Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 20.1
Bible en Swahili de l’est


Égyptiens et Éthiopiens prisonniers

1 Katika mwaka ule jemadari Yule alipofika Ashdodi,alipotumwa na Sargoni mfalme wa Ashuru;naye alipigana na Ashdodi akautwaa.
2 Rois 18.17 Jérémie 25.20 Amos 1.8 1 Samuel 5.1 1 Samuel 6.17
2 wakati huo Bwana alinena kwa kinywa cha Isaya, mwana wa Amozi, akisema, Haya, uvue nguo ya magunia viunoni mwako, na viatu vyako miguuni mwako.
Michée 1.8 1 Samuel 19.24 Ezéchiel 24.23 Ezéchiel 24.17 Zacharie 13.4
3 Naye akafanya hivyo akaenda uchi, miguu yake haina viatu. Bwana akasema, Kama vile mtumishi wangu Isaya anavyokwenda uchi, hana viatu, awe ishara na ajabu kwa muda wa miaka mitatu juu ya Misri na juu ya Kushi;
Esaïe 8.18 Esaïe 37.9 Esaïe 43.3 Apocalypse 11.2-11.3 Esaïe 18.1-18.7
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawachukua uchi, wafungwa wa Misri, na watu wa Kushi waliohamishwa, watoto kwa wazee, hawana viatu, matako yao wazi, Misri iaibishwe.
Esaïe 19.4 Jérémie 13.22 Jérémie 13.26 Michée 1.11 Ezéchiel 30.18
5 Nao watafadhaika, na kuona haya kwa ajili ya Kushi, matumaini yao, na Misri, utukufu wao.
Esaïe 30.3 Esaïe 30.5 Jérémie 17.5 Jérémie 9.23-9.24 1 Corinthiens 3.21
6 Na mwenyeji wa nchi ya pwani atasema katika siku hiyo, Angalia, haya ndiyo yaliyowapata watu wale tuliowatumaini, ambao tuliwakimbilia watuokoe na mfalme wa Ashuru; na sisi je! Twawezaje kupona?
Hébreux 2.3 Matthieu 23.33 1 Thessaloniciens 5.3 Jérémie 30.15-30.17 Esaïe 31.1-31.3

Cette Bible est dans le domaine public.