Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 23.9
Bible en Swahili de l’est


Deux sœurs prostituées

1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Mwanadamu, palikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja;
Jérémie 3.7-3.10 Ezéchiel 16.44-16.46
3 nao walizini huko Misri; walizini wakati wa ujana wao; huko vifua vyao vililemewa, na huko waliyabana matiti ya ubikira wao.
Lévitique 17.7 Ezéchiel 16.22 Josué 24.14 Ezéchiel 20.8 Ezéchiel 23.8
4 Na majina yao, mkubwa aliitwa Ohola, na umbu lake Oholiba; wakawa wangu, wakazaa wana na binti. Na katika hayo majina yao, Samaria ni Ohola, na Yerusalemu ni Oholiba.
Ezéchiel 16.8 Exode 19.5-19.6 Romains 7.4 Psaumes 132.13-132.14 Ezéchiel 16.40
5 Na Ohola alifanya mambo ya kikahaba alipokuwa wangu; naye alipenda mno wapenzi wake, Waashuri, jirani zake,
2 Rois 17.3 Osée 5.13 2 Rois 15.19 2 Rois 16.7 Osée 8.9-8.10
6 waliovikwa samawi, maliwali na mawaziri, wote vijana wa kutamanika, wapanda farasi wakipanda farasi zao.
Ezéchiel 23.23
7 Akawagawia mambo yake ya kikahaba, watu wateule wa Ashuru, wote pia; akajitia unajisi kwa vinyago vyote vya kila mmoja wa hao aliowapenda.
Osée 6.10 Osée 5.3 Ezéchiel 22.3-22.4 Ezéchiel 20.7 Ezéchiel 23.30
8 Wala hakuyaacha mambo yake ya kikahaba tangu siku za Misri, kwa maana wakati wa ujana wake walilala naye, wakayabana matiti ya ubikira wake wakamwaga uzinzi wao juu yake.
Exode 32.4 Ezéchiel 23.3 Ezéchiel 23.19 2 Rois 10.29 2 Rois 17.16
9 Kwa sababu hiyo nalimtia katika mikono ya wapenzi wake, katika mikono ya Waashuri, aliowapendelea.
Osée 11.5 2 Rois 15.29 2 Rois 17.23 2 Rois 17.3-17.6 2 Rois 18.9-18.12
10 Na hawa wakaufunua uchi wake, wakatwaa wanawe na binti zake, wakamwua yeye kwa upanga; akawa jina la aibu kati ya wanawake; kwa maana walitoa hukumu juu yake.
Osée 2.10 Ezéchiel 23.29 Osée 2.3 Jérémie 22.8-22.9 Ezéchiel 16.37-16.41
11 Na umbu lake, Oholiba, akayaona hayo walakini alizidi kuharibika kuliko yeye, kwa kupendelea kwake, na kwa uzinzi wake, uliokuwa mwingi kuliko uzinzi wa umbu lake.
Jérémie 3.8-3.11 Ezéchiel 16.47-16.51 Ezéchiel 23.4
12 Aliwapendelea Waashuri, maliwali na mawaziri, jirani zake, waliovikwa nguo za shani, wapanda farasi wakipanda farasi zao, wote pia vijana wa kutamanika.
2 Rois 16.7-16.15 2 Chroniques 28.16-28.23 Ezéchiel 23.5-23.6 Ezéchiel 16.28 Ezéchiel 23.23
13 Nikaona ya kuwa ametiwa unajisi; wote wawili walifuata njia moja.
Osée 12.1-12.2 2 Rois 17.18-17.19 Ezéchiel 23.31
14 Naye akaongeza uzinzi wake; kwa maana aliona watu waume, ambao sura zao zimeandikwa ukutani, sura za Wakaldayo zilizoandikwa kwa rangi nyekundu;
Ezéchiel 8.10 Jérémie 22.14 Ezéchiel 16.29 Jérémie 50.2 Esaïe 46.1
15 waliofungiwa mikumbuu viunoni mwao, na vilemba vilivyotiwa rangi vichwani mwao; wote wakuu wa kuangaliwa, kwa mfano wa wana wa Babeli katika Ukaldayo, katika nchi ya kuzaliwa kwao.
Esaïe 22.21 2 Samuel 14.25 1 Samuel 18.4 Juges 8.18
16 Na mara alipowaona aliwapendelea, akatuma wajumbe kwao hata Ukaldayo.
Ezéchiel 16.29 Matthieu 5.28 Ezéchiel 23.40-23.41 Job 31.1 Proverbes 23.33
17 Na watu wa Babeli wakamwendea katika kitanda cha mapenzi, wakamtia unajisi kwa uzinzi wao, akatiwa unajisi nao, kisha roho yake ikafarakana nao.
Ezéchiel 23.22 Ezéchiel 23.28 2 Samuel 13.15 Ezéchiel 16.37 Genèse 11.9
18 Basi alifunua uzinzi wake, na kufunua uchi wake; ndipo roho yangu ikafarakana naye, kama ilivyofarakana na umbu lake.
Jérémie 12.8 Psaumes 106.40 Psaumes 78.59 Ezéchiel 21.24 Jérémie 8.12
19 Lakini aliongeza uzinzi wake, akikumbuka siku za ujana wake, alipofanya mambo ya kikahaba katika nchi ya Misri.
Ezéchiel 23.3 Ezéchiel 20.7 Ezéchiel 23.8 Amos 4.4 Ezéchiel 16.29
20 Akawapendelea wapenzi wao, ambao nyama ya mwili wao ni kama nyama ya mwili wa punda, nacho kiwatokacho ni kama kiwatokacho farasi.
Ezéchiel 17.15 Ezéchiel 16.26 Ezéchiel 16.20 Jérémie 5.8
21 Ndivyo ulivyokumbuka uasherati wa ujana wako, yalipobanwa matiti yako na Wamisri, kwa maziwa ya ujana wako.
22 Kwa sababu hiyo, Ewe Oholiba, Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, nitawainua wapenzi wako juu yako, ambao roho yako imefarakana nao, nami nitawaleta juu yako pande zote;
Ezéchiel 16.37 Habakuk 1.6-1.10 Ezéchiel 23.28 Jérémie 6.22-6.23 Esaïe 10.5-10.6
23 watu wa Babeli, na Wakaldayo wote, Pekodi na Shoa na Koa, na Waashuri wote pamoja nao; vijana wa kutamanika, wote pia, maliwali na mawaziri, wakuu, na watu wenye sifa, wote wenye kupanda farasi.
Jérémie 50.21 2 Rois 20.14-20.17 2 Rois 24.2 Esdras 6.22 Genèse 2.14
24 Nao watakuja kwako na silaha zao, na magari ya vita, na magurudumu, na wingi wa mataifa; watajipanga juu yako kwa ngao, na vigao, na chapeo za shaba, pande zote; nami nitawapa uwezo wa kuhukumu, nao watakuhukumu sawasawa na hukumu zao.
Ezéchiel 23.45 Ezéchiel 26.10 Jérémie 47.3 Nahum 2.3-2.4 Ezéchiel 16.38
25 Nami nitaweka wivu wangu juu yako, nao watakutenda mambo kwa ghadhabu; watakuondolea pua yako na masikio yako; na mabaki yako wataanguka kwa, upanga; watawatwaa wanao na binti zako; na mabaki yako watateketea motoni.
Ezéchiel 23.47 Ezéchiel 8.1-8.18 Sophonie 1.18 Ezéchiel 5.13 Ezéchiel 20.47-20.48
26 Pia watakuvua nguo zako, na kukuondolea vyombo vyako vya uzuri.
Ezéchiel 16.39 Jérémie 13.22 Ezéchiel 23.29 1 Pierre 3.3-3.4 Osée 2.3
27 Hivyo ndivyo nitakavyoukomesha uasherati wako, na uzinzi wako, ulioletwa toka nchi ya Misri; usije ukawainulia macho yako, na kukumbuka Misri tena.
Ezéchiel 16.41 Ezéchiel 23.19 Ezéchiel 23.3 Esaïe 27.9 Michée 5.10-5.14
28 Maana Bwana MUNGU asema hivi, Tazama nitakutia katika mikono yao unaowachukia, katika mikono yao, ambao roho imefarakana nao;
Ezéchiel 23.22 Ezéchiel 16.37 Ezéchiel 23.17 Jérémie 34.20 Jérémie 21.7-21.10
29 nao watakutenda mambo kwa chuki, watakuondolea kazi zako zote, watakuacha uchi, huna nguo na aibu ya mambo yako ya kikahaba itafunuliwa, uasherati wako na uzinzi wako.
Ezéchiel 23.45-23.47 Ezéchiel 16.39 Ezéchiel 23.25-23.26 Deutéronome 28.47-28.51 Ezéchiel 23.18
30 Utatendwa mambo hayo kwa sababu umezini na hao wasioamini, na kwa sababu umetiwa unajisi kwa vinyago vyao.
Ezéchiel 6.9 Jérémie 16.11-16.12 Psaumes 106.35-106.38 Jérémie 2.18-2.20 Ezéchiel 23.7
31 Umekwenda katika njia ya umbu lako; basi nitatia kikombe chake katika mkono wako.
Jérémie 7.14-7.15 2 Rois 21.13 Jérémie 25.15 Daniel 9.12 Ezéchiel 23.13
32 Bwana MUNGU asema hivi; Utakinywea kikombe cha umbu lako; chenye nafasi nyingi kikubwa; utadhihakiwa na kudharauliwa; kimejaa sana.
Esaïe 51.17 Psaumes 60.3 Ezéchiel 22.4-22.5 1 Rois 9.7 Apocalypse 18.6
33 Utajazwa ulevi na sikitiko, kwa kikombe cha ushangao na ukiwa, kikombe cha umbu lako Samaria.
Jérémie 25.27 Habakuk 2.16 Esaïe 51.17 Esaïe 51.22 Jérémie 25.15-25.16
34 Naam, utakinywea hata hakitabaki kitu ndani yake, utavitafuna vigae vyake, utayararua maziwa yako; maana mimi, Bwana MUNGU, nimenena neno hili.
Psaumes 75.8 Esaïe 51.17 Ezéchiel 23.8 Apocalypse 18.7 Ezéchiel 23.3
35 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa umenisahau, na kunitupa nyuma yako, basi kwa hiyo, uchukue uasherati wako na uzinzi wako.
1 Rois 14.9 Ezéchiel 22.12 Jérémie 3.21 Esaïe 17.10 Osée 8.14
36 Tena Bwana akaniambia, Mwanadamu, utawahukumu Ohola na Oholiba? Basi uwahubiri machukizo yao.
Ezéchiel 22.2 Ezéchiel 20.4 Ezéchiel 16.2 Esaïe 58.1 Jérémie 1.10
37 Maana wamezini, na damu imo mikononi mwao, nao wamezini na vinyago vyao; tena wana wao walionizalia wamewapitisha katika moto ili waliwe nao.
Ezéchiel 16.36 Ezéchiel 20.26 Ezéchiel 16.20-16.21 Ezéchiel 16.38 Ezéchiel 23.39
38 Tena wamenitenda haya; wamepatia unajisi mahali pangu patakatifu, siku ile ile, nao wamezitangua sabato zangu.
Ezéchiel 20.13 2 Rois 21.7 Ezéchiel 7.20 Ezéchiel 20.24 Jérémie 17.27
39 Kwa maana walipokuwa wamekwisha kuvichinjia vinyago vyao watoto wao, ndipo walipoingia patakatifu pangu, siku ile ile, wapatie unajisi, na tazama, wamefanya hivyo kati ya nyumba yangu.
2 Rois 21.4 Jérémie 23.11 Ezéchiel 44.7 Ezéchiel 23.38 Esaïe 3.9
40 Tena mmewatuma watu kuwaita watokao mbali; ambao mjumbe alitumwa kwao, na tazama, wakaja; nawe ulijiosha kwa ajili yao, ulitia rangi macho yako, na kujipamba vyombo vya uzuri;
Jérémie 4.30 2 Rois 9.30 Ezéchiel 16.13-16.16 Esaïe 3.18-3.23 Esaïe 57.9
41 ukaketi juu ya kitanda cha enzi, na meza imeandikwa tayari mbele yake, ambayo juu yake uliweka uvumba wangu na mafuta yangu.
Esther 1.6 Jérémie 44.17 Ezéchiel 44.16 Esaïe 65.11 Amos 6.4
42 Na sauti za wingi wa watu wenye hali ya raha zilikuwa pamoja naye; na pamoja na watu wasio na adabu, waliletwa walevi toka jangwani; wakawatia vikuku mikononi, na taji nzuri juu ya vichwa vyao.
Ezéchiel 16.11-16.12 Job 1.15 Exode 32.6 Amos 6.1-6.6 Exode 32.18-32.19
43 Ndipo nikasema, Huyo aliye mkongwe atafanya uzinzi! Sasa hao watazini naye, naam, na yeye!
Esdras 9.7 Daniel 9.16 Ezéchiel 23.3 Jérémie 13.23 Psaumes 106.6
44 Wakamwingilia kama watu wamwingiliavyo kahaba; ndivyo walivyowaingilia Ohola na Oholiba, wanawake wale waasherati.
Ezéchiel 23.3 Ezéchiel 23.9-23.13
45 Basi watu wenye haki watawahukumu, kwa hukumu iwapasayo wazinzi, na kwa hukumu iwapasayo wanawake wamwagao damu; kwa sababu wao ndio wazinzi, na mikononi mwao mna damu.
Lévitique 20.10 Osée 6.5 Ezéchiel 23.36-23.39 Jérémie 5.14 Ezéchiel 16.38-16.43
46 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Nitaleta kusanyiko la watu juu yao, nami nitawatoa warushwe huko na huko, na kutekwa nyara.
Ezéchiel 16.40 Jérémie 15.4 Jérémie 24.9 Jérémie 25.9 Jérémie 34.17
47 Na kusanyiko hilo watawapiga kwa mawe, na kuwaua kwa panga zao; watawaua wana wao na binti zao, na kuziteketeza nyumba zao kwa moto.
Ezéchiel 16.40-16.41 Jérémie 39.8 Ezéchiel 24.21 Ezéchiel 9.6 Jérémie 33.4-33.5
48 Hivyo nitaukomesha uasherati katika nchi hii, ili wanawake wote wafundishwe, wasifanye mambo ya uasherati wenu.
2 Pierre 2.6 Ezéchiel 23.27 Ezéchiel 16.41 Esaïe 26.9 Ezéchiel 36.25
49 Nao watawalipa ninyi malipo ya uasherati wenu, nanyi mtachukua dhambi za vinyago vyenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU.
Ezéchiel 7.4 Ezéchiel 9.10 Ezéchiel 20.38 Ezéchiel 7.9 Esaïe 59.18

Cette Bible est dans le domaine public.