Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 1.3
Bible en Swahili de l’est


Prophéties sur Juda

Appel et mission de Jérémie

1 Maneno ya Yeremia, mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani waliokuwa katika Anathothi, katika nchi ya Benyamini;
1 Chroniques 6.60 Ezéchiel 1.3 2 Chroniques 36.21 Jérémie 32.7-32.9 Jérémie 11.21
2 ambaye neno la Bwana lilimjia katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa kumiliki kwake.
Jérémie 25.3 Jérémie 1.11 Jérémie 1.4 2 Rois 21.24-22.20 Osée 1.1
3 Tena lilikuja siku za Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, hata mwisho wa mwaka wa kumi na mmoja wa Sedekia, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; hata wakati ulipochukuliwa mateka Yerusalemu, katika mwezi wa tano.
2 Chroniques 36.5-36.8 Jérémie 39.2 2 Rois 23.34 2 Rois 24.17-25.30 1 Chroniques 3.15
4 Neno la Bwana lilinijia, kusema,
Ezéchiel 3.16 Ezéchiel 1.3 Jérémie 1.2
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Esaïe 49.1 Psaumes 139.16 Psaumes 71.5-71.6 Romains 8.29 Galates 1.15-1.16
6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
Exode 6.12 Jérémie 32.17 Exode 4.10-4.16 1 Rois 3.7-3.9 Exode 4.1
7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.
Nombres 22.20 Marc 16.15-16.16 Matthieu 28.20 Actes 20.27 Ezéchiel 2.3-2.5
8 Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.
Josué 1.5 Josué 1.9 Exode 3.12 Jérémie 15.20-15.21 Deutéronome 31.6
9 Ndipo Bwana akaunyosha mkono wake, akanigusa kinywa changu; Bwana akaniambia, Tazama, nimetia maneno yangu kinywani mwako;
Exode 4.11-4.12 Ezéchiel 3.10 Exode 4.15-4.16 Luc 12.12 Jérémie 5.14
10 angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.
Jérémie 31.28 2 Corinthiens 10.4-10.5 Jérémie 31.4-31.5 Ezéchiel 32.18 Ezéchiel 36.36
11 Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi.
Amos 7.8 Amos 8.2 Zacharie 5.2 Zacharie 4.2 Jérémie 24.3
12 Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.
Ezéchiel 12.28 Ezéchiel 12.25 Deutéronome 32.35 Ezéchiel 12.22-12.23 Jérémie 39.1-39.18
13 Neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema, Waona nini? Nikasema, Naona sufuria lenye maji yatokotayo, na mdomo wake unaelekea toka upande wa kaskazini.
Ezéchiel 11.7 Ezéchiel 11.3 2 Corinthiens 13.1-13.2 Genèse 41.32 Ezéchiel 24.3-24.14
14 Ndipo Bwana akaniambia, Toka kaskazini mabaya yatatokea, na kuwapata watu wote wakaao katika nchi hii.
Jérémie 10.22 Jérémie 4.6 Esaïe 41.25 Ezéchiel 1.4 Jérémie 6.22
15 Kwa kuwa, tazama, nitaziita jamaa zote za falme za kaskazini, asema Bwana; nao watakuja, na kuweka kila mtu kiti chake cha enzi mbele ya mahali pa kuingilia malango ya Yerusalemu, na kuzielekea kuta zake pande zote, na kuielekea miji yote ya Yuda.
Jérémie 4.16 Jérémie 25.9 Jérémie 39.3 Jérémie 9.11 Esaïe 22.7
16 Nami nitatamka hukumu zangu juu yao kwa habari ya uovu wao wote; kwa kuwa wameniacha mimi, wakaifukizia uvumba miungu mingine, wakaziabudu kazi za mikono yao wenyewe.
Jérémie 7.9 Jérémie 19.4 Deutéronome 28.20 Esaïe 2.8 Jérémie 4.12
17 Haya basi, wewe jifunge viuno, ukaondoke ukawaambie maneno yote niliyokuamuru; usifadhaike kwa ajili yao, nisije nikakufadhaisha wewe mbele yao.
1 Rois 18.46 Ezéchiel 3.14-3.18 1 Pierre 1.13 Ezéchiel 3.10-3.11 Jérémie 23.28
18 Maana, tazama, nimekufanya leo kuwa mji wenye boma, na nguzo ya chuma, na kuta za shaba, juu ya nchi yote; juu ya wafalme wa Yuda, na juu ya wakuu wake, na juu ya makuhani wake, na juu ya watu wa nchi hii.
Jérémie 6.27 Esaïe 50.7 Jérémie 15.20 Ezéchiel 3.8-3.9 Jérémie 42.22
19 Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.
Josué 1.9 Jérémie 1.8 Jérémie 20.11 Jérémie 20.1-20.6 Jérémie 26.11-26.24

Cette Bible est dans le domaine public.