Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 14.6
Bible en Swahili de l’est


Rejet des idolâtres

1 Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.
Ezéchiel 8.1 Ezéchiel 20.1 Ezéchiel 33.31 Esaïe 29.13 2 Rois 6.32
2 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
1 Rois 14.4 Amos 3.7
3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?
Ezéchiel 7.19 Ezéchiel 14.7 Esaïe 1.15 Ezéchiel 20.3 Jérémie 11.11
4 Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;
Esaïe 66.4 Ezéchiel 3.17-3.21 Ezéchiel 14.7 Esaïe 3.11 2 Rois 1.16
5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao.
Zacharie 11.8 Esaïe 1.4 Jérémie 2.31-2.32 Deutéronome 32.15-32.16 2 Thessaloniciens 2.9-2.11
6 Kwa sababu hiyo uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Rudini ninyi, mkageuke na kuviacha vinyago vyenu; mkageuze nyuso zenu zisielekee machukizo yenu yote.
Ezéchiel 18.30 Esaïe 30.22 Esaïe 2.20 Esaïe 55.6-55.7 Ezéchiel 14.4
7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;
Exode 20.10 Exode 12.48 Jérémie 37.1-37.3 Lévitique 20.2 Nombres 15.15
8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Ezéchiel 5.15 Ezéchiel 15.7 Jérémie 44.11 Ezéchiel 6.7 Esaïe 65.15
9 Na nabii akidanganyika, na kusema neno, mimi, Bwana, nimemdanganya nabii yule, nami nitaunyosha mkono wangu juu yake, na kumwangamiza, asiwe kati ya watu wangu Israeli.
Jérémie 4.10 Ezéchiel 20.25 Esaïe 66.4 Esaïe 9.12 Jérémie 14.15
10 Nao watauchukua uovu wao; uovu wa nabii utakuwa sawasawa na uovu wake yule amwendeaye aulize neno;
Jérémie 6.14-6.15 Jérémie 14.15 Jérémie 8.11-8.12 Ezéchiel 23.49 Ezéchiel 14.4
11 ili nyumba ya Israeli wasipotee mbali nami, wala wasijitie unajisi tena kwa makosa yao yote; bali wawe watu wangu, nami niwe Mungu wao, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 37.23 Ezéchiel 48.11 Ezéchiel 44.10 Ezéchiel 11.18-11.20 Ezéchiel 44.15

L’exemple de trois hommes justes

12 Neno la Bwana likanijia, kusema,
13 Mwanadamu, nchi itakapofanya dhambi na kuniasi, kwa kukosa, nikaunyosha mkono wangu juu yake, na kulivunja tegemeo la chakula chake, na kuipelekea njaa, na kukatilia mbali mwanadamu na mnyama;
Lévitique 26.26 Ezéchiel 4.16 Ezéchiel 14.21 Ezéchiel 15.8 Esaïe 3.1
14 wajapokuwa watu hawa watatu, Nuhu, na Danieli, na Ayubu, kuwamo ndani yake, wangejiokoa nafsi zao wenyewe tu kwa haki yao, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 15.1 Ezéchiel 14.20 Ezéchiel 28.3 Job 1.1 Job 1.5
15 Nikipitisha wanyama wabaya ndani ya nchi ile, wakaiharibu hata ikawa ukiwa, mtu awaye yote asiweze kupita ndani yake, kwa sababu ya wanyama hao;
Ezéchiel 5.17 Lévitique 26.22 Jérémie 15.3 1 Rois 20.36 2 Rois 17.25
16 wajapokuwamo watu hawa watatu ndani yake, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hawataokoa wana wala binti; wao wenyewe tu wataokoka, bali nchi ile itakuwa ukiwa.
Genèse 19.29 Nombres 14.28-14.29 Actes 27.24 Job 22.20 Ezéchiel 14.20
17 Au nikileta upanga juu ya nchi ile, na kusema, Upanga, pita kati ya nchi hii, hata nikawakatilia mbali na nchi hiyo wanadamu na wanyama;
Ezéchiel 21.3-21.4 Lévitique 26.25 Ezéchiel 25.13 Ezéchiel 5.12 Sophonie 1.3
18 wajapokuwamo watu hawa watatu ndani yake, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hawataokoa wana wala binti; bali wao wenyewe tu wataokoka.
19 Au nikipeleka tauni katika nchi ile, na kumwaga ghadhabu yangu juu yake, kwa damu; ili kuwakatilia mbali nayo wanadamu na wanyama;
Ezéchiel 38.22 Ezéchiel 5.12 2 Samuel 24.15 Ezéchiel 7.8 Jérémie 14.12
20 wajapokuwamo ndani yake Nuhu, na Danieli, na Ayubu, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hawataokoa wana wala binti; watajiokoa nafsi zao tu kwa haki yao.
Ezéchiel 14.14 Sophonie 2.3 Ezéchiel 14.16 Esaïe 3.10 Psaumes 33.18-33.19
21 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Je! U zaidi sana nitakapoleta hukumu zangu nne zilizo kali juu ya Yerusalemu, yaani, upanga, na njaa, na wanyama wabaya, na tauni, niwakatilie mbali nayo wanadamu na wanyama?
Ezéchiel 5.17 Ezéchiel 33.27 Ezéchiel 14.13 Ezéchiel 14.15 Ezéchiel 14.17
22 Lakini, tazama, watasalia mabaki watakaochukuliwa nje, wana na binti; tazama, watawatokea ninyi, nanyi mtaiona njia yao na matendo yao; nanyi mtafarijika katika habari ya mabaya niliyoleta juu ya Yerusalemu, naam, katika habari ya mambo yote niliyoleta juu yake.
Ezéchiel 20.43 Ezéchiel 12.16 Esaïe 6.13 Jérémie 30.11 Esaïe 65.8-65.9
23 Nao watawafariji ninyi, mtakapoona njia yao na matendo yao; nanyi mtajua ya kuwa sikufanya bila sababu mambo yote niliyoutenda, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 22.8-22.9 Genèse 18.22-18.33 Ezéchiel 8.6-8.18 Deutéronome 8.2 Proverbes 26.2

Cette Bible est dans le domaine public.