Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 14
Bible en Swahili de l’est


1 Ee Israeli, mrudie Bwana, Mungu wako; maana umeanguka kwa sababu ya uovu wako.
Osée 6.1 Osée 12.6 2 Chroniques 30.6-30.9 Osée 13.9 1 Samuel 7.3-7.4

Appel à revenir à Dieu et promesses

2 Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng’ombe.
Hébreux 13.15 Luc 18.13 Psaumes 69.30-69.31 Tite 2.14 Ephésiens 2.7-2.8
3 Ashuru hatatuokoa; hatutapanda farasi; wala hatutaiambia tena kazi ya mikono yetu, Ninyi ndinyi miungu yetu; maana kwako wewe wasio na baba hupata rehema.
Psaumes 10.14 Psaumes 68.5 Psaumes 33.17 Esaïe 30.16 Osée 2.17
4 Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha.
Ephésiens 2.4-2.9 Osée 6.1 Jérémie 3.22 Esaïe 57.18 Sophonie 3.17
5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli; naye atachanua maua kama nyinyoro, na kuieneza mizizi yake kama Lebanoni.
Esaïe 35.2 Matthieu 6.28 Esaïe 26.19 Proverbes 19.12 Deutéronome 32.2
6 Matawi yake yatatandaa, na uzuri wake utakuwa kama uzuri wa mzeituni, na harufu yake kama Lebanoni.
Psaumes 52.8 Psaumes 128.3 Cantique 4.11-4.15 Romains 11.16-11.24 Daniel 4.10-4.15
7 Na wao wakaao chini ya uvuli wake watarejea; watafufuka kama ngano, na kuchanua maua kama mzabibu; harufu yake itakuwa kama harufu ya divai ya Lebanoni.
Psaumes 91.1 Psaumes 85.6 Ezéchiel 17.23 Cantique 6.11 Jean 11.25
8 Efraimu atasema, Mimi nina nini tena na sanamu? Mimi nimeitika, nami nitamwangalia. Mimi ni kama mberoshi wenye majani mabichi. Kwangu mimi yamepatikana matunda yako.
Esaïe 41.19 Job 34.32 Esaïe 55.13 Jacques 1.17 1 Pierre 4.3-4.4
9 Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za Bwana zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.
Psaumes 107.43 Proverbes 10.29 Jérémie 9.12 Sophonie 3.5 Jean 8.47

Cette Bible est dans le domaine public.