Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 3.20
Bible en Swahili de l’est


Un temps pour tout

1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Ecclésiaste 3.17 Ecclésiaste 8.5-8.6 Ecclésiaste 2.3 2 Rois 5.26 Proverbes 15.23
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
Hébreux 9.27 Job 14.5 Actes 7.20 Galates 4.4 Matthieu 13.41
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Osée 6.1-6.2 1 Samuel 2.6 Deutéronome 32.39 Esaïe 5.5-5.6 Daniel 9.25-9.27
4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza;
Exode 15.20 Romains 12.15 Jean 16.20-16.22 Psaumes 30.5 Psaumes 126.5-126.6
5 Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia;
2 Rois 3.25 Joël 2.16 1 Corinthiens 7.5 1 Samuel 21.4-21.5 Cantique 2.6-2.7
6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
Luc 9.24-9.25 Matthieu 16.25-16.26 Marc 8.35-8.37 Philippiens 3.7-3.8 Deutéronome 8.17-8.18
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
Amos 5.13 Genèse 37.29 Amos 8.3 Esther 7.4 Actes 9.39
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Luc 14.26 Ephésiens 5.25 Apocalypse 2.2 Genèse 14.14-14.17 Ephésiens 3.19
9 Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?
Ecclésiaste 1.3 Ecclésiaste 5.16 Proverbes 14.23 Ecclésiaste 2.11 Matthieu 16.26
10 Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
Genèse 3.19 Ecclésiaste 2.26 Ecclésiaste 1.13-1.14 1 Thessaloniciens 2.9 2 Thessaloniciens 3.8
11 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
Romains 11.33 Romains 1.19-1.20 Ecclésiaste 8.17 Genèse 1.31 Deutéronome 32.4
12 Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.
Ecclésiaste 3.22 Psaumes 37.3 1 Timothée 6.18 1 Thessaloniciens 5.15-5.16 Deutéronome 28.63
13 Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.
Ecclésiaste 2.24 Esaïe 65.21-65.23 Ecclésiaste 9.7 Ecclésiaste 5.18-5.20 Psaumes 128.2
14 Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.
Jacques 1.17 Romains 11.36 Psaumes 33.11 Actes 2.23 Proverbes 19.21
15 Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo yale yaliyopita.
Ecclésiaste 1.9-1.10 Ecclésiaste 6.10

L’homme et la bête

16 Zaidi ya hayo, nikaona tena chini ya jua ya kwamba, Mahali pa hukumu upo uovu, Na mahali pa haki upo udhalimu.
Ecclésiaste 4.1 Ecclésiaste 5.8 1 Rois 21.9-21.21 Jacques 2.6 Michée 7.3
17 Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.
Matthieu 16.27 Ecclésiaste 3.1 2 Corinthiens 5.10 Psaumes 98.9 2 Thessaloniciens 1.6-1.10
18 Nikasema moyoni mwangu, Ni kwa sababu ya wanadamu, ili Mungu awajaribu, nao waone ya kuwa wao wenyewe wafanana na wanyama.
Psaumes 73.22 Genèse 3.17-3.19 Job 14.1-14.4 Psaumes 90.5-90.12 2 Pierre 2.12
19 Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.
Psaumes 49.12 Psaumes 49.20 Psaumes 39.5-39.6 Psaumes 104.29 Ecclésiaste 2.20-2.23
20 Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.
Genèse 3.19 Job 34.15 Psaumes 104.29 Job 7.9 Job 10.9-10.10
21 Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?
Ecclésiaste 12.7 2 Corinthiens 5.8 Actes 1.25 2 Corinthiens 5.1 Jean 14.3
22 Hivyo nikaona ya kwamba hakuna jema kupita mwanadamu kuzifurahia kazi zake; kwa sababu hili ni fungu lake; kwa maana ni nani atakayemrudisha tena ili ayaone yatakayomfuata baadaye.
Ecclésiaste 2.24 Ecclésiaste 8.7 Ecclésiaste 3.11-3.12 Ecclésiaste 6.12 Ecclésiaste 10.14

Cette Bible est dans le domaine public.