Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 18.23
Bible en Swahili de l’est


Illustration du potier et du vase

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
2 Ondoka, ukashuke mpaka nyumba ya mfinyanzi, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
Jérémie 19.1-19.2 Hébreux 1.1 Jérémie 23.22 Jérémie 13.1 Esaïe 20.2
3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu.
Jonas 1.3 Jean 15.14 Actes 26.19
4 Na chombo kile, alichokuwa akikifinyanga, kilipoharibika mkononi mwake yule mfinyanzi, alikifanyiza tena kuwa chombo kingine, kama alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya.
Jérémie 18.6 Romains 9.20-9.23 Esaïe 45.9
5 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile kama mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema Bwana. Angalieni, kama udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo ninyi katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.
Esaïe 64.8 Esaïe 45.9 Matthieu 20.15 Daniel 4.23 Jérémie 18.4
7 Wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuung’oa, na kuuvunja, na kuuangamiza;
Jérémie 1.10 Jérémie 45.4 Jérémie 12.14-12.17 Jérémie 25.9-25.14 Amos 9.8
8 ikiwa taifa lile nililolitaja litageuka, na kuacha maovu yake nitaghairi, nisitende mabaya yale niliyoazimia kuwatenda.
Ezéchiel 18.21 Jérémie 26.13 Osée 11.8 Jérémie 26.3 Juges 2.18
9 Na wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuujenga na kuupanda,
Jérémie 1.10 Jérémie 31.28 Amos 9.11-9.15 Jérémie 11.17 Ecclésiaste 3.2
10 ikiwa watatenda maovu mbele za macho yangu, wasiitii sauti yangu, basi nitaghairi, nisitende mema yale niliyoazimia kuwatendea.
1 Samuel 2.30 1 Samuel 13.13 Ezéchiel 33.18 1 Samuel 15.11 Psaumes 125.5
11 Haya! Basi, ukawaambie watu wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, ukisema, Bwana asema hivi, Tazama, ninafinyanga mabaya juu yenu, na kuwaza mawazo juu yenu; rudini sasa, kila mmoja na aiache njia yake mbaya; zitengenezeni njia zenu, na matendo yenu.
2 Rois 17.13 Jérémie 35.15 Esaïe 1.16-1.19 Jérémie 25.5 Jérémie 7.3
12 Lakini wao wasema, Hapana tumaini lo lote; maana sisi tutafuata mawazo yetu wenyewe, nasi tutatenda kila mmoja wetu kwa kuufuata ushupavu wa moyo wake mbaya.
Jérémie 2.25 Deutéronome 29.19 Jérémie 16.12 Esaïe 57.10 Jérémie 7.24
13 Basi, kwa ajili ya hayo, Bwana asema hivi, Ulizeni sasa katika mataifa, ni nani aliyesikia habari za mambo kama hayo; bikira wa Israeli ametenda tendo lichukizalo sana.
Jérémie 5.30 Osée 6.10 Jérémie 23.14 Esaïe 66.8 Jérémie 2.10-2.13
14 Je! Theluji ya Lebanoni itakoma katika jabali la kondeni? Au je! Maji ya baridi yashukayo toka mbali yatakauka?
Jean 6.68
15 Maana watu wangu wamenisahau, wameufukizia ubatili uvumba; nao wamewakaza katika njia zao, katika mapito ya zamani, ili wapite katika njia za kando, katika njia isiyotengenezwa;
Esaïe 57.14 Jérémie 6.16 Jérémie 10.15 Jérémie 2.32 Jérémie 2.13
16 ili kufanya nchi yao kuwa kitu cha kushangaza, na cha kuzomewa daima; kila mtu apitaye karibu nayo atashangaa, na kutikisa kichwa chake.
Psaumes 22.7 Jérémie 25.9 Jérémie 50.13 Jérémie 49.13 Ezéchiel 33.28-33.29
17 Nami nitawatawanya mbele ya adui, kama kwa upepo wa mashariki; nami nitaviangalia visogo vyao, wala si nyuso zao, siku ya msiba wao.
Jérémie 13.24 Jérémie 2.27 Osée 13.15 Job 27.21 Psaumes 48.7
18 Hapo ndipo waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na tumpige kwa ndimi zetu, wala tusiyaangalie maneno yake yo yote.
Jérémie 11.19 Psaumes 52.2 Malachie 2.7 Psaumes 21.11 Psaumes 64.3
19 Niangalie, Ee Bwana, ukasikilize sauti ya wanaoshindana nami.
Néhémie 6.9 Michée 7.8 Psaumes 109.28 Jérémie 20.12 Psaumes 55.16-55.17
20 Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili niseme mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.
Psaumes 57.6 Psaumes 35.7 Psaumes 106.23 1 Samuel 24.17-24.19 Psaumes 35.12
21 Kwa sababu hiyo, uwatoe watoto wao waone njaa, uwatoe nguvu za upanga ziwapate; wake zao wafiwe na watoto wao, na kufiwa na waume zao; wanaume wao wauawe, na vijana wao wapigwe kwa upanga vitani.
Psaumes 109.9-109.20 Exode 22.24 Jérémie 15.8 Amos 4.10 Jérémie 16.3-16.4
22 Kilio na kisikiwe kitokacho katika nyumba zao, hapo utakapoleta kikosi juu yao kwa ghafula; kwa maana wamenichimbia shimo waninase, nao wameifichia miguu yangu mitego.
Jérémie 6.26 Psaumes 140.5 Sophonie 1.10-1.11 Jérémie 25.34-25.36 Sophonie 1.16
23 Lakini wewe, Bwana, unajua mashauri yao yote juu yangu, ya kuniua; usiwasamehe uovu wao, wala usifute dhambi yao mbele za macho yako; bali wakwazwe mbele zako; uwatende mambo wakati wa hasira yako.
Esaïe 2.9 Psaumes 35.4 Psaumes 69.22-69.28 Psaumes 109.14-109.15 Néhémie 4.4-4.5

Cette Bible est dans le domaine public.