Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 47.3
Bible en Swahili de l’est


La souveraineté de Dieu

1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.
Psaumes 98.4 Esaïe 55.12 Psaumes 46.1 2 Rois 11.12 1 Samuel 10.24
2 Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.
Psaumes 68.35 Deutéronome 7.21 Malachie 1.14 Psaumes 99.3 Psaumes 65.5
3 Atawatiisha watu wa nchi chini yetu, Na mataifa chini ya miguu yetu.
Psaumes 18.47 Psaumes 81.14 1 Corinthiens 15.25 Psaumes 110.1 Josué 21.44
4 Atatuchagulia urithi wetu, Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.
1 Pierre 1.4 Nahum 2.2 Amos 6.8 Amos 8.7 Osée 14.4
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu.
Psaumes 68.33 Psaumes 150.3 Psaumes 24.7-24.10 2 Samuel 6.15 Josué 6.5
6 Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.
Matthieu 25.34 1 Chroniques 16.9 Zacharie 9.9 Psaumes 68.4 1 Chroniques 29.20
7 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa akili.
Zacharie 14.9 Colossiens 3.16 1 Corinthiens 14.14-14.15 Psaumes 47.2 Psaumes 47.8
8 Mungu awamiliki mataifa, Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.
1 Chroniques 16.31 Psaumes 97.1 Psaumes 48.1 Psaumes 94.20 Hébreux 4.16
9 Wakuu wa watu wamekusanyika, Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu. Maana ngao za dunia zina Mungu, Ametukuka sana.
Psaumes 89.18 Romains 4.11-4.12 Psaumes 72.11 Esaïe 66.19-66.20 Esaïe 49.23

Cette Bible est dans le domaine public.