Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 3.8
Bible en Swahili de l’est


Un temps pour tout

1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Ecclésiaste 3.17 Ecclésiaste 8.5-8.6 Ecclésiaste 2.3 2 Rois 5.26 Matthieu 16.3
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
Hébreux 9.27 Job 14.5 Actes 7.20 Galates 4.4 Genèse 21.1-21.2
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Osée 6.1-6.2 1 Samuel 2.6 Jérémie 45.4 Zacharie 1.12 Jérémie 33.6
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
Exode 15.20 Romains 12.15 Jean 16.20-16.22 Psaumes 126.5-126.6 Jacques 4.9
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
2 Rois 3.25 Joël 2.16 2 Samuel 18.17-18.18 Exode 19.15 Josué 4.3-4.9
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
Matthieu 16.25-16.26 Marc 8.35-8.37 Philippiens 3.7-3.8 Luc 9.24-9.25 Psaumes 112.9
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
Amos 5.13 Genèse 37.29 2 Rois 5.7 Jérémie 8.14 1 Samuel 19.4-19.5
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Luc 14.26 Ephésiens 5.25 Ephésiens 3.19 2 Chroniques 19.2 2 Chroniques 20.1-20.30
9 Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?
Ecclésiaste 1.3 Matthieu 16.26 Ecclésiaste 5.16 Proverbes 14.23 Ecclésiaste 2.11
10 Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
Genèse 3.19 Ecclésiaste 2.26 Ecclésiaste 1.13-1.14 1 Thessaloniciens 2.9 2 Thessaloniciens 3.8
11 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
Romains 11.33 Romains 1.19-1.20 Ecclésiaste 8.17 Genèse 1.31 Deutéronome 32.4
12 Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.
Ecclésiaste 3.22 Psaumes 37.3 1 Thessaloniciens 5.15-5.16 Deutéronome 28.63 Philippiens 4.4-4.9
13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
Ecclésiaste 2.24 Ecclésiaste 9.7 Ecclésiaste 5.18-5.20 Psaumes 128.2 Esaïe 65.21-65.23
14 Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.
Jacques 1.17 Romains 11.36 Psaumes 33.11 Apocalypse 15.4 Proverbes 30.6
15 Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo yale yaliyopita.
Ecclésiaste 1.9-1.10 Ecclésiaste 6.10

L’homme et la bête

16 Zaidi ya hayo, nikaona tena chini ya jua ya kwamba, Mahali pa hukumu upo uovu, Na mahali pa haki upo udhalimu.
Ecclésiaste 4.1 Ecclésiaste 5.8 Esaïe 59.14 Michée 2.2 Actes 23.3
17 Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.
Matthieu 16.27 Ecclésiaste 3.1 2 Corinthiens 5.10 Psaumes 98.9 2 Thessaloniciens 1.6-1.10
18 Nikasema moyoni mwangu, Ni kwa sababu ya wanadamu, ili Mungu awajaribu, nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama.
Psaumes 73.22 Genèse 3.17-3.19 2 Pierre 2.12 Psaumes 51.4 Romains 9.23
19 Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
Psaumes 49.12 Psaumes 49.20 Psaumes 89.47-89.48 Job 14.10-14.12 2 Samuel 14.14
20 Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.
Genèse 3.19 Job 34.15 Job 7.9 Job 10.9-10.10 Ecclésiaste 6.6
21 Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?
Ecclésiaste 12.7 2 Corinthiens 5.1 Jean 14.3 Luc 16.22-16.23 Philippiens 1.23
22 Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye.
Ecclésiaste 3.11-3.12 Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 10.14 Ecclésiaste 2.24 Ecclésiaste 8.7

Cette Bible est dans le domaine public.