Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 30.17
Bible en Swahili de l’est


Annonce de restauration

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
Jérémie 1.1-1.2 Jérémie 26.15
2 Bwana Mungu wa Israeli, asema hivi, ya kwamba, Uyaandike kitabuni maneno hayo yote niliyokuambia.
Esaïe 30.8 Jérémie 36.32 Apocalypse 1.11 Jérémie 51.60-51.64 Job 19.23-19.24
3 Kwa maana, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapowarejeza watu wangu wa Israeli na Yuda waliofungwa, asema Bwana; nami nitawarudisha hata nchi niliyowapa baba zao, nao wataimiliki.
Jérémie 16.15 Jérémie 29.14 Ezéchiel 20.42 Jérémie 32.44 Jérémie 30.18
4 Na haya ndiyo maneno aliyosema Bwana, katika habari za Israeli, na katika habari za Yuda.
5 Maana Bwana asema hivi, Tumesikia sauti ya tetemeko, na ya hofu, wala si ya amani.
Amos 5.16-5.18 Esaïe 5.30 Jérémie 6.23-6.25 Jérémie 25.36 Luc 23.29-23.30
6 Ulizeni sasa, mkaone kwamba mwanamume aona utungu wa uzazi; mbona, basi, ninaona kila mtu anaweka mikono yake viunoni, kama mwanamke aliye na utungu, na nyuso zote zimegeuka rangi.
Joël 2.6 Jérémie 4.31 Nahum 2.10 1 Thessaloniciens 5.3 Osée 13.13
7 Ole! Maana siku ile ni kuu, hata hapana inayofanana nayo, maana ni wakati wa taabu yake Yakobo; lakini ataokolewa nayo.
Joël 2.11 Daniel 12.1 Jérémie 30.10 Lamentations 1.12 Osée 1.11
8 Na itakuwa katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitaivunja nira yake itoke shingoni mwako, nami nitavipasua vifungo vyako; wala wageni hawatamtumikisha tena;
Ezéchiel 34.27 Jérémie 27.2 Nahum 1.13 Esaïe 9.4 Jérémie 28.10
9 bali watamtumikia Bwana, Mungu wao, na Daudi, mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
Osée 3.5 Luc 1.69 Actes 2.30 Esaïe 55.3-55.5 Actes 13.23
10 Kwa sababu hiyo usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu, asema Bwana; wala usifadhaike, Ee Israeli; kwa maana, tazama, nitakuokoa toka mbali, na wazao wako toka nchi ya uhamisho wao; na Yakobo atarudi, naye atatulia na kustarehe, wala hapana mtu atakayemtia hofu.
Esaïe 43.5 Jérémie 46.27-46.28 Jérémie 29.14 Esaïe 35.9 Esaïe 44.2
11 Maana mimi ni pamoja nawe, asema Bwana, nikuokoe; maana nitawakomesha kabisa mataifa yote huko nilikokutawanya, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu.
Jérémie 10.24 Jérémie 4.27 Esaïe 8.10 Jérémie 5.10 Psaumes 6.1
12 Maana Bwana asema hivi, Maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa.
Jérémie 15.18 Jérémie 14.17 2 Chroniques 36.16 Jérémie 30.15 Ezéchiel 37.11
13 Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha yako huna dawa ziponyazo.
Jérémie 46.11 Jérémie 8.22 Job 34.29 Jérémie 33.6 Esaïe 59.16
14 Wote wakupendao wamekusahau; hawakutafuti; maana nimekujeruhi kwa jeraha ya adui, kwa adhabu ya mtu mkatili; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zilikuwa zimeongezeka.
Job 30.21 Jérémie 5.6 Lamentations 1.2 Jérémie 22.20 Jérémie 4.30
15 Mbona unalilia maumivu yako? Hayaponyeki maumivu yako; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka, nimekutenda haya.
Jérémie 30.14 Jérémie 30.12 Jérémie 11.13 Malachie 4.1-4.2 Esdras 9.13
16 Basi, watu wote wakulao wataliwa; na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo.
Jérémie 10.25 Esaïe 14.2 Esaïe 33.1 Exode 23.22 Nahum 1.8
17 Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye.
Psaumes 107.20 1 Pierre 2.24 Jérémie 33.6 Exode 15.26 Esaïe 11.12
18 Bwana asema hivi, Tazama, nitarudisha tena hema za Yakobo zilizohamishwa, na kuyahurumia makao yake; nao mji huo utajengwa juu ya magofu yake wenyewe, nalo jumba litakaliwa, kama ilivyokuwa desturi yake.
Aggée 2.7-2.9 Jérémie 30.3 Psaumes 102.13 Zacharie 1.16 1 Chroniques 29.19
19 Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao wachangamkao; nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala hawatakuwa wanyonge.
Esaïe 51.11 Jérémie 33.22 Esaïe 35.10 Jérémie 31.4 Psaumes 126.1-126.2
20 Watoto wao nao watakuwa kama zamani, na kusanyiko lao litathibitika mbele zangu, nami nitawaadhibu wote wawaoneao.
Psaumes 90.16-90.17 Esaïe 51.22 Esaïe 49.26 Esaïe 1.26-1.27 Jérémie 2.3
21 Na mkuu wao atakuwa mtu wa kwao wenyewe, naye mwenye kuwatawala atakuwa mtu wa jamaa yao; nami nitamkaribisha, naye atanikaribia; maana ni nani aliye na moyo wa kuthubutu kunikaribia? Asema Bwana.
Nombres 16.5 Deutéronome 18.18 Ezéchiel 34.23-34.24 Ezéchiel 37.24 Genèse 49.10
22 Nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
Ezéchiel 36.28 Ezéchiel 37.27 Jérémie 31.1 Jérémie 31.33 Zacharie 13.9
23 Tazama, tufani ya Bwana, yaani, ghadhabu yake, imetokea tufani ya kudumu; itawaangukia waovu vichwani.
Jérémie 25.32 Jérémie 23.19-23.20 Zacharie 9.14 Psaumes 58.9 Proverbes 1.27
24 Hasira kali ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha kutenda, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za mwisho mtayafahamu haya.
Jérémie 23.20 Osée 3.5 Jérémie 4.28 Jérémie 49.39 Nombres 24.14

Cette Bible est dans le domaine public.