Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 44.29
Bible en Swahili de l’est


Les serviteurs de Dieu

1 Kisha akanirudisha kwa njia ya lango lile la nje, la mahali patakatifu lililoelekea upande wa mashariki; nalo lilikuwa limefungwa.
Ezéchiel 43.1 Ezéchiel 42.14 Ezéchiel 40.6 Ezéchiel 40.17 2 Chroniques 20.5
2 Bwana akaniambia, Lango hili litafungwa, halitafunguliwa, wala mtu awaye yote hataingia kwa lango hili, kwa maana Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa hilo; basi kwa sababu hiyo litafungwa.
Ezéchiel 43.2-43.4 Exode 24.10 Esaïe 6.1-6.5
3 Na mkuu, yeye ndiye atakayeketi ndani yake ale chakula mbele za Bwana; ataingia kwa njia ya ukumbi wa lango, naye atatoka kwa njia iyo hiyo.
Ezéchiel 46.2 Ezéchiel 37.25 Genèse 31.54 Ezéchiel 34.24 Ezéchiel 40.9
4 Kisha akanileta, kwa njia ya lango la upande wa kaskazini, mbele ya nyumba; nikaangalia, na tazama, huo utukufu wa Bwana uliijaza nyumba ya Bwana; nikaanguka kifudifudi.
Ezéchiel 1.28 Ezéchiel 3.23 Ezéchiel 43.3-43.5 Ezéchiel 40.20 Aggée 2.7
5 Bwana akaniambia, Mwanadamu, weka moyoni mwako, ukatazame kwa macho yako, ukasikie kwa masikio yako, maneno yote nitakayokuambia, katika habari ya kawaida zote za nyumba ya Bwana, na ya amri zake zote; nawe weka moyoni mwako maingilio ya nyumba, pamoja na matokeo yote ya mahali patakatifu.
Ezéchiel 40.4 Ezéchiel 43.10-43.11 Deutéronome 12.32 Deutéronome 32.46 Proverbes 24.32
6 Nawe utawaambia waasi, yaani nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Enyi nyumba ya Israeli, katika machukizo yenu yote, na iwatoshe,
1 Pierre 4.3 Ezéchiel 45.9 Ezéchiel 3.9 Ezéchiel 2.5-2.8 Ezéchiel 3.26-3.27
7 kuwa mmewaingiza wageni, ambao mioyo yao haikutahiriwa, wala miili yao haikutahiriwa, wawe ndani ya patakatifu pangu, wapatie unajisi, naam, nyumba yangu, mtoapo sadaka ya chakula changu, mafuta na damu; nao wameyavunja maagano yangu, juu ya machukizo yenu yote.
Lévitique 22.25 Jérémie 9.26 Jérémie 4.4 Ezéchiel 44.9 Lévitique 26.41
8 Wala hamkuvilinda vitu vyangu vitakatifu bali mmejiwekea walinzi wa kawaida zangu, katika patakatifu pangu.
Nombres 18.7 1 Chroniques 23.32 Ezéchiel 40.45-40.46 Ezéchiel 44.14 Actes 7.53
9 Bwana MUNGU asema hivi; Hapana mgeni, ambaye moyo wake haukutahiriwa, wala mwili wake haukutahiriwa, atakayeingia patakatifu pangu, miongoni mwa wageni walio kati ya wana wa Israeli.
Joël 3.17 Zacharie 14.21 Ezéchiel 44.7 Psaumes 93.5 Marc 16.16
10 Lakini Walawi waliofarakana nami, hapo Waisraeli walipopotea, waliopotea na kuvifuata vinyago vyao, watachukua uovu wao wenyewe.
Ezéchiel 22.26 Ezéchiel 48.11 Ezéchiel 44.15 2 Rois 23.8-23.9 2 Chroniques 29.4-29.5
11 Hata hivyo watakuwa wahudumu katika patakatifu pangu, wakiwa wasimamizi wa malango ya nyumba, wakihudumu humo nyumbani; watawachinjia watu sadaka za kuteketezwa na dhabihu, nao watasimama mbele yao ili kuwahudumia.
Nombres 16.9 2 Chroniques 29.34 1 Chroniques 26.1-26.19 Ezéchiel 40.45 Nombres 18.6
12 Kwa sababu waliwahudumia mbele ya vinyago vyao, wakawa kwazo la uovu kwa nyumba ya Israeli; basi nimeuinua mkono wangu juu yao, asema Bwana MUNGU, nao watachukua uovu wao.
Psaumes 106.26 Ezéchiel 14.3-14.4 2 Rois 16.10-16.16 Ezéchiel 44.10 Ezéchiel 20.23
13 Wala hawatanikaribia, kunihudumia katika kazi ya ukuhani, wala hawatakaribia vitu vyangu vitakatifu kimojawapo, vitu vilivyo vitakatifu sana; bali watachukua aibu yao, na machukizo yao yote waliyoyatenda.
Nombres 18.3 2 Rois 23.9 Ezéchiel 36.7 Ezéchiel 32.20 Ezéchiel 16.61
14 Lakini nitawafanya kuwa walinzi katika ulinzi wa nyumba, kwa huduma yake yote, na kwa yote yatakayotendeka ndani yake.
1 Chroniques 23.28-23.32 Nombres 18.4
15 Lakini makuhani Walawi, wana wa Sadoki, waliolinda ulinzi wa patakatifu pangu, hapo wana wa Israeli walipopotea na kuniacha, hao ndio watakaonikaribia ili kunihudumia; nao watasimama mbele zangu, kunitolea mafuta na damu, asema Bwana MUNGU;
Ezéchiel 43.19 Ezéchiel 44.7 Ezéchiel 40.46 Ezéchiel 48.11 Deutéronome 10.8
16 wataingia patakatifu pangu, nao wataikaribia meza yangu, ili kunihudumia, nao watalinda ulinzi wangu.
Ezéchiel 41.22 Malachie 1.7 Nombres 18.7-18.8 Malachie 1.12 Apocalypse 1.6
17 Itakuwa, hapo watakapoingia kwa malango ya ua wa ndani, watavikwa mavazi ya kitani; wala sufu haitakuwa juu yao, maadamu wanahudumu katika malango ya ua wa ndani, na ndani ya nyumba.
Apocalypse 19.8 Exode 39.27-39.29 Exode 28.43 Apocalypse 4.4 Lévitique 16.4
18 Watakuwa na vilemba vya kitani juu ya vichwa vyao, nao watakuwa na suruali za kitani viunoni mwao; hawatajifunga kiunoni kitu cho chote kifanyacho jasho.
Lévitique 16.4 1 Corinthiens 11.4-11.10 Esaïe 3.20 Exode 28.40-28.43 Exode 39.28
19 Nao watakapotoka kuingia ua wa nje, yaani, ua wa nje wa watu, ndipo watakapoyavua mavazi yao waliyovaa katika huduma yao, na kuyaweka katika vile vyumba vitakatifu, nao watavaa mavazi mengine, wasije wakawatakasa watu kwa mavazi yao.
Lévitique 6.27 Ezéchiel 46.20 Lévitique 6.10-6.11 Exode 29.37 Exode 30.29
20 Hawatanyoa vichwa vyao, wala hawataacha nywele zao kuwa ndefu sana; watazipunguza nywele za vichwa vyao tu.
Nombres 6.5 Lévitique 21.5-21.24 1 Corinthiens 11.14 Deutéronome 14.1
21 Wala kuhani awaye yote hatakunywa mvinyo, aingiapo katika ua wa ndani.
Lévitique 10.9 1 Timothée 5.23 1 Timothée 3.8 Luc 1.15 Tite 1.7-1.8
22 Wala hawataoa wanawake wajane, wala mwanamke aliyeachwa na mume wake; lakini watatwaa mabikira wa wazao wa nyumba ya Israeli, au mjane aliyefiwa na mumewe kuhani.
Lévitique 21.7 Lévitique 21.13-21.14 1 Timothée 3.2 Deutéronome 24.1-24.4 1 Timothée 3.11-3.12
23 Nao watawafundisha watu wangu tofauti iliyopo kati ya vitu vitakatifu na vitu vya sikuzote, na kuwafundisha kupambanua kati ya yaliyo machafu na yaliyo safi.
Ezéchiel 22.26 Osée 4.6 Lévitique 10.10-10.11 Tite 1.9-1.11 2 Timothée 2.24-2.25
24 Na katika mashindano watasimama ili kuamua; wataamua sawasawa na hukumu zangu; nao watazishika sheria zangu, na amri zangu, katika sikukuu zangu zote zilizoamriwa; nao watazitakasa sabato zangu.
1 Chroniques 23.4 Ezéchiel 22.26 2 Chroniques 19.8-19.10 Deutéronome 17.8-17.13 Nombres 28.1-28.29
25 Wala hawatakaribia maiti na kujitia unajisi; ila kwa ajili ya baba, au mama, au mwana, au binti, au ndugu mwanamume, au ndugu mwanamke asiyeolewa bado, waweza kujitia unajisi.
2 Corinthiens 5.16 Lévitique 21.1-21.6 Matthieu 8.21-8.22 1 Thessaloniciens 4.13-4.15 Luc 9.59-9.60
26 Naye akiisha kutakaswa watamhesabia siku saba.
Nombres 6.10-6.21 Hébreux 9.13-9.14 Nombres 19.11-19.14
27 Na katika siku atakayoingia ndani ya patakatifu, katika ua wa ndani, ili kuhudumu ndani ya patakatifu, atatoa sadaka yake ya dhambi, asema Bwana MUNGU.
Nombres 6.9-6.11 Lévitique 8.14-8.36 Lévitique 4.3-4.35 Hébreux 7.26-7.28 Ezéchiel 44.17
28 Nao watakuwa na urithi; mimi ni urithi wao; wala hamtawapa milki iwayo yote katika Israeli; mimi ni milki yao.
Nombres 18.20 Deutéronome 10.9 Deutéronome 18.1-18.2 Josué 13.33 Ezéchiel 45.4
29 Wataila sadaka ya unga, na sadaka ya dhambi, na sadaka ya hatia, na kila kitu katika Israeli kilichowekwa wakfu kitakuwa chao.
Nombres 18.14 Lévitique 27.21 Lévitique 27.28 Lévitique 6.14-6.18 Lévitique 6.29
30 Na kitu cha kwanza cha malimbuko yote ya vitu vyote, na kila toleo la kila kitu cha matoleo yenu, litakuwa la makuhani. Tena mtampa kuhani sehemu ya kwanza ya unga mbichi, ili kukalisha baraka juu ya nyumba yako.
Néhémie 10.35-10.37 Nombres 15.19-15.21 2 Chroniques 31.4-31.6 Exode 23.19 2 Chroniques 31.10
31 Makuhani hawatakula nyamafu, au iliyoraruliwa, ikiwa ya ndege au ya mnyama.
Lévitique 22.8 Exode 22.31 Deutéronome 14.21 Lévitique 17.15 Romains 14.20

Cette Bible est dans le domaine public.