Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 13
Bible en Swahili de l’est


1 Mwana mwenye hekima husikiliza mausia ya babaye; Bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.
Proverbes 10.1 Proverbes 15.20 Proverbes 9.7-9.8 Esaïe 28.14-28.15 Proverbes 4.20-4.22
2 Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake; Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri.
Proverbes 12.14 Proverbes 18.20 Proverbes 1.31 Proverbes 1.11-1.13 Psaumes 140.11
3 Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake; Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu.
Proverbes 21.23 Proverbes 18.7 Jacques 3.2-3.12 Proverbes 18.21 Proverbes 12.13
4 Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.
Proverbes 12.24 Proverbes 10.4 Proverbes 12.11 Proverbes 2.2-2.9 Proverbes 11.25
5 Mwenye haki huchukia kusema uongo; Bali mtu mbaya huwa karaha, hupatwa na aibu.
Colossiens 3.9 Proverbes 3.35 Ephésiens 4.25 Ezéchiel 6.9 Zacharie 11.8
6 Haki humlinda yeye aliye mnyofu katika njia yake; Bali ubaya humwangusha mwenye dhambi.
Proverbes 11.3 Proverbes 11.5-11.6 Psaumes 15.2 Psaumes 140.11 2 Chroniques 28.23
7 Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu; Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.
1 Corinthiens 4.10-4.11 Luc 18.11-18.14 Apocalypse 3.17 2 Corinthiens 6.10 Proverbes 13.11
8 Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake; Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote.
2 Rois 25.12 Exode 21.30 Jérémie 39.10 1 Pierre 1.18-1.19 Matthieu 16.26
9 Nuru ya mwenye haki yang’aa sana; Bali taa ya mtu mbaya itazimika.
Proverbes 4.18 Proverbes 24.20 Psaumes 112.4 Matthieu 25.8 1 Rois 11.36
10 Kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
Jacques 4.1 Proverbes 20.18 3 Jean 1.9-1.10 1 Rois 12.10-12.11 Juges 12.1-12.6
11 Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.
Proverbes 20.21 Proverbes 10.2 Jacques 5.1-5.5 Proverbes 28.8 Job 20.15
12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.
Proverbes 13.19 Jean 16.22 Psaumes 119.81-119.83 Proverbes 11.30 1 Samuel 1.26-1.28
13 Kila alidharauye neno hujiletea uharibifu; Bali yeye aiogopaye amri atapewa thawabu.
2 Chroniques 36.16 Nombres 15.31 Psaumes 115.13 2 Jean 1.8 Psaumes 19.11
14 Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.
Proverbes 10.11 Proverbes 14.27 Psaumes 18.5 Psaumes 116.3 Proverbes 16.17
15 Ufahamu mwema huleta upendeleo; Bali njia ya haini huparuza.
Proverbes 3.4 Luc 2.52 Jérémie 2.19 Actes 7.10 Romains 6.21
16 Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa; Bali mpumbavu hueneza upumbavu.
Proverbes 15.2 Ecclésiaste 10.3 Proverbes 21.24 Proverbes 12.22-12.23 Esaïe 52.13
17 Mjumbe mbaya huanguka maovuni; Bali mjumbe mwaminifu ni afya.
Proverbes 25.13 2 Corinthiens 2.17 Proverbes 25.23 1 Corinthiens 4.2 2 Timothée 2.2
18 Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa; Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.
Proverbes 15.5 Proverbes 15.31-15.32 Proverbes 12.1 Proverbes 19.6 Proverbes 25.12
19 Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu; Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.
Proverbes 13.12 Job 28.28 Proverbes 3.7 Psaumes 34.14 Proverbes 29.27
20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
1 Corinthiens 15.33-15.34 Proverbes 9.6 2 Corinthiens 6.14-6.18 Proverbes 15.31 Apocalypse 18.4
21 Uovu huwaandamia wenye dhambi; Bali mwenye haki atalipwa mema.
Psaumes 32.10 Genèse 4.7 Proverbes 13.13 Romains 2.7-2.10 Esaïe 3.10-3.11
22 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.
Proverbes 28.8 Job 27.16-27.17 Ecclésiaste 2.26 Genèse 17.7-17.8 Esdras 9.12
23 Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini; Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.
Proverbes 12.11 Proverbes 28.19 Proverbes 27.18 Ecclésiaste 8.5-8.6 Jérémie 8.7-8.10
24 Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.
Proverbes 29.15 Proverbes 19.18 Proverbes 22.15 Proverbes 23.13-23.14 Proverbes 29.17
25 Mwenye haki hula akaishibisha nafsi yake; Bali tumbo la mtu mbaya litaona njaa.
Psaumes 34.10 Proverbes 10.3 Hébreux 13.5 Deutéronome 32.24 Proverbes 6.11

Cette Bible est dans le domaine public.