Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 31.5
Bible en Swahili de l’est


Dieu, seul auteur du salut

1 Ole wao watelemkao kwenda Misri wapate msaada, na kutegemea farasi; watumainio magari kwa kuwa ni mengi, na wapanda farasi kwa kuwa ni hodari sana; lakini hawamwangalii Mtakatifu wa Israeli, wala hawamtafuti Bwana!
Psaumes 20.7 Esaïe 36.6 Deutéronome 17.16 Daniel 9.13 Esaïe 30.16
2 Lakini yeye naye ana akili, naye ataleta uovu, wala hatayatangua maneno yake; bali ataondoka juu ya nyumba yao watendao mabaya, na juu ya msaada wa hao watendao maovu.
Nombres 23.19 Esaïe 45.7 Amos 3.6 Matthieu 24.35 Nombres 10.35
3 Basi Wamisri ni wanadamu wala si Mungu, na farasi zao ni nyama wala si roho; na Bwana atakaponyosha mkono wake, yeye asaidiaye atajikwaa, na yeye asaidiwaye ataanguka, nao wote pamoja watakoma.
Esaïe 9.17 Ezéchiel 28.9 Ezéchiel 20.33-20.34 Jérémie 15.6 Jérémie 37.7-37.10
4 Maana Bwana aniambia hivi, Kama vile ilivyo simba angurumapo na mwana-simba juu ya mawindo yake, wachungaji wengi wakiitwa ili kumpiga, lakini hatiwi hofu na sauti zao, wala kufanya woga kwa sababu ya mshindo wao; ndivyo Bwana wa majeshi atakavyoshuka ili kufanya vita juu ya mlima Sayuni, na juu ya kilima chake.
Amos 3.8 Osée 11.10 Esaïe 42.13 Zacharie 12.8 Zacharie 14.3
5 Kama ndege warukao, Bwana wa majeshi ataulinda Yerusalemu; ataulinda na kuuokoa, atapita juu yake na kuuhifadhi.
Deutéronome 32.11 Psaumes 91.4 Esaïe 38.6 Esaïe 37.35 Psaumes 37.40
6 Mwelekeeni yeye mliyemwasi sana, enyi wana wa Israeli.
Jérémie 3.14 Esaïe 55.7 Jérémie 3.10 Jérémie 3.22 Esaïe 48.8
7 Maana katika siku hiyo kila mtu atatupa sanamu zake za fedha, na sanamu zake za dhahabu, ambazo mikono yenu imezifanya, zikawa dhambi kwenu.
Esaïe 2.20 Esaïe 30.22 Osée 8.11 Osée 14.8 1 Rois 12.28-12.30
8 Ndipo huyo Mwashuri ataanguka kwa upanga ambao si wa mtu; na upanga usio upanga wa mtu utamla; naye ataukimbia upanga, na vijana wake watatoa kodi.
Esaïe 14.25 Genèse 49.15 Osée 1.7 Esaïe 37.7 2 Chroniques 32.21
9 Na mwamba wake utatoweka kwa sababu ya hofu, nao wakuu wake wataionea bendera hofu kuu, asema Bwana, ambaye moto wake u katika Sayuni, na tanuru yake katika Yerusalemu.
Esaïe 29.6 Lévitique 6.13 Deutéronome 32.37 Deutéronome 32.31 Esaïe 10.17

Cette Bible est dans le domaine public.