Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 4.4
Bible en Swahili de l’est


La sécurité qu’accorde l’Éternel

1 Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.
Psaumes 18.18-18.19 Exode 34.6-34.7 Psaumes 17.6 Habakuk 3.19 Job 36.16
2 Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka? Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo?
Osée 4.7 Psaumes 5.6 Psaumes 3.3 1 Samuel 12.21 Ephésiens 4.25
3 Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa; Bwana atasikia nimwitapo.
2 Pierre 2.9 Psaumes 55.16-55.17 Psaumes 56.9 Tite 2.14 2 Timothée 2.19
4 Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.
Ephésiens 4.26 Psaumes 77.6 2 Corinthiens 13.5 Psaumes 63.6 Psaumes 46.10
5 Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana.
Psaumes 37.3 Deutéronome 33.19 Psaumes 62.8 Psaumes 51.19 Psaumes 26.1
6 Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema? Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.
Psaumes 80.7 Psaumes 80.19 Nombres 6.26 Psaumes 89.15 Psaumes 67.1
7 Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.
Esaïe 9.3 Psaumes 63.2-63.5 Cantique 1.4 Juges 9.27 Actes 14.17
8 Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.
Psaumes 3.5 Lévitique 25.18-25.19 Lévitique 26.5 Deutéronome 12.10 Psaumes 16.8-16.9

Cette Bible est dans le domaine public.