Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 38.10
Bible en Swahili de l’est


Jérémie dans une citerne

1 Na Shefatia, mwana wa Matani, na Gedalia, mwana wa Pashuri, na Yukali, mwana wa Shelemia, na Pashuri, mwana wa Malkiya, wakayasikia maneno ambayo Yeremia aliwaambia watu wote, kusema,
Actes 5.28 Esdras 2.3 Néhémie 7.9 Actes 4.6-4.10 1 Chroniques 9.12
2 Bwana asema hivi, Akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; bali yeye atokaye kwenda kwa Wakaldayo ataishi, naye atapewa maisha yake yawe kama nyara, naye ataishi.
Jérémie 34.17 Jérémie 39.18 Jérémie 45.5 Jérémie 42.17 Jérémie 44.13
3 Bwana asema hivi, Bila shaka mji huu utatiwa katika mikono ya jeshi la mfalme wa Babeli, naye atautwaa.
Jérémie 21.10 Jérémie 32.3-32.5
4 Ndipo wakuu wakamwambia mfalme, Twakuomba, mtu huyu auawe, kwa kuwa aidhoofisha mikono ya watu wa vita, waliobaki katika mji huu, na mikono ya watu wote, kwa kuwaambia maneno kama hayo; maana mtu huyu hawatafutii watu hawa heri, bali shari.
Jérémie 26.11 1 Rois 18.17-18.18 Amos 7.10 1 Rois 21.20 Exode 5.4
5 Naye mfalme Sedekia akasema, Tazama, yu mikononi mwenu; maana mfalme siye awezaye kufanya neno lo lote kinyume chenu.
2 Samuel 3.39 2 Samuel 19.22 1 Samuel 15.24 Jean 19.12-19.16 Proverbes 29.25
6 Basi wakamtwaa Yeremia, wakamtupa katika shimo la Malkiya, mwana wa mfalme, lililo katika uwanda wa walinzi; wakamshusha kwa kamba. Na mle shimoni hamkuwa na maji, ila matope tu; naye Yeremia akazama katika matope hayo.
Jérémie 37.16 Zacharie 9.11 Jérémie 37.21 Psaumes 40.2 Actes 16.24
7 Basi, Ebedmeleki, Mkushi, towashi, aliyekuwa katika nyumba ya mfalme, aliposikia kama wamemtia Yeremia shimoni; na wakati huo mfalme alikuwa amekaa katika lango la Benyamini;
Jérémie 29.2 Jérémie 37.13 Deutéronome 21.19 Amos 5.10 Luc 10.30-10.36
8 Ebedmeleki akatoka nyumbani mwa mfalme, akamwambia mfalme, akisema,
9 Ee bwana wangu, mfalme, watu hawa wametenda mabaya katika mambo yote waliyomtenda Yeremia, nabii, ambaye wamemtupa shimoni; naye hakosi atakufa pale alipo, kwa sababu ya njaa; kwa kuwa hapana mkate kabisa katika mji.
Jérémie 52.6 Jérémie 37.21-38.6 Job 31.34 Proverbes 31.8-31.9 Esther 7.4-7.6
10 Ndipo mfalme akamwamuru Ebedmeleki, Mkushi, akisema, Chukua pamoja nawe watu thelathini toka hapa, ukamtoe Yeremia shimoni, kabla hajafa.
Proverbes 21.1 Esther 5.2 Esther 8.7 Psaumes 75.10
11 Basi Ebedmeleki akawachukua watu hao pamoja naye, akaingia ndani ya nyumba ya mfalme chini ya ghala, akatoa mle nguo zilizotupwa, na vitambaa vikuukuu, akamtelemshia Yeremia shimoni kwa kamba.
12 Naye Ebedmeleki, Mkushi, akamwambia Yeremia, Tia nguo hizi zilizotupwa, na vitambaa hivi vikuukuu, chini ya kamba kwapani. Naye Yeremia akafanya hivyo.
Romains 12.15 Ephésiens 4.32 Romains 12.10
13 Basi wakamwinua Yeremia kwa kamba hizo, wakamtoa shimoni; naye Yeremia akakaa katika uwanda wa walinzi.
Jérémie 37.21 Actes 23.35 Actes 28.30 Actes 28.16 Actes 24.23-24.26

Entretien de Jérémie avec Sédécias

14 Kisha mfalme Sedekia akatuma watu, akamleta nabii Yeremia kwake, ndani ya maingilio ya tatu ya nyumba ya Bwana; mfalme akamwambia Yeremia, Nataka kukuuliza neno, nawe usinifiche neno lo lote.
Jérémie 21.1-21.2 Jérémie 37.17 1 Samuel 3.17-3.18 Jérémie 42.20 Jérémie 42.2-42.5
15 Basi Yeremia akamwambia Sedekia, Kama nikikufunulia neno hilo, je! Hutaniua wewe? Tena, mimi nikikupa shauri wewe hutanisikiliza.
Luc 22.67-22.68
16 Basi Sedekia mfalme akamwapia Yeremia kwa siri, akisema, Kama Bwana aishivyo, yeye aliyetufanyia roho zetu, sitakuua, wala sitakutia katika mikono ya watu hao wanaokutafuta wakuue.
Jérémie 37.17 Esaïe 57.16 Zacharie 12.1 Nombres 27.16 Nombres 16.22
17 Ndipo Yeremia akamwambia Sedekia, Bwana, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kama ukitoka kwenda kwa wakuu wa mfalme wa Babeli, basi nafsi yako utaishi, wala mji huu hautateketezwa; nawe utaishi na nyumba yako;
Jérémie 38.2 Jérémie 27.12 Jérémie 39.3 1 Chroniques 17.24 Jérémie 27.17
18 bali ukikataa kutoka kwenda kwa wakuu wa mfalme wa Babeli, basi, mji huu utatiwa katika mikono ya Wakaldayo nao watauteketeza, hata na wewe hutajiepusha na mikono yao.
Jérémie 38.3 2 Rois 25.4-25.10 Jérémie 24.8-24.10 Jérémie 32.3-32.5 Jérémie 37.8
19 Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, Nawaogopa Wayahudi waliowakimbilia Wakaldayo, wasije wakanitia katika mikono yao, nao wakanidhihaki.
Jean 12.42 Jean 19.12-19.13 Jérémie 38.22 Esaïe 51.12-51.13 Esaïe 57.11
20 Lakini Yeremia akasema, La! Hawatakutoa. Nakusihi, uitii sauti ya Bwana katika hayo ninayokuambia; ndivyo itakavyokufaa, na nafsi yako utaishi.
Esaïe 55.3 Actes 26.29 2 Chroniques 20.20 Daniel 4.27 Jérémie 26.13
21 Lakini kama ukikataa kutoka, hili ndilo neno ambalo Bwana amenionyesha;
Jérémie 15.19-15.21 Actes 20.26-20.27 Nombres 23.19-23.20 Actes 18.6 Nombres 24.13
22 Tazama, wanawake wote, walioachwa ndani ya nyumba ya mfalme wa Yuda, watatolewa na kuchukuliwa kwa wakuu wa mfalme wa Babeli, na wanawake hao watasema, Rafiki zako walio karibu wamekudanganya, nao wamekushinda; na kwa kuwa miguu yako imezama matopeni sasa, wamegeuka na kurudi nyuma.
Jérémie 20.10 Jérémie 43.6 Psaumes 69.2 Psaumes 69.14 Psaumes 41.9
23 Na watawatoa wake zako, na watoto wako wote, na kuwachukua kwa Wakaldayo; wala wewe hutapona na mikono yao, bali utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babeli, nawe utakuwa sababu ya kuteketezwa mji huu.
Jérémie 41.10 Jérémie 39.6 Jérémie 38.18 2 Rois 25.7 Ezéchiel 14.9
24 Ndipo Sedekia akamwambia Yeremia, Mtu ye yote asipate habari ya maneno haya, nawe hutakufa.
25 Lakini kama wakuu wakisikia ya kuwa nimenena nawe, nao wakija kwako, na kukuambia, Tufunulie sasa uliyomwambia mfalme; usimfiche, nasi hatutakuua; na pia uliyoambiwa na mfalme;
Jérémie 38.27 Jérémie 38.4-38.6
26 basi, utawaambia, Nalimwomba mfalme asinirudishe nyumbani kwa Yonathani, nisije nikafa humo.
Jérémie 37.20 Jérémie 37.15 Esther 4.8 Jérémie 42.2
27 Ndipo wakuu wakamwendea Yeremia, wakamwuliza; naye akawaambia sawasawa na maneno aliyoamriwa na mfalme. Basi wakaacha kunena naye; maana neno lile halikujulikana.
1 Samuel 10.15-10.16 1 Samuel 16.2-16.5 2 Rois 6.19 Actes 23.6
28 Basi Yeremia akakaa katika uwanda wa walinzi hata siku ile Yerusalemu ulipotwaliwa.
Jérémie 39.14 Jérémie 37.21 Jérémie 15.20-15.21 Jérémie 38.13 Psaumes 23.4

Cette Bible est dans le domaine public.