Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 77.6
Bible en Swahili de l’est


Les hauts faits de Dieu dans le passé

1 Nimpazie Mungu sauti yangu, Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
Psaumes 3.4 Psaumes 39.1 Psaumes 50.1 Psaumes 142.1-142.3 Psaumes 62.1
2 Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana; Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea; Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
Psaumes 50.15 Esaïe 26.9 Genèse 37.35 Esaïe 26.16 Psaumes 18.6
3 Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika; Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
Psaumes 61.2 Job 31.23 Psaumes 88.3-88.18 Psaumes 42.11 Psaumes 143.4-143.5
4 Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike; Naliona mashaka nisiweze kunena.
Job 2.13 Esther 6.1 Psaumes 6.6 Job 7.13-7.15 Job 6.3
5 Nalifikiri habari za siku za kale, Miaka ya zamani zilizopita.
Psaumes 143.5 Esaïe 51.9 Deutéronome 32.7 Psaumes 44.1 Michée 7.14-7.15
6 Nakumbuka wimbo wangu usiku, Nawaza moyoni mwangu, Roho yangu ikatafuta.
Psaumes 4.4 Psaumes 42.8 Ecclésiaste 1.16 Habakuk 3.17-3.18 Lamentations 3.40
7 Je! Bwana atatupa milele na milele? Hatatenda fadhili tena kabisa?
Psaumes 85.1 Psaumes 85.5 Psaumes 79.5 Romains 11.1-11.2 Psaumes 44.9
8 Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?
Nombres 23.19 Romains 9.6 Nombres 14.34 Jérémie 15.18 2 Pierre 3.9
9 Mungu amesahau fadhili zake? Amezuia kwa hasira rehema zake?
Esaïe 49.14-49.15 Esaïe 40.27 Romains 11.32 Esaïe 63.15 Psaumes 51.1
10 Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo; Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.
Psaumes 31.22 Marc 9.24 Lamentations 3.18-3.23 Psaumes 116.11 Psaumes 77.5
11 Nitayakumbuka matendo ya Bwana; Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
Psaumes 143.5 Psaumes 105.5 Psaumes 28.5 Psaumes 78.11 1 Chroniques 16.12
12 Pia nitaitafakari kazi yako yote; Nitaziwaza habari za matendo yako.
Psaumes 143.5 Psaumes 105.2 Deutéronome 6.7 Luc 24.14-24.32 Psaumes 104.34
13 Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu; Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?
Psaumes 73.17 Exode 15.11 Psaumes 63.2 Deutéronome 32.31 Esaïe 40.25
14 Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu; Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.
Josué 9.9-9.10 Esaïe 51.9 Exode 15.11 Daniel 6.27 Psaumes 136.4
15 Kwa mkono wako umewakomboa watu wako, Wana wa Yakobo na Yusufu.
Deutéronome 9.29 Exode 6.6 Esaïe 63.9 Genèse 48.3-48.20 Deutéronome 9.26
16 Ee Mungu, yale maji yalikuona, Yale maji yalikuona, yakaogopa. Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
Exode 14.21 Josué 3.15-3.16 Habakuk 3.8-3.10 Habakuk 3.15 Psaumes 114.3-114.6
17 Mawingu yakamwaga maji. Mbingu nazo zikatoa sauti, Mishale yako nayo ikatapakaa.
Psaumes 18.14 Habakuk 3.11 Psaumes 68.33 Psaumes 68.8-68.9 2 Samuel 22.15
18 Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli; Umeme uliuangaza ulimwengu. Nchi ilitetemeka na kutikisika;
Psaumes 97.4 Exode 19.16 Exode 19.18 Habakuk 3.4 Apocalypse 11.19
19 Njia yako ilikuwa katika bahari. Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; Hatua zako hazikujulikana.
Habakuk 3.15 Exode 14.28 Néhémie 9.11 Nahum 1.3-1.4 Psaumes 97.2
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi, Kwa mkono wa Musa na Haruni.
Psaumes 78.52 Exode 13.21 Esaïe 63.11-63.12 Psaumes 80.1 Exode 14.19

Cette Bible est dans le domaine public.