Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 58.6
Bible en Swahili de l’est


Condamnation des juges injustes

1 Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki? Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?
Psaumes 57.1 2 Samuel 23.3 Deutéronome 16.18-16.19 Luc 23.50-23.51 Actes 5.21
2 Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu; Katika nchi mnapima udhalimu wa mikono yenu.
Psaumes 94.20 Esaïe 10.1 Ecclésiaste 3.16 Ezéchiel 22.27 Michée 3.9-3.12
3 Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.
Psaumes 51.5 Esaïe 48.8 Esaïe 46.3 Proverbes 22.15 Ephésiens 2.3
4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.
Psaumes 140.3 Ecclésiaste 10.11 Matthieu 3.7 Job 20.14 Romains 3.13
5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.
Deutéronome 18.11 Esaïe 19.3 Jérémie 8.17
6 Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.
Psaumes 3.7 Job 29.17 Psaumes 10.15 Nombres 23.24 Job 4.10-4.11
7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.
Psaumes 112.10 Josué 7.5 Esaïe 13.7 Psaumes 64.3 Josué 2.9-2.11
8 Kama konokono ayeyukaye na kutoweka, Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,
Job 3.16 Ecclésiaste 6.3 Jacques 1.10 Psaumes 37.35-37.36 Matthieu 24.35
9 Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, Ataipeperusha kama chamchela, Iliyo mibichi na iliyo moto.
Psaumes 118.12 Proverbes 10.25 Ecclésiaste 7.6 Psaumes 10.2 Proverbes 1.27
10 Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.
Psaumes 68.23 Psaumes 64.10 Psaumes 107.42 Apocalypse 11.17-11.18 Apocalypse 18.20
11 Na mwanadamu atasema, Hakika iko thawabu yake mwenye haki. Hakika yuko Mungu Anayehukumu katika dunia.
Esaïe 3.10 Psaumes 67.4 Psaumes 92.15 Psaumes 64.9 Romains 6.21-6.22

Cette Bible est dans le domaine public.