Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 39.2
Bible en Swahili de l’est


Délégation de Babylone auprès d’Ézéchias

1 Wakati huo Merodaki-baladani, mwana wa Baladani, mfalme wa Babeli, alipeleka barua na zawadi kwa Hezekia; kwa maana amepata habari kwamba amekuwa hawezi, na kwamba amepona.
2 Rois 20.12-20.19 2 Chroniques 32.31 Esaïe 13.1 Esaïe 13.19 2 Chroniques 32.23
2 Hezekia akawafurahia, akawaonyesha nyumba yake yenye vitu vyake vya thamani, fedha na dhahabu, na manukato, na marhamu ya thamani, na nyumba yote yenye silaha zake za vita, na vitu vyote vilivyoonekana katika hazina zake; hapakuwa na kitu nyumbani mwake wala katika ufalme wake asichowaonyesha.
2 Chroniques 32.31 2 Chroniques 32.25 Jérémie 17.9 Job 31.25 Psaumes 146.3-146.4
3 Ndipo Isaya nabii akamwendea mfalme Hezekia, akamwambia, Watu hawa walisema nini? Nao wametoka wapi kuja kwako? Hezekia akasema, Wametoka katika nchi iliyo mbali, wakaja kwangu toka Babeli.
Deutéronome 28.49 2 Samuel 12.1 2 Chroniques 16.7 Jérémie 5.15 2 Rois 20.14-20.15
4 Ndipo akasema, Wameona nini katika nyumba yako? Hezekia akajibu, Wameviona vitu vyote vilivyomo nyumbani mwangu; hapana kitu katika hazina zangu nisichowaonyesha.
Josué 7.19 Job 31.33 Proverbes 28.13 1 Jean 1.9 Proverbes 23.5
5 Ndipo Isaya akamwambia Hezekia, Basi, lisikie neno la Bwana wa majeshi.
1 Samuel 15.16 1 Samuel 13.13-13.14
6 Tazama, siku zinakuja, ambazo vitu vyote vilivyomo nyumbani mwako, na hivyo vilivyowekwa akiba na baba zako hata leo, vitachukuliwa mpaka Babeli; hapana kitu cho chote kitakachosalia; asema Bwana.
2 Rois 24.13 2 Rois 25.13-25.15 Jérémie 20.5 2 Rois 20.17-20.19 2 Chroniques 36.18
7 Na baadhi ya wana wako utakaowazaa, watakaotoka kwako, watawachukulia mbali; nao watakuwa matowashi katika jumba la mfalme wa Babeli.
2 Rois 24.12 2 Chroniques 36.10 2 Rois 25.6-25.7 Daniel 1.1-1.7 2 Chroniques 33.11
8 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya, Neno la Bwana ulilolinena ni jema. Tena akamwambia, Maana itakuwapo amani na kweli katika siku zangu mimi.
2 Chroniques 34.28 2 Chroniques 32.26 Lévitique 10.3 Lamentations 3.39 Zacharie 8.19

Cette Bible est dans le domaine public.