Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 62.3
Bible en Swahili de l’est


Dieu le seul refuge

1 Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya, Wokovu wangu hutoka kwake.
Psaumes 37.7 Psaumes 33.20 Psaumes 37.39 Psaumes 123.2 Psaumes 130.5-130.6
2 Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.17 Psaumes 62.6 2 Corinthiens 4.8-4.9 1 Corinthiens 10.13
3 Hata lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama kitalu kilicho tayari kuanguka,
Psaumes 140.2 Psaumes 38.12 Proverbes 1.22 Psaumes 82.2 Psaumes 4.2
4 Hufanya shauri kumwangusha tu katika cheo chake; Huufurahia uongo. Kwa kinywa chao hubariki; Kwa moyo wao hulaani.
Psaumes 28.3 Psaumes 55.21 Psaumes 5.9 Romains 7.22 Psaumes 119.163
5 Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa kimya. Tumaini langu hutoka kwake.
Psaumes 27.13-27.14 Michée 7.7 Psaumes 71.5 Psaumes 104.1 Psaumes 146.1
6 Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana.
Psaumes 62.2 Psaumes 16.8 Psaumes 112.6 Proverbes 12.7 Osée 1.7
7 Kwa Mungu wokovu wangu, Na utukufu wangu; Mwamba wa nguvu zangu, Na kimbilio langu ni kwa Mungu.
Jérémie 3.23 Psaumes 85.9 Esaïe 45.25 Psaumes 94.22 Jérémie 9.23-9.24
8 Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu.
Philippiens 4.6 Lamentations 2.19 1 Samuel 1.15 Psaumes 142.2 Psaumes 42.4
9 Hakika binadamu ni ubatili, Na wenye cheo ni uongo, Katika mizani huinuka; Wote pamoja ni hafifu kuliko ubatili.
Psaumes 39.5 Esaïe 40.15 Esaïe 40.17 Psaumes 39.11 Matthieu 21.9
10 Msiitumainie dhuluma, Wala msijivune kwa unyang’anyi; Mali izidipo msiiangalie sana moyoni.
Esaïe 30.12 Psaumes 52.7 Deutéronome 8.12-8.14 Jérémie 17.11 Esaïe 59.4
11 Mara moja amenena Mungu; Mara mbili nimeyasikia haya, Ya kuwa nguvu zina Mungu,
Apocalypse 19.1 Psaumes 68.34-68.35 Esaïe 26.4 Job 33.14 Job 40.5
12 Na fadhili ziko kwako, Ee Bwana; Maana ndiwe umlipaye kila mtu Sawasawa na haki yake.
Job 34.11 Matthieu 16.27 Psaumes 103.8 Daniel 9.9 1 Corinthiens 3.8

Cette Bible est dans le domaine public.