kwake.
Osée 12.11 Osée 10.1-10.2 Deutéronome 4.28 Osée 10.8 Jérémie 16.13
12 Nijapomwandikia sheria yangu katika amri elfu kumi, zimehesabiwa kuwa ni kitu kigeni.
Osée 4.6 Psaumes 50.17 2 Rois 17.15-17.16 Ezéchiel 20.11 Romains 7.12
13 Kwa habari za dhabihu za matoleo yangu, hutoa dhabihu ya nyama na kuila; lakini Bwana hawakubali; sasa ataukumbuka uovu wao, na kuwapatiliza dhambi zao; watarudi kwenda Misri.
Osée 9.6 Osée 9.9 Deutéronome 28.68 Osée 9.3-9.4 Osée 11.5
14 Maana Israeli amemsahau Muumba wake, naye amejenga nyumba za enzi; na Yuda ameongeza miji yenye maboma; lakini nitapeleka moto juu ya miji yake, nao utaziteketeza ngome zake.
Jérémie 17.27 Deutéronome 32.18 Amos 2.5 Osée 13.6 Amos 1.10

Cette Bible est dans le domaine public.