Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 13.1
Bible en Swahili de l’est


La ceinture de lin

1 Bwana akaniambia hivi, Enenda, ukajinunulie mshipi wa kitani, ukajivike viuno, wala usiutie majini.
Jérémie 13.11 Ezéchiel 4.1-4.5 Hébreux 1.1 Jérémie 27.2 Jérémie 19.1
2 Basi nikanunua mshipi sawasawa na neno la Bwana, nikajivika viunoni.
Ezéchiel 2.8 Esaïe 20.2 Osée 1.2-1.3 Proverbes 3.5 Jean 15.14
3 Nalo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
Jérémie 13.8
4 Twaa mshipi ule ulioununua, ulio viunoni mwako, kisha ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukaufiche huko katika pango la jabali.
Jérémie 51.63-51.64 Psaumes 137.1 Michée 4.10
5 Basi nikaenda, nikauficha karibu na mto Frati, kama Bwana alivyoniamuru.
Exode 40.16 Exode 39.42-39.43 Hébreux 11.17-11.19 Actes 26.19-26.20 Matthieu 22.2-22.6
6 Hata ikawa, baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, Ondoka, enenda mpaka mto Frati, ukautwae ule mshipi, niliokuamuru kuuficha huko.
7 Ndipo nikaenda mpaka mto Frati, nikachimba, nikautwaa ule mshipi katika mahali pale nilipouficha; na tazama, mshipi ulikuwa umeharibika, haukufaa tena kwa lo lote.
Esaïe 64.6 Jérémie 24.1-24.8 Jérémie 13.10 Romains 3.12 Luc 14.34-14.35
8 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
9 Bwana asema hivi, Jinsi iyo hiyo nitakiharibu kiburi cha Yuda, na kiburi kikuu cha Yerusalemu.
Lévitique 26.19 Esaïe 23.9 Jérémie 13.15-13.17 Esaïe 2.10-2.17 Sophonie 3.11
10 Watu hawa waovu, wanaokataa kusikiliza maneno yangu, wanaokwenda kwa ushupavu wa mioyo yao, na kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu, watakuwa hali moja na mshipi huu, usiofaa kwa lo lote.
Jérémie 16.12 2 Chroniques 36.15-36.16 Jérémie 9.14 Nombres 14.11 Jérémie 11.7-11.8
11 Maana kama vile mshipi unavyoshikamana na viuno vya mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami nyumba yote ya Israeli; na nyumba yote ya Yuda, asema Bwana; wapate kuwa watu kwangu mimi, na jina, na sifa, na utukufu; lakini hawakutaka kusikia.
Jérémie 33.9 Exode 19.5-19.6 Esaïe 43.21 Psaumes 81.11 Psaumes 147.20
12 Basi utawaambia neno hili, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila chupa itajazwa divai; nao watakuambia, Je, sisi hatujui ya kuwa kila chupa itajazwa divai?
Ezéchiel 24.19
13 Ndipo utakapowaambia, Bwana asema hivi, Tazama, nitawajaza ulevi wenyeji wote wa nchi hii, hata wafalme wanaoketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
Psaumes 75.8 Esaïe 51.17 Esaïe 63.6 Psaumes 60.3 Jérémie 51.7
14 Nitawagonganisha, mtu na mwenzake, naam, baba za watu na watoto wao pamoja, asema Bwana; sitahurumia, wala sitaachilia, wala sitarehemu, hata nisiwaangamize.
Deutéronome 29.20 Esaïe 27.11 Jérémie 6.21 Psaumes 2.9 Esaïe 9.20-9.21
15 Sikilizeni ninyi, kategeni masikio yenu; msifanye kiburi; maana Bwana amenena.
Esaïe 28.14-28.22 Amos 7.15 Joël 1.2 Actes 4.19-4.20 Apocalypse 2.29
16 Mtukuzeni Bwana, Mungu wenu, kabla hajaleta giza, na kabla miguu yenu haijakwaa juu ya milima yenye giza; na wakati mnapoitazamia nuru, kabla hajaigeuza kuwa kivuli cha mauti, na giza nene.
Esaïe 8.22 Esaïe 59.9 Josué 7.19 Esaïe 60.2 Proverbes 4.19
17 Bali kama hamtaki kusikia, roho yangu italia kwa siri, kwa sababu ya kiburi chenu; na jicho langu litalia sana na kutoka machozi mengi, kwa kuwa kundi la Bwana limechukuliwa hali ya kufungwa.
Jérémie 9.1 Malachie 2.2 Psaumes 80.1 Jérémie 14.17 Psaumes 119.136
18 Mwambie mfalme, na mama ya mfalme, Nyenyekeeni na kuketi chini; Kwa maana vilemba vyenu vimeshuka, naam, taji ya utukufu wenu.
2 Rois 24.12 Jérémie 22.26 2 Rois 24.15 2 Chroniques 33.19 2 Chroniques 33.12
19 Miji ya Negebu imefungwa malango yake, wala hapana mtu wa kuyafungua; Yuda amechukuliwa hali ya kufungwa; amechukuliwa kabisa hali ya kufungwa.
Jérémie 52.27 2 Rois 25.21 Deutéronome 28.52 Jérémie 52.30 Jérémie 39.9
20 Inua macho yako, Ee Yerusalemu, ukawatazame hawa wanaokuja kutoka kaskazini; liko wapi kundi lako ulilopewa, kundi lile zuri?
Jérémie 6.22 Habakuk 1.6 Jérémie 1.14 Jérémie 23.2 Jérémie 13.17
21 Utasema nini wewe, atakapowaweka rafiki zako kuwa kichwa juu yako, ikiwa wewe mwenyewe umewafundisha kuwa juu yako? Je! Huzuni haitakushika, kama utungu wa mwanamke aliye katika kuzaa?
Esaïe 13.8 Jérémie 4.31 Jérémie 5.31 Jérémie 38.22 Esaïe 10.3
22 Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya wingi wa uovu wako, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia.
Nahum 3.5 Jérémie 5.19 Osée 2.10 Jérémie 16.10-16.11 Jérémie 9.2-9.9
23 Je! Mkushi aweza kuibadili ngozi yake, au chui madoa-doa yake? Kama aweza, ndipo na ninyi mwaweza kutenda mema, ninyi mliozoea kutenda mabaya.
Matthieu 19.24-19.28 Jérémie 9.5 Jérémie 2.22 Esaïe 1.5 Proverbes 27.22
24 Kwa sababu hiyo nitawatawanya, kama makapi yapitayo, kwa upepo wa jangwani.
Psaumes 1.4 Lévitique 26.33 Ezéchiel 5.2 Ezéchiel 5.12 Osée 13.3
25 Hiyo ndiyo kura yako, fungu lako ulilopimiwa na mimi, asema Bwana; kwa kuwa umenisahau, na kuutumainia uongo.
Job 20.29 Jérémie 2.32 Matthieu 24.51 Psaumes 9.17 Psaumes 11.6
26 Kwa ajili ya hayo, mimi nami nitayafunua marinda yako mbele ya uso wako, na aibu yako itaonekana.
Lamentations 1.8 Osée 2.10 Ezéchiel 23.29 Jérémie 13.22 Ezéchiel 16.37
27 Nimeona machukizo yako, naam, uzinifu wako, na ubembe wako, na uasherati wa ukahaba wako, juu ya milima katika mashamba. Ole wako, Ee Yerusalemu! Hutaki kutakaswa; mambo hayo yataendelea hata lini?
Ezéchiel 6.13 Osée 8.5 Ezéchiel 24.13 Esaïe 65.7 Jérémie 5.7-5.8

Cette Bible est dans le domaine public.