Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 39.3
Bible en Swahili de l’est


La fragilité de l’homme

1 Nalisema, Nitazitunza njia zangu Nisije nikakosa kwa ulimi wangu; Nitajitia lijamu kinywani, Maadamu mtu mbaya yupo mbele yangu.
1 Rois 2.4 2 Rois 10.31 Job 2.10 Psaumes 119.9 1 Chroniques 16.41
2 Nalikuwa sisemi, nalinyamaa kimya, Sina faraja, maumivu yangu yakazidi.
Matthieu 27.12-27.14 Actes 4.20 Psaumes 38.13-38.14 Job 32.19-32.20 Esaïe 53.7
3 Moyo wangu ukawa moto ndani yangu, Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka; Nalisema kwa ulimi wangu,
Jérémie 20.9 Luc 24.32 Ezéchiel 3.14
4 Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; Nijue jinsi nilivyo dhaifu.
Psaumes 90.12 Psaumes 119.84 Psaumes 103.14 Job 14.13
5 Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri; Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako. Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.
Psaumes 62.9 Psaumes 89.47 Psaumes 144.4 Psaumes 90.9-90.10 Ecclésiaste 1.2
6 Binadamu huenda tu huko na huko kama kivuli; Hufanya ghasia tu kwa ajili ya ubatili; Huweka akiba wala hajui ni nani atakayeichukua.
Luc 12.20-12.21 1 Corinthiens 7.31 Ecclésiaste 2.26 Ecclésiaste 5.14 Job 27.16-27.17
7 Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana? Matumaini yangu ni kwako.
Psaumes 38.15 Romains 15.13 Psaumes 130.5-130.6 Psaumes 119.81 Genèse 49.18
8 Uniokoe na maasi yangu yote, Usinifanye laumu ya mpumbavu.
Psaumes 44.13 Psaumes 79.4 Psaumes 51.14 2 Samuel 16.7-16.8 Michée 7.19
9 Nimenyamaza, sitafumbua kinywa changu, Maana Wewe ndiwe uliyeyafanya.
Job 2.10 2 Samuel 16.10 1 Samuel 3.18 Psaumes 38.13 Job 40.4-40.5
10 Uniondolee pigo lako; Kwa uadui wa mkono wako nimeangamia.
Job 9.34 Job 13.21 Psaumes 25.16-25.17 Job 40.8 Psaumes 38.3-38.4
11 Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake, Watowesha uzuri wake kama nondo. Kila mwanadamu ni ubatili.
Job 13.28 Esaïe 50.9 Job 4.19 Apocalypse 3.19 Job 30.30
12 Ee Bwana, usikie maombi yangu, Utege sikio lako niliapo, Usiyanyamalie machozi yangu. Kwa maana mimi ni mgeni wako, Msafiri kama baba zangu wote.
1 Pierre 2.11 Hébreux 11.13 Genèse 47.9 Psaumes 119.19 1 Chroniques 29.15
13 Uniachilie nikunjuke uso, Kabla sijaondoka nisiwepo tena.
Job 14.10-14.12 Job 10.20-10.21 Genèse 5.24 Genèse 42.36 Job 7.19

Cette Bible est dans le domaine public.