Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 47
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur les Philistins

1 Neno la Bwana lililomjia Yeremia, nabii, katika habari za Wafilisti, kabla Farao hajapiga Gaza.
Jérémie 25.20 Genèse 10.19 1 Rois 4.24 Zacharie 9.5-9.7 Exode 25.15-25.17
2 Bwana asema hivi, Tazama, maji yanatokea katika pande za kaskazini, nayo yatakuwa mto ufurikao, nayo yataifunika nchi, na kila kitu kilichomo, huo mji na wote wakaao ndani yake; nao watu watalia na watu wote wakaao katika nchi watapiga yowe.
Jérémie 8.16 Jérémie 1.14 Esaïe 8.7-8.8 Jérémie 46.20 Esaïe 15.2-15.5
3 Kwa sababu ya mshindo wa kukanyaga kwato za farasi wake walio hodari, kwa sababu ya mwendo wa mbiombio wa magari yake ya vita; kwa sababu ya ngurumo ya magurudumu yake, hao akina baba hawatazami nyuma ili kuwaangalia watoto wao, kwa kuwa mikono yao ni dhaifu;
Juges 5.22 Jérémie 8.16 Ezéchiel 26.10-26.11 Job 39.19-39.25 Nahum 2.4
4 kwa sababu ya siku ijayo kuwaangamiza Wafilisti wote, kukatilia mbali kila msaidizi wa Tiro na Sidoni asaliaye; maana Bwana atawaharibu Wafilisti, mabaki ya kisiwa cha Kaftori.
Amos 9.7 Deutéronome 2.23 Esaïe 20.6 Amos 1.8-1.10 Ezéchiel 7.5-7.7
5 Upaa umeupata Gaza; Ashkeloni umenyamazishwa Mabaki ya bonde lao; Hata lini utajikata-kata?
Jérémie 48.37 Jérémie 25.20 Michée 1.16 Jérémie 41.5 Zacharie 9.5-9.7
6 Ee upanga wa Bwana, Siku ngapi zitapita kabla hujatulia? Ujitie katika ala yako; Pumzika, utulie.
Jérémie 12.12 Ezéchiel 21.3-21.5 Jérémie 4.21 Esaïe 10.5 Jérémie 12.4
7 Utawezaje kutulia, Ikiwa Bwana amekupa agizo? Juu ya Ashkeloni na juu ya pwani, Ndipo alipoyaamuru hayo.
Michée 6.9 Ezéchiel 14.17 Esaïe 10.6 Esaïe 13.3 Ezéchiel 25.16

Cette Bible est dans le domaine public.