Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 27.15
Bible en Swahili de l’est


1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Na wewe, mwanadamu, mfanyie Tiro maombolezo;
Jérémie 9.10 Jérémie 9.17-9.20 Ezéchiel 28.12 Ezéchiel 19.1 Amos 5.1
3 umwambie Tiro, Ewe ukaaye penye maingilio ya bahari, uliye mchuuzi wa watu wa kabila nyingi, mpaka visiwa vingi, Bwana MUNGU asema hivi; Wewe, Tiro, umesema, Mimi ni ukamilifu wa uzuri.
Ezéchiel 27.4 Esaïe 23.2-23.3 Psaumes 50.2 Ezéchiel 28.2-28.3 Esaïe 23.11
4 Mipaka yako i kati ya moyo wa bahari; wajenzi wako wameukamilisha uzuri wako.
Ezéchiel 26.5
5 Mbao zako zote wamezifanya kwa misunobari itokayo Seniri; wametwaa mierezi ya Lebanoni ili kukufanyia mlingoti;
Deutéronome 3.9 Cantique 4.8 Psaumes 29.5 Psaumes 104.16 Psaumes 92.12
6 kwa mialoni ya Bashani wamefanya makasia yako; na sitaha zako wamezifanya kwa pembe iliyotiwa kazi ya njumu katika mti wa mihugu itokayo Kitimu.
Genèse 10.4 Esaïe 2.13 Zacharie 11.2 Jérémie 2.10 Jérémie 22.20
7 Tanga lako lilikuwa la kitani safi itokayo Misri, iliyotiwa taraza, ili iwe bendera kwako; na chandalua chako kilikuwa cha rangi ya samawi na urujuani toka visiwa vya Elisha.
Jérémie 10.9 Exode 25.4 Genèse 10.4 1 Rois 10.28 1 Chroniques 1.7
8 Wakaao Sidoni na Arvadi ndio waliovuta makasia yako; wana wako wenye akili, Ee Tiro, walikuwa ndani yako, ndio waliokuwa rubani zako.
Genèse 10.18 1 Rois 9.27 Ezéchiel 27.11 Ezéchiel 27.28 Josué 11.8
9 Wazee wa Gebali na wenye akili wake walikuwa ndani yako, wenye kutia kalafati; merikebu zote za bahari na mabaharia wao walikuwa ndani yako, ili kubadiliana biashara yako.
1 Rois 5.18 Josué 13.5 Psaumes 83.7
10 Watu wa Uajemi na Ludi na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita; walitungika ngao na chapeo ndani yako; wakadhihirisha uzuri wako.
Ezéchiel 38.5 Ezéchiel 30.5 Jérémie 46.9 Cantique 4.4 Esaïe 66.19
11 Watu wa Arvadi, pamoja na jeshi lako, walikuwa juu ya kuta zako pande zote, na Wagamadi walikuwa ndani ya minara yako; walitungika ngao zao juu ya kuta zako pande zote; wakaukamilisha uzuri wako.
Ezéchiel 27.3-27.4
12 Tarshishi alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa utajiri wa kila aina; kwa fedha, na chuma, na bati, na risasi, walifanya biashara, wapate vitu vyako vilivyouzwa.
Esaïe 23.10 1 Rois 10.22 Ezéchiel 38.13 Genèse 10.4 Esaïe 23.14
13 Uyunani na Tubali na Mesheki ndio waliokuwa wachuuzi wako; walitoa wanadamu, na vyombo vya shaba, kwa biashara yako.
Genèse 10.2 Esaïe 66.19 Ezéchiel 39.1 Apocalypse 18.13 1 Chroniques 1.5
14 Watu wa nyumba ya Togarma walifanya biashara, kwa farasi, naam, farasi za vita, na nyumbu, wapate vitu vyako vilivyouzwa.
Ezéchiel 38.6 Genèse 10.3 1 Chroniques 1.6
15 Wadedani walikuwa wachuuzi wako, visiwa vingi vilikuwa soko la mkono wako; walikuletea pembe, na mpingo, ili kuvibadili.
Genèse 10.7 1 Rois 10.22 Apocalypse 18.12 Ezéchiel 27.20 Jérémie 25.23
16 Shamu alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa kazi za mkono wako walifanya biashara kwa zumaridi, na urujuani, na kazi ya taraza, na kitani safi, na marijani, na akiki, wapate vitu vyako vilivyouzwa.
Juges 10.6 Ezéchiel 28.13 2 Samuel 15.8 2 Samuel 8.5 2 Samuel 10.6
17 Yuda, na nchi ya Israeli, walikuwa wachuuzi wako; walitoa badala ya bidhaa yako ngano ya Minithi, na mtama, na asali, na mafuta, na zeri.
Juges 11.33 1 Rois 5.9 Esdras 3.7 Actes 12.20 Genèse 43.11
18 Dameski alikuwa mfanya biashara kwako, kwa habari ya wingi wa kazi za mkono wako, kwa ajili ya wingi wa aina zote za utajiri; akaleta divai ya Helboni, na sufu nyeupe.
Esaïe 7.8 Genèse 15.2 1 Rois 11.24-11.25 Actes 9.2 Ezéchiel 47.16-47.18
19 Wedani, na Yavani, walifanya biashara toka Uzali kwa vitu vyako; chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai, vilikuwa katika bidhaa yako.
Exode 30.23-30.24 Juges 18.29 Cantique 4.13-4.14 Psaumes 45.8
20 Dedani alikuwa mchuuzi wako, kwa nguo za thamani za kutandikia farasi.
Genèse 25.3 Ezéchiel 27.15
21 Arabuni, na wakuu wote wa Kedari, ndio waliokuwa wafanya biashara wa mkono wako; kwa wana-kondoo, na kondoo waume, na mbuzi; kwa hao walifanya biashara nawe.
Esaïe 60.7 Genèse 25.13 2 Chroniques 17.11 Actes 2.11 Esaïe 21.16
22 Wachuuzi wa Sheba, na Raama, ndio waliokuwa wachuuzi wako; badala ya vitu vyako walitoa manukato yaliyo mazuri, na kila aina ya vito vya thamani, na dhahabu.
Genèse 10.7 Esaïe 60.6 1 Chroniques 1.9 1 Rois 10.1-10.13 Psaumes 72.10
23 Harani, na Kane, na Adini, wachuuzi wa Sheba, na Ashuru, na Kilmadi, walikuwa wachuuzi wako.
2 Rois 19.12 Esaïe 37.12 Amos 1.5 Genèse 10.22 Esaïe 7.18
24 Hao ndio waliokuwa wachuuzi wako, kwa vitu vya tunu, kwa vitumba vya nguo za samawi na kazi ya taraza, na masanduku ya mavazi ya thamani, yaliyofungwa kwa kamba, na kufanyizwa kwa mti wa mierezi, katika bidhaa yako.
2 Rois 2.8
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara yako, kwa bidhaa yako; nawe ulijazwa sana, ukawa mtukufu sana, katika moyo wa bahari.
Esaïe 2.16 Esaïe 23.14 Psaumes 48.7 1 Rois 10.22 Esaïe 60.9
26 Wavuta makasia wako walikuleta katika maji makuu; upepo wa mashariki umekuvunja moyoni mwa bahari.
Psaumes 48.7 Jérémie 18.17 Actes 27.14 Ezéchiel 26.19 Ezéchiel 27.34
27 Mali zako, na bidhaa yako, na utajiri wako, wana-maji wako, na rubani zako, na wenye kutia kalafati wako, na wafanya biashara wako, na watu wako wa vita wote, walio ndani yako, pamoja na jeshi lako lote lililo ndani yako, wataanguka katika moyo wa bahari katika siku ya kuangamia kwako.
Proverbes 11.4 Ezéchiel 26.21 Ezéchiel 27.7-27.9 Ezéchiel 27.22 Ezéchiel 27.34
28 Kwa sauti ya vilio vya rubani zako viunga vyako vitatetema.
Ezéchiel 26.10 Exode 15.14 Nahum 2.3 Ezéchiel 27.35 Ezéchiel 26.15-26.18
29 Na wote wavutao kasia, wana-maji, na rubani zote wa baharini, watashuka katika merikebu zao, na kusimama katika nchi kavu;
Apocalypse 18.17-18.24 Ezéchiel 32.10 Ezéchiel 26.16
30 nao watasikizisha watu sauti zao juu yako, nao watalia kwa uchungu, na kutupa mavumbi juu ya vichwa vyao, na kugaagaa katika majivu;
Jérémie 6.26 2 Samuel 1.2 Lamentations 2.10 1 Samuel 4.12 Esaïe 23.1-23.6
31 nao watajifanya kuwa na upaa kwa ajili yako, na kujifunga nguo za magunia viunoni, nao watakulilia kwa uchungu wa roho, kwa maombolezo ya uchungu.
Esaïe 22.12 Esaïe 16.9 Ezéchiel 7.18 Esaïe 22.4 Esaïe 15.2
32 Na katika kulia kwao watakufanyia maombolezo, na kukuombolezea, wakisema, Ni nani aliye kama Tiro, kama yeye aliyenyamazishwa kati ya bahari?
Ezéchiel 26.17 Apocalypse 18.18 Ezéchiel 27.2 Lamentations 2.13 Lamentations 1.12
33 Bidhaa zako zilipotoka katika bahari, uliwajaza watu wa kabila nyingi; uliwatajirisha wafalme wa dunia, kwa wingi wa mali zako, na kwa utajiri wako.
Apocalypse 18.19 Apocalypse 18.12-18.15 Ezéchiel 28.4-28.5 Ezéchiel 27.3 Ezéchiel 27.12-27.36
34 Wakati ulipovunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na jeshi lako lote walianguka kati yako.
Ezéchiel 27.26-27.27 Zacharie 9.3-9.4 Ezéchiel 26.19-26.21 Ezéchiel 26.12-26.15
35 Wote wakaao katika visiwa vile watakustaajabia, na wafalme wao wameogopa sana, wamefadhaika nyuso zao.
Esaïe 23.6 Ezéchiel 32.10 Ezéchiel 26.15-26.18 Apocalypse 18.9-18.10 Ezéchiel 28.17-28.19
36 Wafanya biashara kati ya kabila za watu wakuzomea; umekuwa kitu cha kutisha, wala hutakuwapo tena milele.
Jérémie 18.16 Jérémie 19.8 Psaumes 37.36 Psaumes 37.10 Sophonie 2.15

Cette Bible est dans le domaine public.