Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 77.13
Bible en Swahili de l’est


Les hauts faits de Dieu dans le passé

1 Nimpazie Mungu sauti yangu, Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
Psaumes 3.4 Psaumes 50.1 Psaumes 39.1 1 Chroniques 25.3 1 Chroniques 16.41-16.42
2 Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana; Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea; Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
Esaïe 26.9 Genèse 37.35 Psaumes 50.15 Esaïe 26.16 Genèse 32.7-32.12
3 Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika; Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
Psaumes 61.2 Job 6.4 Lamentations 3.39 Job 23.15-23.16 Job 31.23
4 Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike; Naliona mashaka nisiweze kunena.
Job 6.3 Job 2.13 Esther 6.1 Psaumes 6.6 Job 7.13-7.15
5 Nalifikiri habari za siku za kale, Miaka ya zamani zilizopita.
Deutéronome 32.7 Psaumes 143.5 Esaïe 51.9 Psaumes 44.1 Esaïe 63.9-63.15
6 Nakumbuka wimbo wangu usiku, Nawaza moyoni mwangu, Roho yangu ikatafuta.
Psaumes 4.4 Psaumes 42.8 Actes 16.25 1 Corinthiens 11.28-11.32 Job 35.10
7 Je! Bwana atatupa milele na milele? Hatatenda fadhili tena kabisa?
Psaumes 85.1 Psaumes 85.5 Psaumes 13.1-13.2 Psaumes 37.24 Psaumes 89.38
8 Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?
Romains 9.6 Nombres 23.19 Luc 16.25-16.26 Esaïe 27.11 Nombres 14.34
9 Mungu amesahau fadhili zake? Amezuia kwa hasira rehema zake?
Esaïe 49.14-49.15 Psaumes 40.11 Luc 13.25-13.28 Esaïe 40.27 Romains 11.32
10 Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo; Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.
Psaumes 31.22 Exode 15.6 Habakuk 3.2-3.13 Job 42.3 Marc 9.24
11 Nitayakumbuka matendo ya Bwana; Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
Psaumes 143.5 Psaumes 105.5 Psaumes 111.4 Esaïe 5.12 Psaumes 28.5
12 Pia nitaitafakari kazi yako yote; Nitaziwaza habari za matendo yako.
Psaumes 71.24 Psaumes 145.11 Psaumes 145.4 Psaumes 143.5 Psaumes 105.2
13 Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu; Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?
Exode 15.11 Psaumes 73.17 Psaumes 63.2 Deutéronome 32.31 Psaumes 89.6-89.8
14 Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu; Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.
Psaumes 136.4 Exode 13.14 Josué 9.9-9.10 Esaïe 51.9 Exode 15.11
15 Kwa mkono wako umewakomboa watu wako, Wana wa Yakobo na Yusufu.
Exode 6.6 Deutéronome 9.29 Psaumes 136.11-136.12 Psaumes 74.2 Esaïe 63.9
16 Ee Mungu, yale maji yalikuona, Yale maji yalikuona, yakaogopa. Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
Exode 14.21 Josué 3.15-3.16 Psaumes 114.3-114.6 Habakuk 3.8-3.10 Habakuk 3.15
17 Mawingu yakamwaga maji. Mbingu nazo zikatoa sauti, Mishale yako nayo ikatapakaa.
Psaumes 18.14 Psaumes 144.6 Juges 5.4 Habakuk 3.11 Psaumes 68.33
18 Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli; Umeme uliuangaza ulimwengu. Nchi ilitetemeka na kutikisika;
Psaumes 97.4 2 Samuel 22.8 Juges 5.4 Apocalypse 18.1 Exode 19.16
19 Njia yako ilikuwa katika bahari. Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; Hatua zako hazikujulikana.
Habakuk 3.15 Nahum 1.3-1.4 Exode 14.28 Néhémie 9.11 Psaumes 29.10
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi, Kwa mkono wa Musa na Haruni.
Exode 13.21 Psaumes 78.52 Exode 14.19 Esaïe 63.11-63.12 Psaumes 80.1

Cette Bible est dans le domaine public.