Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 64
Bible en Swahili de l’est


1 Laiti ungepasua mbingu, na kushuka, ili milima iteteme mbele zako;
Michée 1.3-1.4 Amos 9.13 Marc 1.10 Psaumes 68.8 Exode 19.11
2 kama vile moto uchomapo vichaka, na moto uchemshapo maji; ili kuwajulisha adui zako jina lako, mataifa wakatetemeke mbele zako!
Jérémie 5.22 Psaumes 99.1 Jérémie 33.9 Daniel 6.25-6.27 Michée 7.15-7.17
3 Ulipofanya mambo ya kutisha tusiyoyatazamia, ulishuka, milima ikatetema mbele zako.
Psaumes 106.22 Psaumes 66.5 Psaumes 66.3 Psaumes 65.5-65.6 Deutéronome 10.21
4 Maana tangu zamani za kale watu hawakusikia, wala kufahamu kwa masikio, wala jicho halikuona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake amngojaye.
Psaumes 31.19 1 Corinthiens 2.9-2.10 Esaïe 25.9 Colossiens 1.26-1.27 Jacques 5.7
5 Wewe wamlaki yeye afurahiaye yaliyo haki na kuyatenda, watu wale wakukumbukao katika njia zako; tazama, ulikuwa na hasira, nasi tulitenda dhambi; tumekuwa katika mambo haya muda mwingi; nasi, je! Tutaokolewa?
Exode 20.24 Psaumes 90.7-90.9 Exode 30.6 Hébreux 4.16 Psaumes 25.10
6 Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi; sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo.
Psaumes 90.5-90.6 Ephésiens 2.1-2.2 Job 42.5-42.6 Job 14.4 Romains 7.24
7 Tena hapana aliitiaye jina lako, ajitahidiye akushike; kwa kuwa umetuficha uso wako, nawe umetukomesha kwa njia ya maovu yetu.
Esaïe 59.16 Osée 7.7 Ezéchiel 22.30 Esaïe 54.8 Esaïe 56.4
8 Lakini sasa, Ee Bwana, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.
Esaïe 29.16 Esaïe 45.9 Jérémie 18.2-18.6 Romains 9.20-9.24 Esaïe 63.16
9 Ee Bwana, usione hasira nyingi, wala usiukumbuke uovu siku zote; tazama, angalia, twakusihi, sisi sote tu watu wako.
Psaumes 79.13 Psaumes 74.1-74.2 Jérémie 10.24 Psaumes 6.1 Malachie 1.4
10 Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa, Sayuni umekuwa jangwa, Yerusalemu umekuwa ukiwa.
Esaïe 1.7 Lamentations 2.4-2.8 Luc 21.24 Apocalypse 11.1-11.2 2 Rois 25.9
11 Nyumba yetu takatifu, nzuri, walimokusifu baba zetu, imeteketea moto; vitu vyetu vyote vyenye kupendeza vimeharibika.
2 Rois 25.9 Lamentations 1.7 Psaumes 74.5-74.7 2 Chroniques 36.19 Lamentations 1.10-1.11
12 Utajizuia usiyaangalie mambo haya, Ee Bwana? Utanyamaza, na kututesa sana?
Esaïe 42.14 Psaumes 74.10-74.11 Psaumes 74.18-74.19 Zacharie 1.12 Psaumes 83.1

Cette Bible est dans le domaine public.