Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 39.15
Bible en Swahili de l’est


Jugement de Gog

1 Na wewe, mwanadamu, tabiri juu ya Gogu, useme, Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali;
Ezéchiel 38.2-38.3 Nahum 2.13 Nahum 3.5 Ezéchiel 35.3
2 nami nitakugeuza na kukuongoza, nami nitakupandisha toka pande za mwisho za kaskazini; nami nitakuleta juu ya milima ya Israeli;
Ezéchiel 38.15 Psaumes 68.2 Daniel 11.40 Psaumes 40.14 Esaïe 37.29
3 nami nitaupiga upinde wako, utoke katika mkono wako wa kushoto, na mishale yako nitaiangusha, itoke katika mkono wako wa kulia.
Psaumes 76.3 Osée 1.5 Jérémie 21.4-21.5 Psaumes 46.9 Ezéchiel 20.21-20.24
4 Utaanguka juu ya milima ya Israeli, wewe, na vikosi vyako vyote, na watu wa kabila nyingi walio pamoja nawe; nami nitakutoa na kuwapa ndege wa kila namna walao nyama, na wanyama wa nchi, uliwe na wao.
Ezéchiel 33.27 Ezéchiel 39.17-39.20 Ezéchiel 38.21 Ezéchiel 32.4-32.5 Jérémie 15.3
5 Utaanguka katika uwanda; kwa maana mimi nimenena neno hili, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 8.2 Ezéchiel 29.5 Jérémie 22.19 Ezéchiel 32.4
6 Nami nitapeleka moto juu ya Magogu; na juu ya watu wote wakaao salama katika visiwa; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 30.8 Amos 1.4 Ezéchiel 30.16 Jérémie 25.22 Psaumes 72.10
7 Na jina langu takatifu nitalifanya kuwa limejulika kati ya watu wangu Israeli; wala sitaliacha jina langu takatifu kutiwa unajisi tena; nao mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, na Aliye Mtakatifu katika Israeli.
Ezéchiel 38.16 Ezéchiel 38.23 Exode 20.7 Ezéchiel 20.39 Esaïe 12.6
8 Tazama, linakuja, nalo litatendeka, asema Bwana MUNGU; hii ndiyo siku ile niliyoinena.
Ezéchiel 38.17 Apocalypse 21.6 2 Pierre 3.8 Apocalypse 16.17 Ezéchiel 7.2-7.10
9 Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka, nao watafanya mioto kwa silaha za vita na kuziteketeza, ngao, na vigao, na pinde, na mishale, na mafumo, na mikuki, nao watazitumia kama kuni kwa muda wa miaka saba;
Psaumes 46.9 Esaïe 66.24 Josué 11.6 Malachie 1.5 Psaumes 111.2-111.3
10 hata hawataokota kuni mashambani, wala hawatakata kuni msituni; maana watafanya mioto kwa silaha zile; nao watawateka nyara watu waliowateka wao, na kunyang’anya vitu vya watu walionyang’anya vitu vyao, asema Bwana MUNGU.
Esaïe 33.1 Esaïe 14.2 Michée 5.8 Exode 3.22 Habakuk 3.8
11 Tena, itakuwa katika siku hiyo, nitampa Gogu pa kuzikia katika Israeli, bonde la wapitao, upande wa mashariki wa bahari; nalo litawazuia wapitao; na huko watamzika Gogu na watu wake jamii yote; nao wataliita, Bonde la Hamon-Gogu.
Nombres 34.11 Ezéchiel 38.2 Jean 6.1 Luc 5.1 Ezéchiel 47.18
12 Na kwa muda wa miezi saba nyumba ya Israeli watakuwa wakiwazika, wapate kuisafisha nchi.
Deutéronome 21.23 Ezéchiel 39.14 Ezéchiel 39.16 Nombres 19.16
13 Naam, watu wote wa nchi hiyo watawazika; itakuwa ni sifa kwao katika siku ile nitakapotukuzwa, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 28.22 Sophonie 3.19-3.20 Jérémie 33.9 Deutéronome 26.19 Psaumes 149.6-149.9
14 Nao watawachagua watu wa kufanya kazi ya daima, watakaopita kati ya nchi, ili kuwazika waliosalia juu ya uso wa nchi, ili kuisafisha; miezi saba itakapokwisha kupita watatafuta.
Nombres 19.11-19.19 Ezéchiel 39.12
15 Na hao wapitao kati ya nchi watatafuta; na mtu ye yote aonapo mfupa wa mtu, ndipo atakapoweka alama karibu nao, hata wazishi watakapouzika katika bonde la Hamon- Gogu.
Luc 11.44
16 Tena, Hamona litakuwa jina la mji. Hivyo ndivyo watakavyosafisha nchi.
17 Na wewe, mwanadamu, Bwana MUNGU asema hivi; Sema na ndege wa kila namna, na kila mnyama wa kondeni, Jikusanyeni, mje; jikusanyeni pande zote mwijilie sadaka yangu niifanyayo kwa ajili yenu, naam, sadaka kubwa juu ya milima ya Israeli, mpate kula nyama na kunywa damu.
Sophonie 1.7 Ezéchiel 39.4 Jérémie 12.9 Esaïe 34.6 Apocalypse 19.17-19.18
18 Mtakula nyama yao walio hodari, na kunywa damu ya wakuu wa dunia, ya kondoo waume na ya wana-kondoo, na ya mbuzi, na ya ng’ombe, wote na wanono wa Bashani.
Psaumes 22.12 Jérémie 51.40 Jérémie 50.27 Amos 4.1 Ezéchiel 29.5
19 Nanyi mtakula mafuta na kushiba, mtakunywa damu na kulewa, na sadaka yangu niliyoifanya kwa ajili yenu.
20 Nanyi mtashibishwa mezani pangu kwa farasi, na magari ya vita, na mashujaa, na watu wote wa vita, asema Bwana MUNGU.
Apocalypse 19.18 Ezéchiel 38.4 Psaumes 76.5-76.6 Aggée 2.22
21 Nami nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa wote wataiona hukumu yangu niliyoitekeleza, na mkono wangu niliouweka juu yao.
Ezéchiel 38.16 Ezéchiel 38.23 Esaïe 37.20 Ezéchiel 36.23 Exode 9.16
22 Basi, nyumba ya Israeli watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wao, tangu siku hiyo na baadaye.
Ezéchiel 39.28 Jérémie 24.7 Psaumes 9.16 Jérémie 31.34 Ezéchiel 39.7
23 Nao mataifa watajua ya kuwa nyumba ya Israeli walihamishwa, na kwenda kifungoni, kwa sababu ya uovu wao; kwa sababu waliniasi, nami nikawaficha uso wangu; basi nikawatia katika mikono ya adui zao, nao wakaanguka kwa upanga, wote pia.
Esaïe 59.2 Esaïe 1.15 Jérémie 22.8-22.9 Lévitique 26.25 Ezéchiel 39.29
24 Kwa kadiri ya uchafu wao, kwa kadiri ya makosa yao, ndivyo nilivyowatenda, nami nikawaficha uso wangu.
Jérémie 4.18 Jérémie 2.19 Ezéchiel 36.19 Jérémie 2.17 Daniel 9.5-9.10
25 Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU asema hivi, Sasa nitawarejeza watu wa Yakobo waliohamishwa, nitawahurumia nyumba yote ya Israeli; nami nitalionea wivu jina langu takatifu.
Esaïe 27.12-27.13 Ezéchiel 34.13 Jérémie 31.1 Ezéchiel 37.21-37.22 Osée 1.11
26 Nao watachukua aibu yao, na makosa yao yote waliyoniasi, watakapokaa salama katika nchi yao wenyewe, wala hapana mtu atakayewatia hofu;
1 Rois 4.25 Michée 4.4 Ezéchiel 16.63 Ezéchiel 34.27-34.28 Ezéchiel 32.25
27 nitakapokuwa nimewaleta tena kutoka kabila za watu, na kuwakusanya kwa kuwatoa katika nchi za adui zao, na kutakaswa kati yao mbele ya macho ya mataifa mengi.
Ezéchiel 38.16 Ezéchiel 36.23-36.24 Ezéchiel 38.23 Ezéchiel 39.25 Ezéchiel 39.13
28 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wao, kwa kuwa naliwahamisha, waende utumwani kati ya mataifa, na mimi nikawakusanya, na kuwaingiza katika nchi yao wenyewe; wala sitawaacha tena huko kamwe, hata mmojawapo;
Ezéchiel 39.22 Romains 11.1-11.7 Amos 9.9 Néhémie 1.8-1.10 Ezéchiel 34.30
29 wala sitawaficha uso wangu tena; kwa maana nimemwaga roho yangu juu ya nyumba ya sraeli, asema Bwana MUNGU.
Joël 2.28 Esaïe 32.15 Esaïe 45.17 1 Jean 3.24 Ezéchiel 36.25-36.27

Cette Bible est dans le domaine public.