Condamnation des juges injustes
 1 Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki? Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?
Psaumes 57.1  Actes 5.21  Matthieu 26.3  Psaumes 82.1-82.2  Psaumes 59.1  
 2 Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu; Katika nchi mnapima udhalimu wa mikono yenu.
Psaumes 94.20  Esaïe 10.1  Michée 3.9-3.12  Ezéchiel 22.12  Jean 11.47-11.53  
 3 Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.
Psaumes 51.5  Esaïe 48.8  Esaïe 46.3  Proverbes 22.15  Ephésiens 2.3  
 4 Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.
Psaumes 140.3  Ecclésiaste 10.11  Job 20.14  Romains 3.13  Jacques 3.8  
 5 Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.Deutéronome 18.11  Esaïe 19.3  Jérémie 8.17  
 6 Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.
Psaumes 3.7  Job 29.17  Nombres 23.24  Job 4.10-4.11  Ezéchiel 30.21-30.26  
 7 Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.
Psaumes 112.10  Josué 7.5  Esaïe 13.7  Psaumes 64.3  Josué 2.9-2.11  
 8 Kama konokono ayeyukaye na kutoweka, Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,
Job 3.16  Ecclésiaste 6.3  Jacques 1.10  Psaumes 37.35-37.36  Matthieu 24.35  
 9 Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, Ataipeperusha kama chamchela, Iliyo mibichi na iliyo moto.
Psaumes 118.12  Proverbes 10.25  Ecclésiaste 7.6  Job 20.5-20.29  Jérémie 23.19  
 10 Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.
Psaumes 68.23  Psaumes 64.10  Psaumes 107.42  Apocalypse 19.1-19.6  Deutéronome 32.43  
 11 Na mwanadamu atasema, Hakika iko thawabu yake mwenye haki. Hakika yuko Mungu Anayehukumu katika dunia.
Esaïe 3.10  Psaumes 67.4  Psaumes 96.13  Psaumes 9.16  Malachie 3.14